Makapuku Forum

Makapuku Forum

Clatous Chama RS Berkane, FAR Rabat
Screenshot_20210812-173822_GBInsta.jpg
 
MOLOKO MIWILI YANGA
.
Mbadala wa Tuisila Kisinda, Jesus Moloko amesaini miaka miwili Yanga akitokea AS Vita ya DR Congo.
.
Moloko amesaini jana mbele ya mabosi wa Vita aliyoitumikia msimu uliopita na muda wowote ndani ya saa 24 kuanzia leo atatua nchini.
.
Tayari Yanga jana baada ya kuupokea tu mkataba wa Moloko wakamuingiza katika msafara wao unaoondoka Agosti 15 kwenda Morocco.
Screenshot_20210812-174302_GBInsta.jpg
 
Waziri, Makapu ndo basi tena Yanga
.
Yanga uhakika watatua jijini Casablanca Jumanne tayari kwa kambi yao ya maandalizi na wataondoka na mastaa wote isipokuwa Waziri Junior na Saidi Makapu.
.
Yanga itaondoka na msafara wa wachezaji 28 katika safari hiyo lakini taarifa zinasema ni wachezaji wawili tu hawamo katika orodha hiyo na hawatakuwa sehemu ya kikosi msimu ujao.
.
Wachezaji hao ni mshambuliji Waziri Junior na kiungo Said Makapu.
Screenshot_20210812-174427_GBInsta.jpg
 
DROO YA SIMBA, YANGA KIMATAIFA NI KESHO
.
Habari ndo hiyo. Shirikisho la Soka Afrika CAF limetangaza kuwa Droo ya michuano ya Kimataifa Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho itachezeshwa kesho Ijumaa jijini Cairo
.
Droo hiyo ndio itakayotoa washindani wa Simba, Yanga, Azam na Biashara.
.
Simba na Yanga zitashiriki Ligi ya Mabingwa Afrika huku Azam na Biashara zikienda Shirikisho Afrika.
Screenshot_20210812-174653_GBInsta.jpg
 
AZAM UELEKEO NI NDOLA ZAMBIA
.
Baada ya Simba na Yanga kutangaza kuweka kambi nchini Morocco, ripoti zinadai kwamba wababe wemzao, Azam FC wamewakwepa na kupanga kupiga kambi Zambia katika jiji la Ndola.
.
Azam tayari timu ipo kambimi tangu Jumatatu na Maandalizi hayo yamepagwa kuanza wiki ijayo kama mambo yataenda vizuri.
.
Inaelezwa kuwa Usajili wa wachezaji wa kigeni Azam tayari wamemaliza na sasa wako kwenye harakati za kunasa nyota wasiozidi watatu wa ndani kisha kwenda Zambia.
Screenshot_20210812-175432_GBInsta.jpg
 
Daniel Popa SIMBA SC
.
Mashine ya mabao kutoka Romania, Daniel Popa muda wowote wiki hii anatarajiwa kujiunga na mabingwa wa nchi, Simba SC baada ya kufikia makubaliano juu ya ada ya uhamisho.
.
Msimu uliopita wa 2020/21 katika Ligi kuu ya Romania mechi 27 kafunga mabao 15 na assist 4.
.
Kwa sasa, mazungumzo yanaendelea kuhusiana na mshahara wa Popa ambaye anaripotiwa kutaka zaidi ya sh milioni 250 kwa mwaka katika mkataba wa miaka mitatu.
Screenshot_20210812-175540_GBInsta.jpg
 
Banda apewa jezi ya Miquissone
.
Katika kile kinachoashiria safari ya Luis Miquissone kujiunga na Al Ahly ya Misri imeiva, winga mpya wa Simba, Peter Banda amepewa jezi namba 11 ambayo ilikuwa ikitumiwa na nyota huyo kutoka Msumbiji.
.
Kwenye mazoezi yake ya kwanza ambayo Simba imeyafanya huko Morocco leo ambako imeweka kambi ya kujiandaa na msimu, Banda ameonekana akiwa amevaa jezi namba 11 ambayo hutumiwa na Miquissone.
Screenshot_20210812-175810_GBInsta.jpg
 
Mbappe: Karibu Paris Messi
.
Staa wa PSG, Kylian Mbappe amemkaribisha Lionel Messi kwenye klabu hiyo kwa kupost kwenye ukurasa wake wa Instagram akiandika: "Karibu Paris Leo"
.
Mbappe ni mmoja wa watu wanaomkubali Cristiano Ronaldo lakini sasa atakuwa akicheza timu moja na Messi.
Screenshot_20210812-180030_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom