Makapuku Forum

Makapuku Forum

David in Madrid

David Alaba kitasa kipya cha Real Madrid

Mbadala sahihi wa Sergio Ramos? Majibu yataanza kupatikana, weekend hii.
Screenshot_20210813-145457_GBInsta.jpg
 
There's no permanent friend, there's no permanent enemy there's only permanent interest

Hakuna Rafiki wa kudumu, hakuna adui wa kudumu bali kuna maslahi ya kudumu pekee

Lionel Messi na Sergio Ramos ni stori ya maadui waliobadilika na kuwa marafiki
Screenshot_20210813-150119_GBInsta.jpg
 
MIKONO YA KIHAMU @jr_farhanjr

Duniani kote Matajiri wakiwekeza kwenye timu ni ngumu kuwapa nafasi watu wa mpira moja kwa moja kwenye utendaji haswa mambo ya kifedha

Matajiri wanajihisi huru pale ambapo anakuwepo Afisa anaesimamia mambo, akiamini hawezi kumpigisha shoti bali kumpa taarifa sahihi

Watu walishawahi kukosoa Engineer Hersi pale Yanga kuwa na nguvu kubwa licha ya kuwa ni Mjumbe tu, lakini watu wanasahau ni Mkurugenzi wa Uwekezaji pale GSM ni mtu wa Boss

Watu waliwahi kuhoji uwepo wa Barbra pale Simba, wakasema hana analojua kuhusu mpira ndio inaweza kuwa sahihi lakini Boss ndie mtu anaemuamini, atapigania maslahi ya timu na yake binafsi

Hii sio Tanzania tu bali duniani kote! Maboss wanahitaji watu wao

Mfano Manchester United ile familia ya Glazer's ilimuamini sana Ed Woodward, Mtendaji na Mwandamizi kwenye masuala ya kiuchumi, watu walisema hana analojua kuhusu mpira lakini vitabu vilibalance sana

Mfano PSG wana Nasser El Kherrafi, yule sio Mmiliki wa timu bali ni Mwenyekiti na CEO wa timu, ni mtu wa karibu na Mmiliki wa PSG anaitwa Tamim Bin Hamad Al Thani, ila Nasser anasimamia kutokana na kusimamia projects nyingi za Boss

Mfano Chelsea wana Marina Granovskaia, hakuwahi kuushi mpira alikuwa Msimamizi wa biashara za Roman Abramovich, ila Tajiri alitaka Mtu wa kulinda maslahi yake, akamleta kwenye mpira, itazame Chelsea sasa kibiashara ni hatari

Huwezi kuwekeza kwenye mpira na ukaacha utendaji kwa Mtu ambaye sio wako, utalia kilio cha mbwa meno nje! Watu wa Maboss ni watu sahihi kulinda maslahi duniani kote
Screenshot_20210813-150315_GBInsta.jpg
 
Taarifa kwa mujibu wa tovuti ya MIRROR ni kuwa PSG tayari wameanza mpango wa kumnasa Cristiano Ronaldo mwishoni mwa msimuu huu kama Mchezaji huru

PSG wamekubali Kylian Mbappe kuondoka huru kuelekea Real Madrid msimu ujao ila wao watajipooza na saini ya Ronaldo

Ndoto ya Rais wa PSG ni kuwaona Ronaldo na Messi ndani ya timu moja na Wamiliki wameshaipitisha

Busy summer ahead of us next year
Screenshot_20210813-151415_GBInsta.jpg
 
MANE MASTERCLASS|

Hospitali hii imejengwa na Sadio Mane, kwa gharama za EURO 530,000 ikiwa sawa na billion 1.4 za Kitanzania

Ikumbukwe pia Mane amejenga shule hapo kijijini kwao Bambali.
Screenshot_20210813-151644_GBInsta.jpg
Screenshot_20210813-151708_GBInsta.jpg
Screenshot_20210813-151724_GBInsta.jpg
 
Kaimu Afisa Habari wa Simba Sports Club Ezekiel Kamwaga Athibitisha Kuuzwa Kwa Chama.

NI kweli kwamba nyota wetu mahiri, Clatous Chama amejiunga na timu ya RS Berkane ya Morocco na sisi kama uongozi tumeridhia kwa kuzingatia maslahi mapana ya mchezaji pamoja na klabu yetu ya Simba.

Na pia Fedha tulizopata kwa kumuuza Chama ni kubwa mno na tutazitumia kuboresha kikosi chetu.
Screenshot_20210813-152722_GBInsta.jpg
 
JUST IN |

Raisi wa PSG, Nasser Al Khelaifi sasa anaamini kwamba Kylian Mbappe hataongeza tena mkataba wa kubaki PSG, na amefikiria kumruhusu aende Real Madrid kabla ya 2022.
.
Tayari Bodi ya PSG imepitisha jina la mbadala wa wa Mbappe. Naye ni CRISTIANO RONALDO, ambaye mkataba wake na Juventus utamalizika msimu ujao.
Screenshot_20210813-153118_GBInsta.jpg
 
Chris Kope Mugalu FAR Rabat
.
Muda mchache uliopita Tovuti ya Goal imeripoti kuwa klabu ya FAR Rabat iko kwenye hatua ya mwisho kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa Simba, Chris Mugalu (31)
.
Rabat inayonolewa na Kocha wa zamani wa Simba, Sven Vandenbroeck "kishingo" imeongeza dau kutoka dola laki 4 hadi dola 450,000 (Sh bilioni 1)
Screenshot_20210813-153756_GBInsta.jpg
 
CONFIRMED|

Sadio Kanoute "fundi" SIMBA SC
.
Kiungo wa timu ya Taifa ya Mali na klabu ya Al Ahly Bengazi ya Libya, Sadio Kanoute (24) fundii tayari ame tua nchini ili kuja kuongeza nguvu katika eneo la kiungo la mabingwa wa nchi, SIMBA SC.
.
Ni suala la muda atatambulishwa rasmi kuwa MWEKUNDU.
.
Screenshot_20210813-153946_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom