Makapuku Forum

Makapuku Forum

| Andreas Perreira FLAMENGO
.
Klabu ya Manchester United imemtoa kwa mkopo kiungo Andreas Perreira kwenda Flamengo ya Brazil
.
Pereira mwenye umri wa miaka 25 amecheza michezo 75 akiwa na uzi wa Mashetani wekundu na amefanikiwa kutupia wavuni magoli 4.
Screenshot_20210821-210909_GBInsta.jpg
 
Kiumri umekuwa mtu mzima, lakini haimaanishi ushiriki tendo la ndoa. Kama ulivyoliita ni tendo la ndoa na wewe hujaolewa pengine unasoma hivyo jipe muda wakati ukifika utashiriki mpaka uchoke.

Hao wanaokuona una matatizo kisa hujaanza kujamiiana hawana hekima na wanachangia kwa kiasi kikubwa mmomonyoko wa maadili.

Kujamiiana wakati ukifika kuna faida zake kitaalamu, ikiwamo kupata mtoto kwa waliojaaliwa. Lakini ukilazimisha kufanya hivyo kabla ya wakati madhara ni makubwa, ikiwamo kupata mimba za utotoni na maradhi ya zinaa ukiwamo Ukimwi.
Hii inatokana na unapokuwa na umri mdogo unakosa weledi wa kupambanua mambo hivyo kuingia katika masuala hayo bila tahadhari.

Usikimbilie kujiingiza huko, mambo hayo yalikuwepo tangu enzi na enzi na yataendelea kuwepo, muhimu ni kutulia hadi upate mwenza wako wa halali ule ufurahi naye kwa amani na salama.
Screenshot_20210822-122051_GBInsta.jpg
 
Ulimwengu unawatazama Taliban kama watu hatari na haushangazwi jinsi walivyoichukua Afghanistan na kuiweka kwenye himaya yao, bali unastaajabishwa na namna ilivyokuwa rahisi kuliteka Taifa hilo.

Wengi wanataka kujua Taliban ni akina nani, walikotoka na kiwango cha nguvu zao, lakini swali mama ambalo wengi wanajiuliza, wanaweza vipi kuitesa Marekani?

Historia ya kuanzishwa na kukua kwa Taliban kunahusisha msaada wa mataifa mawili; Marekani na Pakistan. Naam, Marekani wanateswa na kinyago chao wenyewe. Si kwamba Marekani ilisaidia moja kwa moja, bali kwa mlango wa nyuma.

Nguvu kubwa ya Marekani katika kuidhoofisha Dola ya Umoja wa Nchi za Sovieti (USSR) ndiyo sababu ya kuibuka kwa Taliban.
Screenshot_20210822-122249_GBInsta.jpg
 
Mwili wa mwalimu Alex Kashasha aliyefariki dunia Agosti 19, 2021 katika Hospitali ya Kairuki jijini Dar es Salaam alipokuwa anapatiwa matibabu, unafanyiwa ibada leo Agosti 22, 2021 katika maeneo ya Buza, Dar es Salaaam na mazishi yatafanyika kesho.
Screenshot_20210822-122427_GBInsta.jpg
 
Zoezi la Utoaji wa chanjo ya UVIKO-19 kwa wananchi likiwa linaendea hapa katika viwanja vya Uhuru Temeke jijini Dar es salaam likiongozwa na mkuu wa mkoa wa dar-es-salaam Mhe.Enock Makalla
Screenshot_20210822-122634_GBInsta.jpg
Screenshot_20210822-122654_GBInsta.jpg
Screenshot_20210822-122713_GBInsta.jpg
 
Mazoezi ya kutatanisha ambayo hufanywa na wanajeshi wa US na Thailand ya kunywa damu ya nyoka na kula Viumbe hatarishi kama N'ge, zoezi hili la kijeshi huitwa Cobra Gold hufanywa kila mwaka, kwa mwaka huu yamesitishwa amri toka PETA.

Mazoezi haya hufanywa ikiwa ni njia ya kuongeza ustadi wa kijeshi hasa wakiwa msituni kozi hiyo ya siku 10 inajumuisha masomo ya viumbehai wa msituni kwa kutumia nyoka, nge na geckos. Mafunzo ya kikambi ya wanyama yamekuwa sehemu zenye kumbukumbu za mazoezi, na picha na video za shughuli za umwagaji damu mara nyingi hutolewa kila mwaka.

PETA [people for the Ethical Treatment of Animal] ilisema unywaji damu wa nyoka umesitishwa kwa programu baada ya kampeni ya kumaliza mazoezi, ambayo ilijifunza tu mwaka jana. Kikundi cha haki za wanyama kilipinga nje ya Pentagon huko Washington, kiliwasiliana na Jeshi la Wanamaji la Amerika, na kutuma barua kwa waziri mkuu wa Thailand.

Mafunzo ya Cobra Gold yalifanyika kwa mara ya kwanza nchini Thailand mnamo 1982 ili kuboresha uhusiano kati ya vikosi vya jeshi la Amerika na Thailand, ambapo sasa wanaushirika mkubwa. Mpango huo umepanuka na kushirikisha nchi 29 pamoja na Indonesia, Malaysia, Singapore na Korea Kusini..
Screenshot_20210822-122847_GBInsta.jpg
Screenshot_20210822-122904_GBInsta.jpg
 
Mchungaji wa kanisa la Zion (22) nchini Zambia James Sakara, aliyewaomba baadhi ya waumini wake wamchimbie kaburi na kisha wamzike akiwa hai kwa madai ya kwamba baada ya siku tatu angefufuka kama Yesu, amekutwa akiwa amefariki dunia.
Screenshot_20210822-123033_GBInsta.jpg
 
Mwenda 2:3 - Naye Mwenda akamuuliza kijana wa Rabat nkufanye nini, kijana wa Rabat kwa hekima kubwa akajibu Nifanye utakavyo eewe bwana : Basi Mwenda akamuacha kijana wa Far Rabat akigalagala na kuenda zake.
Screenshot_20210822-123658_GBInsta.jpg
 
Nuno akiwa na Spurs anakutana na timu yake ya zamani Wolverhampton Wonderers? Vipi atatoboa?
.
Lukaku anarudi Chelsea na mechi yake ya kwanza itakuwa dhidi ya the Gunners. Vipi Arteta ataweza rudisha Tumaini la Asernal au ndio jahazi litazidi kuzama.
.
Karata ya pili kwa Manchester United wakiwa ugenini.
Screenshot_20210822-123814_GBInsta.jpg
 
Aubameyang kuivaa Chelsea
.
Habari njema kwa the Gunners ni kurejea kwa Pierre Emerick Aubameyang ambaye hakucheza mechi ya kwanza .
.
Leo Jumapili Arsenal ina kibarua cha kusaka pointi tatu mbele ya Chelsea na utakuwa ni mchezo wa pili kwenye Ligi Kuu England wakiwa na kumbukumbu ya kufungwa mabao 2-0 dhidi ya Brentford kwenye mchezo wa kwanza.
.
Arsenal wametoa taarifa kwamba mchezaji huyo walikuwa na corona hata kabla ya mchezo wa wikiendi iliyopita lakini atakuwepo kwenye mchezo wa leo baada ya kupimwa na kukutwa hana virusi huku wengine wawili Lacazette na Runarsson bado hawajawa fiti.
Screenshot_20210822-124113_GBInsta.jpg
 
AGUERO AKATAA JEZI YA MESSI
.
Sergio Aguero ni mchezaji mwingine kwenye kikosi cha Barcelona kukataa jezi Namba 10 iliyokuwa ikivaliwa na supastaa wa Kiargentina, Lionel Messi.
.
Sasa jezi hiyo haina mtu huko Nou Camp baada ya Messi kuondoka bure mwanzoni mwa mwezi huu kwenda kujiunga wa PSG kwa mkataba wa miaka miwili.
.
Aguero alikuwa akivaa Namba 10 klabuni Man City, lakini alikataa kuvaa jezi yenye namba kama hiyo huko Barcelona alipopewa, akiheshimu mafanikio ya swahiba wake, Messi.
.
Mchezaji mwingine aliyekataa jezi hiyo ni kiungo wa Kibrazili, Philippe Coutinho ambaye alipewa nafasi ya kuvaa.
Screenshot_20210822-124222_GBInsta.jpg
 
Solskjaer aweka jina la Mbappe United
.
Staa wa Paris St-Germain , Kylian Mbappe, 22, yupo kwenye orodha ya wachezaji ambao Manchester United inafikiria kuwasajili katika dirisha lijalo la majira ya kiangazi.
.
Man United ambayo ilihusishwa kuwa kwenye harakati za kuiwania saini ya Erling Haaland katika dirisha hili na ikashindwa kumpata, inahitaji kupata straika bora atakayeweza kuitumikia timu hiyo kwa muda mrefu kuanzia msimu ujao.
.
Eneo la ushambulaji ambalo msimu huu amesajiliwa Jadon Sancho ili kuongeza nguvu halionekani kuwa na makali sana ukizingatia Ednson Cavani umri unazidi kumtupa mkono, vilevile mastaa wengine kama Murcus Rashford na Antony Martial wamekuwa hawaonyesha kiwango kile kinachohitajika.
Screenshot_20210822-124617_GBInsta.jpg
 
"Nimeiona Simba yenye mabadiliko kwenye kikosi, wachezaji wenye umri mdogo na wenye morali ya kuipambania timu, kuna mfungaji wa bao la pili (Sakho) ni mchezaji bora sana nadhani atakuwa na mchango mkubwa kwenye timu.
Screenshot_20210822-124807_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom