Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mfahamu Janet Kainembabazi Kataaha Museveni, mwanamke anayeaminiwa kuwa na ushawishi mkubwa Uganda.

Bi Janet Kainembabazi Kataaha Museveni ni mmoja wa wake wa marais waliohudumu kwa muda mrefu katika wadhifa huo nchini Uganda, kutokana na mume wake Yoweri Kaguta Museveni kuwa mamlakani kwa muhula wa sita sasa.

Sawa na wake wa marais wa Rwanda na Burundi Janet Museveni alionja maisha ya kuwa mkimbizi kabla ya kuwa mke wa rais.

Alikimbia ghasia kufuatia mapiganao ya mwaka 1971, wakati Idi Amin alipoupindua utawala wa Milton Obote na wakati alipokuwa ukimbizini alikutana na Bw Yoweri Museveni na wakaoana.

Mnamo mwaka 1979, alirejea nyumbani nchini Uganda kutoka Tanzania ambako alikuwa akiishi kama mkimbizi na mume wake.
Screenshot_20210727-200317_GBInsta.jpg
 
Mfahamu Floyd Mayweather Jr Bondia anayeamini mwanaume anapaswa kuwa na wanawake wengi.

Floyd Joy Mayweather Jr. amestaafu kutoka masumbwi na sasa anamiliki kampuni yake ya kusimamia mchezo huo wa masumbwi ama ndondi inayoitwa Mayweather Promotions.

Ni baba wa watoto watano, mkubwa ni Koraun, ana miaka 21, anayefuata ni binti yake Iyanna mwenye miaka 20, Zion kijana wa miaka 19 na binti yake wa mwisho ana miaka 16 anaitwa Jirah.

Devion Cromwell, mtoto wa mpenzi wake wa zamani Melissa Brim, anamtaja kama mtoto wake aliyemuasili, licha ya taratibu zingine ambazo hazikuwa zimekamilika.

Koraun, Zion na Jirah amezaa na Josie Harris wakati Iyanna amezaa na muigizaji, mfanyabiashara na mtangazaji wa TV, Melissa Brim.

Floyd Joy Mayweather Jr. alizaliwa Februari 24, 1977 huko Michigan Marekani katika familia ya wanamasumbwi.

Baba yake, Mayweather Sr. alishawahi hata kupambana na bondia mkali, Sugar Ray Leonard.

Baba zake wadogo Jeff na Roger Mayweather, walikuwa mabondia pia wakulipwa.
Screenshot_20210727-201303_GBInsta.jpg
Screenshot_20210727-201321_GBInsta.jpg
 
Winga wa Uingereza Jadon Sancho anasema kujiunga na Manchester United ni "ndoto inayotimia" baada ya kumaliza uhamisho wake wa pauni milioni 73 kutoka Borussia Dortmund.

Sancho ndiye mchezaji wa pili mwenye gharama ya juu zaidi wa England wakati wakati wote nyuma ya mwenzake mpya wa United Harry Maguire.

Anajiunga na United kwa mkataba wa miaka mitano.

"Nitashukuru Dortmund kila mara kwa kunipa nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza, ingawa siku zote nilijua kwamba nitarudi England," Sancho, 21, alisema
Screenshot_20210727-201842_GBInsta.jpg
 
Bodi ya Wakurugenzi ya club ya Simba leo imemtangaza mwanahabari mkongwe Ezekiel Kimwaga kuwa kaimu mkuu wa idara ya habari ya Simba SC kwa kipindi cha miezi miwili ili kusaidia kujenga mfumo wa idara hiyo.

Kamwaga atakaimu nafasi hiyo ambayo awali alikuwa akiitumikia Haji Manara, hivyo baada ya wiki kadhaa Simba itatangaza nafasi za ajira katika idara yao ya habari
Screenshot_20210728-150710_GBInsta.jpg
Screenshot_20210728-150739_GBInsta.jpg
 
Club ya Simba imemteua Ezekiel Kamwaga kuwa Kaimu Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Klabu hiyo kwa kipindi cha miezi miwili baada ya Hajis Manara kuondoka Simba na kuachia nafasi hiyo.

Katika kipindi hicho cha miezi miwili Kamwaga atashiriki katika maboresho ya muundo wa utendaji wa Idara hiyo akiwa ni Mwandishi wa Habari mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 15 kwenye tasnia ya habari akifanya kazi katika Vyombo vya Habari vya ndani na Kimataifa.

Taarifa ya Simba SC imesema Kamwaga anaijua vizuri Club ya Simba na historia yake kwani amewahi kuitumikia katika nafasi za Msemaji wa Klabu na Kaimu Katibu Mkuu wa Simba.
Screenshot_20210728-151005_GBInsta.jpg
 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa niaba ya Menejimenti ya Wizara ya Afya na Wataalamu wote wa Sayansi ya Afya amempongeza na kumshukuru Rais kwa kitendo cha kuongoza uzinduzi wa mpango wa kuchanja ambacho kinaashiria uongozi wa ushujaa na uzalendo kwa Tanzania.

“Kwa awamu ya kwanza Serikali imepokea dozi 1,058,400 hivyo, wataanza kuchanja makundi ya kipaumbele kwenye kila mkoa wakiwemo Watoa huduma za afya walio mstari wa mbele, wenye magonjwa sugu na wenye umri wa miaka 50 na zaidi” ——— asema Dr. Gwajima.

“Kufikia tarehe 22 Julai, 2021 jumla watu 4,127,963 walishapoteza maisha duniani huku 191,773,590 wakiwa wamethibitika kuwa na maambukizi ya covid-19, upande wa Afrika kwa tarehe hiyo hesabu ya walioambukizwa lishafikia 4,583,414 na vifo 108,056"
Screenshot_20210728-151130_GBInsta.jpg
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa jana, July 27, 2021 amepokea taarifa ya Kamati ya Uchunguzi wa tukio la moto uliyotokea katika Soko la Kimataifa la Kariakoo July 10, 2021 jijini Dar es salaam.

Majaliwa amepokea taarifa hiyo kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo, CP Liberati Sabas na kuahihidi kuwa Serikali itayafanyia kazi mapendekezo yote yaliyotolewa na Kamati hiyo.

Akizungumza baada ya kuipokea taarifa hiyo kwenye Makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es salaam, Majaliwa amewashukuru na amewapongeza Wajumbe wa Tume hiyo kwa kazi nzuri iliyofanyika kwa weledi mkubwa.

Majaliwa amesema ataifikisha taarifa hiyo kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwani tukio hilo limewagusa watu ndani na nje ya Nchi———“Naahidi mbele yako Mwenyekiti kuwa Serikali nimeridhishwa na taarifa mliyo nikabidhi leo na mapendekezo yote mliyoyatoa yatazingatiwa”
Screenshot_20210728-151231_GBInsta.jpg
 
Serikali ya China imetoa msaada wa Chanjo 100,000 za COVID-19 kwa Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto ya Zanzibar.

Msaada huo umepokelewa leo jijini Beijing na Balozi Mbelwa Kairuki na kusafirishwa kwenda Zanzibar July 30 , 2021.
Screenshot_20210728-151423_GBInsta.jpg
Screenshot_20210728-151439_GBInsta.jpg
Screenshot_20210728-151457_GBInsta.jpg
 
“Leo tunazindua uchanjaji Tanzania tukijua chanjo ni ndogo ukilinganisha na idadi ya Watu, kama alivyosema Waziri wapo wanaozikataa lakini wanaozitaka ni wengi sana, nina meseji nyingi Watu wakiuliza Mama chanjo lini chanjo lini?” ——— asema Rais Samia Ikulu DSM leo akizindua uchanjaji chanjo ya corona Tanzania.

“Niwahakikishie Watanzania wale wote ambao kwa hiari yao wapo tayari kuchanjwa tutahakikisha chanjo zinapatikana, chanjo ni hiari ya Mtu lakini pia chanjo ni imani, mwilini mwangu hii chanjo ya leo ni ya sita, tulichanjwa tangu nikiwa Shule ya Msingi na zimenipa uzima wa kutosha mpaka leo nipo hapa”

“Wakati ule tukiwa tunachanja wapo Wazee walikataza lakini Shuleni tulilazimishwa tukachanja, yapo madhara kuna waliovimba mikono mpaka leo wana makovu lakini tulichomwa” ——— Rais Samia.
Screenshot_20210728-151609_GBInsta.jpg
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema yupo tayari kuchanjwa leo ili kumuunga mkono Rais Samia na kuwaonesha Watanzania kuwa chanjo za Covid 19 zinazotolewa ni salama.

Tayari Rais Samia amechanjwa huku TV mbalimbali ikiwemo Ayo TV zikionesha live zoezi hilo kutokea Ikulu Dar es salaam.
Screenshot_20210728-151743_GBInsta.jpg
 
“Nakemea upotoshaji unaofanywa, pia nakupongeza Mhe. Rais Samia kwa kusimama bila kutetereka wala kukatishwa tamaa katika kuitekeleza kazi ya kupambana na UVIKO-19 “

“Tukio hili la Rais Samia kuliongoza Taifa katika kuchanja chanjo ya UVIKO-19 linathibitisha kuwa wewe ni kiongozi wa mfano, jasiri, mwenye uthubutu na mwenye maamuzi ya kizalendo”

“Chanjo hizi ni bora, salama na zimehakikiwa na wataalamu wetu kama tunavyohakiki dawa zingine ambazo zinatoka nje ya nchi kwa Wafadhili wetu”

“Chanjo za UVIKO-19 zimeonesha faida nyingi zikiwemo za kupunguza maambukizi, kupunguza makali ya ugonjwa hasa wanaopumulia mashine pia kupunguza vifo”——— asema Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Dorothy Gwajima mbele ya Rais Samia Ikulu DSM leo.
Screenshot_20210728-152003_GBInsta.jpg
 
Hizi ni picha za Wakuu wa Wilaya za Temeke Jokate Mwegelo, Kinondoni Godwin Gondwe na Kigamboni Fatma Nyangasa wakichomwa chanjo ya corona IKULU Dar es salaam leo baada ya Rais Samia na Waziri Mkuu kuchanjwa.
Screenshot_20210728-172955_GBInsta.jpg
Screenshot_20210728-173018_GBInsta.jpg
Screenshot_20210728-173033_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom