Makapuku Forum

Makapuku Forum

Makampuni mengine sita ya Tanzania yamepata idhini ya kuuza Maharage ya Soya nchini China na hivyo kuifanya idadi ya Makampuni ya Tanzania yanayoruhusiwa kuuza maharage ya soya katika soko la China kufikia 72.

Itakumbukwa Mwezi June mwaka huu Ubalozi wa Tanzania nchini China ulitangaza Makampuni 16 ya Tanzania ambayo yalipewa kibali cha Serikali ya China kuuza maharage ya soya katika Soko la China na ikafanya idadi ya Makampuni ya Tanzania yenye idhini ya kuuza maharage ya soya China kufikia 65. View attachment 1862424
 
Polisi Mwanza wamefunga barabara ilipo Hoteli ambayo ukumbi wake ulipangwa kutumika leo kwa kongamano la Katiba Mpya lililoandaliwa na CHADEMA na kuizingira hoteli hiyo.

Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu amesema Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe na wengine 11 wamekamatwa na Polisi.
Screenshot_20210721-180650_GBInsta.jpg
 
Mwili wa Kijana Alex Korosso maarufu Simba umeagwa Katika Kanisa Katoliki Parokia ya Muhimbili Dar es salaam ambapo miongoni mwa walioshiriki kuuaga ni Wasanii mbalimbali wa Bongo Movie ambao Marehemu Alex alifanya nao kazi akiwa Mwanachama na Mweka Hazina wa Chama cha Waigizaji Tanzania.

Mwili wa Alex ambaye alijiua mwenyewe kwa risasi baada ya kumpiga risasi Kijana mwenzake Gift Mushi wakiwa Bar Sinza Dar es salaam weekend iliyopita, unasafirishwa kwenda kuzikwa nyumbani kwao Moshi mkoani Kilimanjaro.
Screenshot_20210721-181054_GBInsta.jpg
Screenshot_20210721-181631_GBInsta.jpg
Screenshot_20210721-181651_GBInsta.jpg
Screenshot_20210721-181714_GBInsta.jpg
 
Kijana Gift Mushi ambaye aliuwawa kwa kupigwa risasi akiwa Bar Sinza kwa Remy Dar es salaam weekend iliyopita, amezikwa leo kwenye makaburi ya Vikunai Mtoni Kijichi Dar es salaam.

Meneja wa Bar hiyo alisema Gift alipigwa risasi na Kijana mwenzake Alex Korosso baada ya kuinuka kutoka kwenye meza yake kwenda kumuomba Alex aache kutisha Watu kwa bastola aliyokua nayo ndipo Alex alipompiga risasi kwa hasira.

Kamanda wa Polisi Kinondoni Ramadhani Kingai amesema bastola aliyokua nayo Alex alikua akiimiliki kihalali lakini akawataka Watu kutokwenda na silaha Bar kunywa pombe hata kama wanazimiliki kihalali kwani wakilewa zinaweza kusababisha madhara kwao au kwa wengine.
Screenshot_20210721-182232_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom