Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais Joe Biden wa Marekani amezungumza leo baada ya Wanamgambo wa Taliban kuiweka Nchi mikononi mwao siku chache baada ya Majeshi ya Marekani kuondolewa Nchini humo.

Biden amewajibu wanaosema amekosea kuyaondoa Majeshi ya Marekani Nchini Afghanistan kwa kusema Wanajeshi wa Marekani hawatakiwi na hawatotakiwa kupigania vita na kufa kwenye vita ambayo Wanajeshi wa Afghanistan wenyewe hawajitoi kuipigania Nchi yao.

Ameitoa kauli hiyo kutokana na baadhi ya Wanajeshi wa Afghanistan kujisalimisha kwa Wanamgambo wa Taliban na kuwarahisishia Wanamgambo kuiweka Nchi mikononi mwao.

Rais Biden pia amesema Wanajeshi wa Afghanistan walipewa mafunzo na Marekani na kila kitu walichohitaji kwenye vifaa vya kijeshi hata jeshi la anga lakini wameshindwa kupambana na Wanamgambo hao ambao hawana Jeshi la anga.
Screenshot_20210817-062531_GBInsta.jpg
 
Rais Biden pia amesema Wanajeshi wa Afghanistan walipewa mafunzo na Marekani na kila kitu walichohitaji kwenye vifaa vya kijeshi hata jeshi la anga lakini wameshindwa kupambana na Wanamgambo wa Taliban ambao hawana Jeshi la anga.
Screenshot_20210817-062904_GBInsta.jpg
 
Marekani imewaonya Wanamgambo wa Taliban kutofanya shambulizi lolote au kuingilia utaratibu wake wa kuwaondoa Watu Nchini Afghanistan na kama wakifanya hivyo basi Marekani itafanya juu chini kujibu mashambulizi kwa lengo la kuwalinda Watu wake, tayari Ubalozi wa Marekani Nchini humo umefungwa na Watu wote wameondolewa na kuwekwa uwanja wa Ndege wa Kabul ambao uko chini ya Jeshi la Marekani.
Screenshot_20210817-063248_GBInsta.jpg
 
Serikali imemuonya Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima na Mbunge wa jimbo la Kawe, Askofu Josephat Gwajima kwa kile kinachodaiwa kuwa anaupotosha umma kuhusu chanjo ya Uviko - 19
Screenshot_20210817-064209_GBInsta.jpg
 
Wakati Serikali ikitoa takwimu za waliopata chanjo ya Uviko-19 kuwa 207,391, baadhi ya watu ambao hawajachanjwa katika nchi kadhaa duniani wameanza kukosa huduma mbalimbali.

Miongoni mwa huduma hizo ni safari za kimataifa, kazi, utoaji huduma katika migahawa, hospitali, masoko ya ndani ‘supermakert’.

Machi mwaka huu, Saudi Arabia ilitangaza kuwa waumini wa dini ya Kiislamu watakaoruhusiwa kuhudhuria ibada ya Hijja kwa mwaka 2021 wanapaswa kuthibitisha kuwa wamepatiwa chanjo dhidi ya Uviko-19.

Tayari nchi 27 zinazounda Jumuiya ya Ulaya zimeshakubaliana pasi na chanjo mtu hatoruhusiwa kuingia kwa nchi mwanachama.

Kwa nchi za Afrika Mashariki Kenya, Rwanda na Uganda kila moja imetoa masharti kwa wafanyakazi wawe mapata chanjo hiyo ndipo waruhusiwe kuendelea na kazi.
Screenshot_20210817-064209_GBInsta.jpg
 
Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Jacob Zuma ambaye anatumikia kifungo chake, amefanyiwa upasuaji na bado yuko hospitalini akiendelea na matibabu, maafisa wa magereza wamesema.

Hadi sasa hakuna taarifa yoyote kuhusu upasuaji huo au ni lini kiongozi huyo wa zamani anatarajiwa kutoka hospitalini.
Screenshot_20210817-070654_GBInsta.jpg
 
Televisheni ya Taifa Tanzania (TBC) leo imetangaza kifo cha Waziri wa Fedha wa zamani Basil Pesambili Mramba aliyefariki leo Aug. 17 akitibiwa kwenye Hospitali ya Regency Dar es Salaam.

Mramba alikua Waziri wa Fedha katika utawala wa Rais Mkapa mwaka 2001-2005 na baadae akawa Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko kwenye utawala wa Rais Kikwete 2006 - 2008.

Kwa mujibu wa TBC, Familia ya Mramba imethibitisha kutokea kwa kifo hicho na kusema ni Wanafamilia wachache wataruhusiwa kufika kutoa pole nyumbani kwa Marehemu Oysterbay Dar es Salaam.
Screenshot_20210817-141703_GBInsta.jpg
 
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dr. Faustin Ndugulile amesema Tanzania ina Watumiaji wa mitandao ya kijamii milioni 16.5 ambapo Facebook na Whatsapp ndio zinaongoza kwa kuwa na Watumiaji zaidi ya milioni sita wakati Instagram ikiwa na Watumiaji milioni 4.5.

Waziri Ndugulile amesema kwa usajili wa line kwa sasa ni zaidi ya milioni 50 na Watumiaji wa internet wakiwa takribani milioni 30 na wanaofanya miamala ya fedha ni zaidi ya milioni 32.

Dkt. Ndugulile ametoa tathmini hiyo wakati wa uzinduzi wa mfumo wa kielectroniki wa uratibu na ufuatiliaji wa shughuli za kiserikali utakaosaidia kuweka uwazi na uwajibikaji na kufikisha taarifa kwa umma.
Screenshot_20210817-141957_GBInsta.jpg
 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr. Doroth Gwajima ameliagiza Jeshi la Polisi na Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa ( TAKUKURU) kumkamata na kumhoji Mbunge wa Kawe Askofu Josephat Gwajima ili athibitishe kauli anazozitoa dhidi ya Serikali na Viongozi kuhusu chanjo ya covid-19.

Dr. Gwajima ametoa agizo hilo leo Jumanne Agosti 17, 2021 katika kijiji cha Kyatunge Butiama na kusema Askofu Gwajima amekuwa akitoa taarifa za kupotosha kwa makusudi jambo linaloivuruga Wizara yake na Serikali katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo.
Screenshot_20210817-142428_GBInsta.jpg
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemfutia kesi na kumwachia huru msanii wa vichekesho, Idris Sultani na wenzake wawili baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP) kuieleza mahakama hiyo kuwa hana nia ya kuendelea na shauri hilo.

Sultan na wenzake walikuwa wanakabiliwa na shtaka moja la kuchapisha maudhui mtandaoni bila kuwa na kibali.
Screenshot_20210817-143300_Instagram%20Lite.jpg
 
HATMA YA CRISTIANO RONALDO

"Hatma ya Cristiano Ronaldo inaweza ikabadilika muda wowote ndani ya siku 14 zijazo" Edu Aguirre, Rafiki wa karibu wa Cristiano Ronaldo
Screenshot_20210817-144836_GBInsta.jpg
 
Zlatan Ibrahimovic:

"Siipendi Chelsea, basi tu. Ni timu inayotumia makocha wawili katika msimu mmoja kabla ya kuweza kufanikiwa, kwangu hiyo sio timu. Chelsea ilinunua mafanikio kwa pesa, yani rahisi hivyo. "
Screenshot_20210817-145318_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom