Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kwa mujibu wa fivethirtyeight Hivi hapa ndo vilabu vinapewa nafasi ya kubeba ubingwa wa LALIGA msimu huu
.
Barcelona - 44%
Real Madrid - 26%
Atletico Madrid - 16%
Sevilla - 06%
Real Sociedad - 03%
Villarreal - 01%
Screenshot_20210820-184742_GBInsta.jpg
Screenshot_20210820-184904_GBInsta.jpg
Screenshot_20210820-184920_GBInsta.jpg
Screenshot_20210820-184936_GBInsta.jpg
Screenshot_20210820-184952_GBInsta.jpg
 
RASMI!

Mabingwa wa nchi Simba SC wamemtambulisha kiungo wa Mali Sadio Kanoute (24) kwa kandarasi ya miaka mitatu kutoka kwa miamba ya Libya Al Ahly Benghazi kwa takribani dola za Kimarekani 150,000.

Kanoute alikuwa mmoja wa nyota wa kikoso cha Mali kwenye mashindano ya CHAN 2020 huko Cameroon.
Screenshot_20210820-185235_GBInsta.jpg
 
Anchelotti kumbakiza Bale Madrid
.
Staa wa klabu ya Real Madrid na timu ya taifa ya Wales Gareth Bale, hana mpango wa kuondoka katika dirisha hili baada ya kocha wa timu hiyo Carlo Ancelotti, kuonyesha nia ya kuhitaji kumtumia zaidi katika kikosi chake ambacho kimepoteza nahodha Sergio Ramos na beki Varane Raphael.
.
Bale mwenye umri wa miaka 32 Mkataba wake unaisha 2022.
Screenshot_20210820-185344_GBInsta.jpg
 
Aouar akaribia kuitosa Arsenal, kutua Spurs
.
Tottenham ipo tayari kutoa Pauni 30 milioni ili kuipata saini ya kiungo wa Olympique Lyon, Houssem Aouar katika dirisha hili.
.
Staa huyu alikuwa anawindwa sana na Arsenal ambayo imeonekana kushindwa kuipata saini yake kutokana na kushindwa kutoa kiasi cha pesa kilichohitajika na Lyon. Mkataba wake unamalizika mwaka 2023.
.
Nuno ameonekana kuhitaji huduma ya fundi huyo kwa asilimia nyingi kwani anaamini ikiwa atasainishwa ataenda kuongeza nguvu kwenye eneo la ushambuliaji la Spurs hata Harry Kane akiondoka kwenye dirisha hili.
Screenshot_20210820-185446_GBInsta.jpg
 
CONFIRMED | Klabu ya FAR Rabat ya Morocco inayonolewa na kocha wa zamani wa Simba, Sven Vamdenbroeck imethibitiha kuwa kesho Jumamosi itacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Mabingwa wa nchi, Simba SC.
.
Mechi hiyo inatarajiwa kupigwa saa 10 jioni za Morocco sawa na saa 12 kwa Tanzania.
.
Sven alikuwa na Simba kabla ya kuwakacha na kutua kwenye timu hiyo ya Morocco ndipo wakambeba Didier Gomes akawapa makombe mawili VPL na FA
.
Screenshot_20210820-185656_GBInsta.jpg
 
Liverpool huenda ikaachana na mpango wake wa kuiwania saini ya kiungo wa Lille na timu ya taifa ya Ureno, Renato Sanches, 24, baada ya fundi huyo kupatwa na majeraha yanayoweza kumuweka nje kwa zaidi ya wiki sita.
.
Mkataba wake unamalizika mwaka 2023. Mbali ya Liver, Barca pia ilihusishwa kumhitaji.
Screenshot_20210820-185800_GBInsta.jpg
 
Nuno juu ya Harry Kane : "Anajisikia vizuri. Anazidi kuwa fiti kila siku. Yuko tayari kujumuika na wenzake kutoka hapo tutafanya uamuzi kama acheze mechi ya Jumamosi dhidi ya Wolves."

Screenshot_20210820-185902_GBInsta.jpg
 
Serikali ya China sasa itawaruhusu Wanandoa kuzaa Watoto watatu kwani inahofia Taifa hilo kuwa na idadi ndogo ya Watu hali itakayotishia mipango yake ya kukuza maendeleo na ushawishi ulimwenguni ambapo jana Ijumaa Bunge lilirekebisha sheria ya idadi ya Watu na uzazi wa mpango.

Hii imekuja miaka sita tangu kufanyika kwa mabadiliko ya mwisho yaliyoruhusu Wazazi kuzaa watoto wawili ambapo tangu miaka ya 1980 China ilikuwa ikiruhusu familia kuzaa Mtoto mmoja tu na hiyo ilisababisha baadhi ya Wazazi kutoa mimba huku wengine waliotaka Mtoto huyo mmoja awe wa kiume wakiwaua Watoto wao wa kike kitu ambacho kilisababisha tofauti kubwa katika uwiano wa kijinsia nchini humo.

Japan na Ujerumani ni Nchi nyingine tajiri zinazokabiliwa na changamoto sawa na hiyo ya kuwa na Wafanyakazi wachache Vijana huku idadi kubwa ya ikiwa ni Wazee.
Screenshot_20210821-201931_GBInsta.jpg
 
Spika wa Bunge, Job Ndugai ameamuru Wabunge wawili Josephat Gwajima na Jerry Silaa kupelekwa mbele ya Kamati ya Maadili na Madaraka ya Bunge ili kujibu tuhuma mbalimbali ikiwemo kusema uongo na kushusha hadhi na heshima ya Bunge.

Gwajima anatakiwa kufika mbele ya Kamati hiyo Jumatatu August 23,2021 saa saba mchana na Silaa anatakiwa kufika Jumanne August 24,2021.

“Endapo yeyote kati ya Gwajima na Silaa hatofika mbele ya Kamati hiyo kwa siku na muda uliotajwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa”.
Screenshot_20210821-202225_GBInsta.jpg
 
Rais wa Marekani Joe Biden ameapa kuwa atawarejesha nyumbani Raia wote wa Marekani kutoka nchini Afghanistan pamoja na Waafghani waliosaidia juhudi za Nchi yake kwenye vita vya karibu miaka 20.

Biden ametoa ahadi hiyo alipozungumza na waandishi habari mjini Washington wakati hatma ya maelfu ya Wamarekani waliokwama kwenye uwanja wa ndege mjini Kabul ikiwa bado haijulikani.

Hadi kufikia sasa ni Watu 5,700 pekee ikiwemo Wamarekani 250 ndio wameondoshwa nchini Afghanistan na kupelekwa kwenye vituo vya muda vilivyoandaliwa kwenye mataifa jirani.

Utawala wa Biden unaandamwa na ukosoaji mkubwa nyumbani kutokana na kuchukua hatua za polepole za kuwahamisha Raia wake tangu kundi la Taliban lilipoukamata mji mkuu wa Afghanistan, Kabul siku kadhaa zilizopita.
Screenshot_20210821-202513_GBInsta.jpg
 
KOCHA wa Yanga amewaangalia vijana wake akawaambia mashabiki kwamba; “sasa hii ndiyo Yanga niliyoitaka.”

Akizungumza na Mwanaspoti ambalo ndilo gazeti pekee la Tanzania liliko nchini Morocco, Kocha Nesreddine Nabi alisema usajili ambao umefanywa na matajiri wao wa GSM umemfurahisha na sasa amepata timu sahihi itakayokuwa na sura sahihi ya kupigania mataji.
Screenshot_20210821-205222_GBInsta.jpg
 
Baada ya kuanza Ligi Kuu England kwa kichapo dhidi ya Tottenham kwa bao 1-0 leo wamelipiza kisasi kwa kumpiga Norwich -

MATOKEO MENGINE

Leeds 2-2 Everton
Aston Villa 2-0 Newcastle United
Crystal Palace 0-0 Brentford
Liverpool 2-0 Burnley
Screenshot_20210821-205632_GBInsta.jpg
 
LUIS, TAU AL AHLY
.
Percy Tau (27) na Luis Jose Miquissone watawasili jijini Cairo wiki ijayo kukamilisha dili la kujiunga na Al Ahly
.
Tau anaripotiwa kujiunga na mabingwa hao wa Afrika kwa dau la Euro milioni 1.8 (Bilioni 4.9) na Miquissone kwa Euro 900,000 (Sh bilioni 2.4).
Screenshot_20210821-210544_GBInsta.jpg
 
Kiungo wa Manchester United na England, Jesse Lingard, 28, ana asilimia nyingi za kuondoka katika dirisha hili kwani kocha wa timu hiyo haonekani kuwa tayari kumtumia kama mchezaji tegemeo kwenye kikosi cha kwanza.
.
Lingard amesisitiza kuwa ili abaki lazima ahakikishiwe namba.
Screenshot_20210821-210809_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom