Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20210724-055015_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20210724-055236_Opera%20Mini.jpg
 
Kama na wewe ulitamani kuiona hiyo Night Club iliyotengenezwa ndani ya Treni iliyobeba Mashabiki wa Simba na Yanga kwenda 89.3 Kigoma leo ikitokea 88.5 DSM, picha ndio hizi hapa.

Kwenye picha ya mwisho kabisa wanaonekana Wana wakicheza Playstation 5 ndani ya treni…. Kigoma na Dar ni KM 1444 za barabara kwa mujibu wa google lakini kwa hili bata ndani ya Treni, hakuna ataeboreka.

Mashabiki hawa watarudi Dar na Treni hii siku ya Jumapili, huu ni mchongo ulioandaliwa na CLOUDS MEDIA GROUP kwa kushirikiana na Shirika la Reli Tanzania na hii sio mara ya kwanza kwa CLOUDS kufanikisha bata la kwenye Treni.

Nimejikuta natamani eti
Screenshot_20210724-060241_GBInsta.jpg
Screenshot_20210724-062305_GBInsta.jpg
Screenshot_20210724-062324_GBInsta.jpg
Screenshot_20210724-062339_GBInsta.jpg
 
Kama na wewe ulitamani kuiona hiyo Night Club iliyotengenezwa ndani ya Treni iliyobeba Mashabiki wa Simba na Yanga kwenda 89.3 Kigoma leo ikitokea 88.5 DSM, picha ndio hizi hapa.

Kwenye picha ya mwisho kabisa wanaonekana Wana wakicheza Playstation 5 ndani ya treni…. Kigoma na Dar ni KM 1444 za barabara kwa mujibu wa google lakini kwa hili bata ndani ya Treni, hakuna ataeboreka.

Mashabiki hawa watarudi Dar na Treni hii siku ya Jumapili, huu ni mchongo ulioandaliwa na CLOUDS MEDIA GROUP kwa kushirikiana na Shirika la Reli Tanzania na hii sio mara ya kwanza kwa CLOUDS kufanikisha bata la kwenye Treni.

Nimejikuta natamanieti

Safi sana hii nakumbuka ile ya kipindi kile clouds walifanya Dar - kisaki Moro
 
Mashabiki wa Simba na Yanga wameondoka leo asubuhi Dar es salaam kuelekea Kigoma kushuhudia mechi ya timu hizo ambayo itachezwa Jumapili ya weekend hii.

Safari hii ambayo imefanikishwa kwa ushirikiano wa CLOUDS MEDIA na Shirika la Reli (TRC) itakua ya kipekee kwa abiria wote kutokana na mazingira ya kuenjoy kuboreshwa zaidi.

Kuna behewa ambalo halina viti ambalo humo ndani ni kama night club Watu wata-enjoy ngoma kali kutoka kwa DJ, kula na kunywa huku safari ikiendelea, behewa jingine litakua na games kama Playstation, bao na michezo mingine ya kutengeneza kumbukumbu bora.

Hii sio mara ya kwanza kwa CLOUDS MEDIA kuratibu bata za kwenye Treni na zikafanikiwa na kubakiza kumbukumbu bora za wakati wote, burudani ni jadi ya Clouds na jadi ni kuendeleza burudani.
Screenshot_20210724-062852_GBInsta.jpg
Screenshot_20210724-062913_GBInsta.jpg
Screenshot_20210724-062938_GBInsta.jpg
 
Vyama vya NCCR- Mageuzi na ACT- Wazalendo kwa pamoja vimeeleza kusikitishwa kukamatwa na kuendelea kushikiliwa kwa siku mbili kwa Viongozi wa CHADEMA wakiongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe.

Vyama hivyo vimetoa wito kwa Polisi kuwaachia Viongozi na Wanachama hao bila masharti na kisha Viongozi wa Serikali na Viongozi wa Vyama vya siasa wakae mezani.

“Tunatoa wito kwa Viongozi wa Serikali na Viongozi wa Vyama vya siasa nchini tukae chini tuzungumze namna njema ya kufanya siasa bila uhasama, ni wakati sasa wa Viongozi kuzungumza (political dialogue)” imesema taarifa ya pamoja iliyotolewa na vyama hivyo na kusainiwa na Viongozi wake James Mbatia na Zitto Kabwe.
Screenshot_20210724-063116_GBInsta.jpg
 
Mbunge wa Ukonga amesema imefikia hatua Wabunge waanze kulipa kodi kupitia mishahara yao ili wapate uwezo wa kuwaambia Wananchi na wao walipe kodi.

Silaa ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliowashirikisha wananchi wa Mzinga Ukonga jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Maendeleo jimboni kwake.

"Mie nimeanza Ubunge juzi mwaka jana mwezi wa 11, kwahiyo nimekuta hayo yanayosemwa mengine yameshapitishwa tayari Bungeni na katika hili niungane na Mbunge wa Kinondoni, Abbas Tarimba kwamba vikiliwa vya Mwali na vya Kungwi viliwe”

“Ni wakati muafaka sisi Waheshimiwa Wabunge ili tupate uwezo wa kuwaambia Watu waanze kulipa kodi na sisi tuanze kulipa kodi katika mishahara yetu, hakuna sababu ya kuwa wengine wanalipa wengine hawalipi ukishakuwa haulipi unakosa ile nguvu ya kumwambia mwenzako alipe”

“Kwahiyo niseme tu kwamba kazi kubwa inayotakiwa tuifanye sisi kama viongozi ni kutowadanganya Watanzania kwamba tunaweza kuiendesha nchi bila Kodi, haitowezekana” ———Jerry Silaa
Screenshot_20210724-063316_GBInsta.jpg
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla ameeleza kukasirishwa kwake na utaratibu usiofaa wa ukamataji wa magari kwenye maegesho yasiyo rasmi ‘wrong parking’, sasa ameelekeza kuitishwa kikao cha pamoja baina yake, Wakurugenzi wa Halmashauri na TARURA ili kupatia ufumbuzi.

RC Makalla amefikia hatua hiyo baada ya kupokea malalamiko mengi ya Wananchi juu ya utaratibu mbovu unaotumika na kusema Kama kiongozi hawezi kuruhusu jambo hilo liendelee.

RC Makalla amesema amebaini pia baadhi ya Vijana wanaofanya kazi hiyo wamekosa weledi na busara na wengi wao wamekuwa wakivizia Mtu afanye kosa ili wamuadhibu badala ya kutoa elimu ili makosa yasifanyike.

Makalla amesema hayo wakati wa uwekaji wa Jiwe la Msingi kwenye Jengo la utawala la Manispaa ya Ubungo na kuipongezea Manispaa hiyo kwa usimamizi mzuri wa fedha za Serikali na kuwataka Watumishi kutoa huduma bora kwa Wananchi.

RC Makalla ameipongeza Manispaa hiyo kwa ukusanyaji Mapato jambo linalopelekea waanze kutekeleza miradi kwa fedha za ndani na pia kutumia Force Account kukamilisha miradi iliyokuwa ikisuasua ikiwemo Jengo hilo la utawala.
Screenshot_20210724-063633_GBInsta.jpg
Screenshot_20210724-063707_GBInsta.jpg
Screenshot_20210724-063725_GBInsta.jpg
 
“Tatizo la Corona lipo na linagharimu Watu uchumi na uhai, jana nilitangaza kuwa July 21,2021 tulikuwa na wagonjwa waliolazwa 682 Nchi nzima (ambao ndiyo tuliweza kuzifikia takwimu zao) kwa jana peke yake wagonjwa wapya waliolazwa kwa takwimu zilizotufikia walikuwa 176, ikumbukwe hawa ndio walioripoti vituo vya huduma za afya na huenda wengine wako majumbani”

“Vilevile, ikumbukwe kwamba sio kwamba Watu hawafariki la hasha wanafariki na kwa takwimu za July 21, 2021 waliofariki ni 29 kwa takwimu zilizotufikia, itoshe kusema tatizo lipo, lazima tusimame tupambane bila kuathiri shughuli zetu za uchumi na kutiana hofu tukajikuta tumeongezea tatizo lingine”———Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dr. Dorothy Gwajima akiwa Dar es salaam
Screenshot_20210724-064016_GBInsta.jpg
 
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi leo Dar es salaam ameiagiza COSOTA kufuatilia na kuhakikisha Msanii anapata haki zake kutoka kwenye kampuni ambazo zimetumia muziki wake bila yeye kupata chochote.

Ametoa maagizo hayo Dar es Salaam alipomwita Msanii huyo aliyekuwa amelalamika kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kudhulumiwa.

“Hili limeisha COSOTA simamieni Msanii huyu apate haki zake kutoka kampuni hizo anazozilalamikia, muwasiliane mara moja na wenzetu wa Kenya kuhakikisha kazi za Mb Dogg zinapata stahiki yake”———Dr. Abbas

Msanii Mb Dogg alitumia ukurasa wake kulalamikia kile alichodai baadhi ya Kampuni kutumia Muziki wake kujinufaisha bila ya yeye kupata haki yake na hata alipojaribu kuwasiliana nao hawakumpa ushirikiano.
Screenshot_20210724-064135_GBInsta.jpg
Screenshot_20210724-064200_GBInsta.jpg
 
Mwanamuziki Na Mwanzilishi mwenza wa Kilimanjaro Band ‘Njenje’ Mzee Keppy Kiombile amethibitisha kufariki kwa msanii Mkongwe wa Band hiyo Waziri Ally.

“Alianza kujisikia vibaya Jumatano akiwa Tanga ambako Jumamosi alitumbuiza na alisafiri mpaka Tanga akiendesha gari mwenyewe, jumatano alisema hajisikii vizuri na atakapo rudi Dar es salaam itabidi akachek sasa Jana akarudi na kaka yetu mwingine ndiyo alimuendesha alipofika mchana akaenda Dispensary Mwenge, akahudumiwa Na akawekewa drip mbili na alipotoka pale alikuwa fresh”

“Ilipofika jioni jana akawa anasema hajisikii vizuri akaingia ndani kulala, baadae akawa haongei na hali yake ikabadilika na kuwa mbaya zaidi wakati tunampeleka Hospitali, tulipofika Hospitali Mwananyamala nafikiri alikuwa ameshakata roho njiani”

“Alikua na presha kwa muda mrefu na hata hivyo anashida ya moyo na alishawahi kwenda India kufanya matibabu mwaka jana na alikuwa akitibiwa na dawa za India pia, kuhusu msiba ulipo tumekuja kwa Baba yake Mwembe Chai hivyo tunajaribu kujadili kuona Baba yake atasemaje” ——— Keppy Kiombile.
Screenshot_20210724-081608_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom