Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,978
“Kumekuwa na maneno yanaendelea kwamba kuna uwezekano wa kufuta Elimu ya msingi bila ada, sio kweli ni uzushi, Serikali itaendelea kutoa fedha kugharamia Elimu ya Msingi na Sekondari na tayari mwezi huu tumeshapokea zaidi ya Tsh. Bilioni 200, sera ya Elimu bila ada itaendelea kutekelezwa na sisi tutaendelea kusimamia”
“Nimetambulishwa hapa kama mnufaika na nakiri TAMISEMI imepokea kutoka hazina Tsh. Bilioni 22 .5 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya 90 na vitajengwa katika Halmashauri 82 za Tanzania Bara, fedha hizi tayari zmeshafika kwenye akaunti za Halmashauri husika, zitajenga vituo vya afya Katika tarafa ambazo hazina vituo vya afya”
“Nitoe maelekezo kwa Wakuu wa Mikoa kupitia Sekretarieti za Mikoa kuhakikisha vituo hivi vya afya vinajengwa katika Makao Makuu ya Tarafa ambayo hazina vituo vya afya, na kama kwenye Tarafa kuna Hospitali ya Halmashauri fedha zipelekwe kwenye kata ya kimkakati ambayo haina kituo cha afya”
“Nasisitiza Wakurugenzi wa Halmashauri fedha hizi zikajenge majengo mapya sio kuleta ujanjaujanja wa ukarabati, sisi TAMISEMI tutasimamia kikamilifu matumizi ya fedha hizi na nawataka Wakuu wa Mikoa wasimamie matumizi ya fedha hizi, kuna ongezeko la Wanafunzi lakini pia nako tumepata fedha za kujenga madarasa 560 kutoka kwenye Bilion 7 ambayo Waziri Mwigulu ameahidi kutupa” ———-Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu
“Nimetambulishwa hapa kama mnufaika na nakiri TAMISEMI imepokea kutoka hazina Tsh. Bilioni 22 .5 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya 90 na vitajengwa katika Halmashauri 82 za Tanzania Bara, fedha hizi tayari zmeshafika kwenye akaunti za Halmashauri husika, zitajenga vituo vya afya Katika tarafa ambazo hazina vituo vya afya”
“Nitoe maelekezo kwa Wakuu wa Mikoa kupitia Sekretarieti za Mikoa kuhakikisha vituo hivi vya afya vinajengwa katika Makao Makuu ya Tarafa ambayo hazina vituo vya afya, na kama kwenye Tarafa kuna Hospitali ya Halmashauri fedha zipelekwe kwenye kata ya kimkakati ambayo haina kituo cha afya”
“Nasisitiza Wakurugenzi wa Halmashauri fedha hizi zikajenge majengo mapya sio kuleta ujanjaujanja wa ukarabati, sisi TAMISEMI tutasimamia kikamilifu matumizi ya fedha hizi na nawataka Wakuu wa Mikoa wasimamie matumizi ya fedha hizi, kuna ongezeko la Wanafunzi lakini pia nako tumepata fedha za kujenga madarasa 560 kutoka kwenye Bilion 7 ambayo Waziri Mwigulu ameahidi kutupa” ———-Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu
Kanoute yuko tayari kuwapa furaha Wanasimba. 
ARSENAL 
AS FAR RABAT
SIMBA SC 
Jumamosi | 21/08
12 Jioni.
Centre Sportif
| Marco Asensio