Mikono ya farhan jr
Huyo pichani ni YUSUPH MHILU, nyota wa zamani wa Kagera Sugar ambaye sasa yupo SIMBA
Well kwenye nchi yetu tuna vitu viwili SIGNING FEE na TRANSFER FEE, Mchezaji akiwa na mkataba basi utafanya vyote viwili
SIGNING FEE, ni ada ya kusaini! Hii anachukua Mchezaji mwenyewe na Simba walikubaliana kila kitu na Kijana na akapewa kinachomuhusu
TRANSFER FEE, hii ilipaswa alipwe Kagera kwakuwa Mchezaji alikuwa na mkataba wa mwaka mmoja! Hii ni ada ya uhamisho, hapo sasa ni Simba vs Kagera
Anyways tuachane na hapo juu! Lakini kwenye Transfer Fee inategemea na vipengele vya kimkataba kati ya Mchezaji na klabu yake!
Hapo kuna kitu kinaitwa RELEASE CLAUSE! Picha lipo hapa, kwenye hii mkataba unasema ili Yusuph aondoke anapaswa kulipa Mshahara wa miezi ya kimkataba ambayo ni 12 zidisha kwa Mshahara
Ukifanya hivyo unakuwa umenunua mkataba wake na anakuwa huru kujiunga na timu yako
Ule utata mdogo ulikuwa Simba kusimamia kipengele cha mkataba (Release Clause) ambayo haikuwa kubwa kuliko ada ya uhamisho inayotakiwa