Makapuku Forum

Makapuku Forum

Waziri wa Afya wa Zanzibar Nassor Mazrui amethibitisha kuchanjwa na chanjo aina ya SINOVAC ambayo ni msaada kutokea China na kusema watakaopewa kipaumbele kwenye kupewa chanjo hiyo ni pamoja Wahudumu wa Afya walio mstari wa mbele, Wafanyakazi wa Airport na wanaojishughulisha na Sekta ya Utalii.

"Nimekuja hapa kuchanja na tumepata msaada kutokea Serikali ya China, tumepata Dozi Elfu kumi kwa ajili ya kuchanja Watu Elfu 5 na tunatarajia tena kupokea chanjo Dozi Laki moja hivi karibuni, tutahakikisha Wazanzibar wote watachanjwa kwa anaetaka “———Mazrui
Screenshot_20210722-193444_GBInsta.jpg
 
Jeshi la Polisi Mwanza limethibitisha kuwashikilia Watu 15 Viongozi na Wafuasi wa CHADEMA akiwemo Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe kwa mahojiano.

“Freeman Mbowe alikamatwa na Polisi Mwanza kwa kupanga maandamano na wakati tunaendelea kumuhoji ile alfajiri wenzetu wa Dar es salaam walikuwa wanamuhitaji kwa makosa mengine ya jinai na tukamsafirisha kwenda Dar es salaam kisha tutamrudisha hapa Mwanza kuungana na wenzake” amesema RPC Mwanza Ramadhani Ng’anzi.
Screenshot_20210722-193813_GBInsta.jpg
 
Jeshi la Polisi limesema Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe anashikiliwa kwa tuhuma za kula njama ya kufanya vitendo vya kigaidi ikiwepo kuua Viongozi wa Serikali ambapo wenzake 6 walishafikishwa Mahakamani

“Freeman Mbowe alikuwa anafahamu fika kuwa ana tuhuma zinazomkabili zinachunguzwa na kwamba wakati wowote angehitajika Polisi kwa hatua nyingine za kisheria mara tu uchunguzi utakapokamilika hatua ambayo imefikiwa kwa sasa”

“Kama ilivyo kwa baadhi ya Watu kucheza na nyakati na matukio akaona ni vyema akimbilie Mwanza kwa kigezo cha kongamano la Katiba Mpya ili akikamatwa Umma uamini amekamatwa kwasababu hiyo”

“Hata hivyo uchunguzi unaendelea kule Mwanza kutokana na vitendo vya uvunjifu wa amani, ukibaini kuna sheria aliyovunja hatutasita pia kumfikisha Mahakamani pamoja na Viongozi wenzake wanaoshikiliwa kule”———-David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi
Screenshot_20210722-211152_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom