Makapuku Forum

Makapuku Forum

MIKONO YA KIHAMU : NDOTO ZA SIMBA KUBEBA UBINGWA WA AFRIKA ZIONEKANE KWA VITENDO
.
"Pesa waliyouza Miquisson au Chama unaweza kuipata ukiingia makundi CAF, ukafuzu robo fainali mpaka nusu! Unaweza kuwa nayo, kwanini usilinde project?
.
"Leo hii Simba haanzi hatua za awali ni kutokana na ubora uliotokana na Wachezaji, ameokoa gharama nyingi hapo za tiketi na malazi! Unaona thamani inavyofanya kazi kuliko pesa ya muda mfupi?
.
"Leo hii Wadhamini wanapaswa kwenda kuweka pesa nyingi kutokana na ukubwa wa Simba uliotokana na ubora wa wachezaji, hatuoni kuna pesa kubwa inapatikana nyuma ya kulinda hii project?
.
"Dewji aliwahi kusema anahitaji Simba wabebe ubingwa Afrika, ila huo ni mchakato! Mchakato wa kufika robo mara nyingi, nusu kisha fainali sio muda mfupi
.
"Ndoto hizi zinapaswa kuonekana kwa vitendo, ikiwemo kulinda project kwa gharama kubwa! Uza wasio na umuhimu kisha ongeza saini muhimu, kikosi kiwe imara kama unaitaka Afrika
.
"Kuuza Wachezaji ni pesa ya muda mfupi, ni njia fupi ya kupata pesa ambayo mtakula kwa uchungu mkubwa! Binafsi nilidhani Simba walipaswa kulinda project yao ina thamani kuliko pesa
.
[@jr_farhanjr ]
Screenshot_20210813-154237_GBInsta.jpg
 
PIGO ARSENAL| Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta amethibitisha kuwa Washambuliaji wake tegemeo nahodha Pierre-Emerick Aubameyang na Alexandre Lacazette hawako fit na hawatacheza dhidi ya Brentford usiku wa leo
.
Muda wa stress kwa Mashabiki wa Arsenal umefika na msimu ndo kwanza unaanza
.
Screenshot_20210813-154537_GBInsta.jpg
 
Taarifa kwa mujibu wa tovuti ya MIRROR ni kuwa PSG tayari wameanza mpango wa kumnasa Cristiano Ronaldo mwishoni mwa msimuu huu kama Mchezaji huru

PSG wamekubali Kylian Mbappe kuondoka huru kuelekea Real Madrid msimu ujao ila wao watajipooza na saini ya Ronaldo

Ndoto ya Rais wa PSG ni kuwaona Ronaldo na Messi ndani ya timu moja na Wamiliki wameshaipitisha

Busy summer ahead of us next year View attachment 1890745
Wamezidi sasa
 
NANI KUONDOKA NA CROWN?

NI siku saba (7) pekee zimesalia kabla ya nchi kusimama kwa muda kupisha pambano kubwa la masumbwi, litakalowakutanisha mabondia nguli wa uzani wa Super Middle (Kg 76) nchini, Dullah Mbabe na Twaha Kiduku.

Wawili hao watakutana Ijumaa ijayo Agosti 20, katika ukumbi wa ubungo Plaza Dar es salaam, katika pambano lao la tatu la marejeano lililopewa jina la 'PAYBACK NIGHT' wakiwania gari ya kisasa aina ya Crown.

Dullah Mbabe ambaye alipoteza pambano lililopita lililowakutanisha wawili hao amesema:"Twaha sio bondia, Twaha ni mbeba vyuma tu, hawezi kuwa bondia, mashabiki wangu wasiwe na wasiwasi tutashinda mapema tu."

Kwa upande wake Twaha Kiduku, amesema:"Naendelea vizuri na mazoezi, naomba mashabiki wangu waniombee na wategemee ushindi, Dullah Mbabe ni bondia mzuri lakini tutashinda kwa uwezo wa mungu."

Kesho tarehe 14 mabondia hao watakutana kwenye zoezi la 'FACE OF OF' mjini Morogoro, ambapo kutakuwa na mapambano 12 yatakayopigwa, huku pambano la Joseph Mchapeni na Dani Mwanafyale likisubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa ngumi.
Screenshot_20210813-172044_GBInsta.jpg
 
Klabu ya Simba ni moja kati ya vilabu 10 bora Afrika vitakavyoepuka kuanzia hatua ya awali kwenye mashindano ya klabu bingwa Afrika kwa msimu wa 2021/22.

Orodha ya vilabu bora ni kama ifuatavyo

1. Al Ahly
2. Zamalek
3. Espérance
4. ES Sahel
5. Wydad Casablanca
6. Raja Casablanca
7. TP Mazembe
8. Mamelodi Sundowns
9. Horoya AC
10. Simba SC
Screenshot_20210813-172255_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom