Mkono wa farhan jr
Kuna maswali mawili kwenye issue ya Luis Miquisson na Clatous Chama! Nadhani ni maswali mepesi sana yanayojibika kirahisi sana
Kwanini Simba hawajataja timu walizoenda?
Jibu jepesi hapo ni PRINCIPLE OF CONFIDENTIALITY na EXCLUSIVITY! Klabu kama Al Ahly na RS Berkane wana namna yao ya kutangaza wachezaji wao
Wana haki ya kupewa exclusive, hapo Simba amewaheshimu wanunuzi wake ili wabaki na exclusive zao kwakuwa biashara haitoishia hapa! Huo ndio weledi wa klabu kubwa, Simba wana kosa gani hapo?
Kwanini hawajataja bei? Ni hapo hapo Confidential kuna kitu kinaitwa UNDISCLOSED FEE! Nitajieni klabu inayotaja bei iliyouza Mchezaji wake duniani ni ipi
Sasa kwanini Simba wakatangaza kwa kutumia Public notice?
Well, jibu jepesi sana wiki chache zijazo majina ya wachezaji wapya yatatangazwa, Simba ametoa taarifa kufuta taharuki pale ambapo majina ya wachezaji hao yasipoonekana, kuna kosa kwa klabu kufuta taharuki?
Taarifa zimeshasambaa mitandaoni ikiwemo na picha za Wachezaji mfano Chama akiwa Berkane, sasa klabu kutoa taarifa ina ubaya gani
Lastly watu wanahoji mkataba wa SIMBA na Luis Miquisson, kuna tatizo?
Kama Miquisson sio Mchezaji wa Simba, well nani katoa taarifa ya Mchezaji kuondoka? Wametoa UD SONGO? wametoa MAMELODI SUNDOWNS? jibu ni kuwa wametoa SIMBA
Miquisson alisaini kandarasi ya miaka mitatu na nusu! Amecheza mwaka mmoja na nusu, Chama alikuwa na mkataba wa miaka miwili
Mkitaka kupata taarifa sahihi wala msipende sana kutumia WIKIPEDIA, anyone can edit