Twenzetu Kigoma ndio maneno mawili ya mwanzo yanayotumika sana kwa sasa kuelekea mechi ya Simba vs Yanga itakayochezwa July 25 2021 Lake Tanganyika Stadium Kigoma, wanasema raha ya kwenda 89.3 Kigoma sio ndege wala basi, raha uende na Treni.... ujionee uzuri wa Tanzania na ushibe experience ya kusafiri umbali mrefu kwa treni ndani ya ardhi ya Tanzania.
Hata wenye magari yao binafsi hawatoyatumia kusafiri kwenda Kigoma, Shirika la Reli Tanzania limesema tickets zinanunulika kwa wingi "imagine uko treni moja, behewa moja na Watu wako mkila na kunywa, ndani ya Treni kuna Bar, usalama wa kutosha, clubs, perfomances kutoka kwa DJ's, Chege, Juma Nature, G Nako, Profesa J, Sholo Mwamba, Madee, Linah, Luludiva, Aslay na wengine"
TRC ambayo imeshirikiana CLOUDS MEDIA GROUP kwenye safari hii, imesema tickets bado zinaendelea kuuzwa kwa 100000 kwa daraja la tatu, laki na elfu ishirini kwa daraja la pili kukaa na shilingi laki moja na elfu hamsini kwa daraja la pili lenye sehemu ya kulala ambapo unaweza kununua ticket yako kwenye booking.trc.co.tz au fika Stesheni Dar es salaam Kamata, Dodoma, Morogoro na Tabora.
Safari itaanza Ijumaa tarehe 23 July na kufika Kigoma July 24 na itageuza baada ya mechi hiyo July 25.