Makapuku Forum

Makapuku Forum

Joseph Mbilinyi maarufu ‘Sugu’ Mbunge wa Mbeya mjini aliyepita ni miongoni mwa Watanzania wa mwanzomwanzo kupata chanjo ya corona Nchini Tanzania.

Sugu ambae alipata chanjo hiyo pamoja na Mke wake ameandika yafuatayo baada ya kuweka picha hii “I feel relieved at last, nilikua niko tayari kuifuata hii chanjo kokote duniani, leo Mimi na Wife wangu tumechoma hapahapa nyumbani
Screenshot_20210731-045550_GBInsta.jpg
 
Gari la Abiria kampuni ya Salvation linalofanya safari zake kati ya Karagwe, Bukoba mpaka Mwanza limeteketea kwa moto baada ya kufika eneo la Ilemela kata ya Gwanseli iliyopo Wilaya ya Muleba Mkoa wa Kagera wakati likielekea Mwanza.

Gari hilo limeteketea mapema leo na taarifa zinadai abiria wote wamenusurika japo wengine wamejeruhiwa na kukimbizwa Hospitali.
Screenshot_20210731-050150_GBInsta.jpg
Screenshot_20210731-050211_GBInsta.jpg
 
“Idadi ya Watu wanaosafiri na Ndege za ATCL baada ya kufufuliwa imeongezeka kutoka abiria 4000 hadi Elfu 60 kwa Mwezi , hivi karibuni anga likifunguliwa vizuri, safari za Kimataifa zitaongezeka” ———Rais Samia

“Shirika limeanza kufanya huduma za viwanjani na kutayarisha vyakula kwa ajili ya ndege zake, Shirika linaweza pia kufanya matengenezo madogo na makubwa ya Ndege hongereni sana”——-Rais Samia

“Nimefurahi kuona miongoni mwa Marubani, wanne ni Wanawake na nashuhudia hili kwasabau wananirusha hata kwa Safari za Kimataifa na naambiwa wengine watatu wataongezeka”———Rais Samia

“Miaka mitano ijayo Serikali tumejipanga kuliimarisha Shirika la Ndege, lakini pia Sekta nyingine za usafirishaji Baharini, Barabara na Reli ili kuimarisha Sekta ya Usafirishaji, Watanzania tujipange vema ili kunufaika na fursa za usafirishaji ” ——-Rais Samia

“Nimepokea mpango kazi wa Shirika, changamoto zote za Shirika tumezipokea tutazifanyia kazi, niliombe Shirika tuzitunze Ndege hizi, tumepanga pia kununua Ndege ya mizigo “———Rais Samia kwenye mapokezi ya Ndege mpya aina ya Bombardier 8-Q400 leo Julai 30, 2021 Uwanja wa Julius Nyerere, Dar es Salaam
Screenshot_20210731-050430_GBInsta.jpg
Screenshot_20210731-050447_GBInsta.jpg
 
Staa wa Simba SC Bernard Morrison amefungiwa mechi tatu na faini ya Tsh milioni 3 kwa kosa la kimaadili, nidhamu na udhalilishaji

(Morrison alivua nguo) baada ya mchezo wa fainali ya ASFC kati ya Yanga na Simba SC uliyochezwa Kigoma na kumalizika kwa Simba SC kuwa Bingwa kwa ushindi wa 1-0
Screenshot_20210731-050746_GBInsta.jpg
 
Baadhi ya abiria waliokuwa wakisafiri katika Mabasi mawili tofauti kutoka Mbeya kwenda Tunduma wamejeruhiwa katika ajali ya Barabarani eneo la mlima Iwambi Barabara Kuu ya TANZAM majira ya saa mbili usiku.

Baadhi ya mashuhuda wamedai chanzo cha ajali ni mwendokasi na uzembe wa moja ya Mabasi hayo kujaribu kulipita basi jingine ndipo lilipopoteza mwelekeo kisha kuligonga basi jingine na yote yaliingia korongoni.

Taarifa za awali kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ulrich Matei eneo la ajali hakuna kifo chochote kilichotokea na idadi ya majeruhi bado haijafamika na ameelekea hospitali teule ya Ifisi ili kujua madhira ya abiria.

Ulinzi umeimarishwa eneo la ajali chini ya Mkuu wa Wilaya ya Kipolisi Mbalizi Debora Lukololo, updates zaidi kukujia.
Screenshot_20210731-051816_GBInsta.jpg
Screenshot_20210731-051831_GBInsta.jpg
Screenshot_20210731-051850_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom