Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kesi ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake imeahirishwa leo hadi Alhamisi Julai 22, 2021 kutokana na shahidi wa pili Numan Jasin (17) kuhudhuria swala ya Eid leo.
Screenshot_20210720-130402_GBInsta.jpg
 
Mwanamfalme Prince Harry ameishangaza familia ya kifalme nchini Uingereza baada ya kugundulika kuwa ana mpango wa kuandika kitabu ambacho kimezua wasiwasi kwamba anaweza kutoa taarifa zaidi za ndani kuhusu familia hiyo.

Harry na mkewe Meghan wamekuwa kwenye vyombo vya habari tangu alipoamua kuachana na familia ya kifalme na kutaka kuishi maisha ya kawaida.
Screenshot_20210720-130525_GBInsta.jpg
 
Mshambuliaji nyota wa Ureno na Juventus ya Italia Cristiano Ronaldo anaonekana kupendezwa na gari la kifahari aina ya 2021 Rolls Royce Sedan Phantom EWB.

Ronaldo anajivunia mkusanyiko mzuri wa gari unaofikiriwa kuwa na thamani ya pauni milioni 16.

Mchezaji huyo wa miaka 36 ambaye hivi karibuni alishinda tuzo ya mfungaji bora wa Euro 2020 alichapisha picha yake kando ya gari hilo na ujumbe "Siku ya uamuzi,". •

Chapisho limevutia likes Milioni 11.8 kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Gari hilo la 2021 Phantom EWB hugharimu takriban dola milioni moja nukta moja $ 1.1million kwa mujibu wa tovuti ya kuuza magari ya Cars Guide.

Mwezi Februari, Ronaldo aligonga vichwa vya habari duniani baada ya kununua gari la bei kubwa dola $18 million USD Bugatti Centodieci kusherehekea siku yake ya kuzaliwa ya 36
Screenshot_20210720-130846_GBInsta.jpg
 
Polisi nchini Kenya wamemkamata mshukiwa wa utekaji na mauaji ya watoto takriban 10.

Masten Milimu Wanjala aliwaelekeza maafisa wa polisi katika sehemu mbalimbali alikotupa miili ya waathiriwa wake baada ya kuwaua katika tukio ambalo limeibua taharuki jijini Nairobi .

Polisi wanasema mbinu zake za kutekeleza mauaji ni za kuogofya na amekiri kwamba amekuwa akitumia kemikali inayofanana na unga kwa wathiriwa wake kabla ya kuwaua kwa kuwanyonga au kuwafyonza damu kupitia mishipa .

Miili ya waathiriwa wake wawili ilipatikana katika eneo la Kabete,viungani mwa jiji la Nairobi kisha mwili mwingine ulipatikana jana karibu na eneo hilo hilo pembezoni mwa mto.

Polisi wanasema mshukiwa alianza kutekeleza mauaji ya watoto akiwa na umri wa miaka 16.

Screenshot_20210720-131200_GBInsta.jpg
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia kwa dhamana aliyekuwa Mkurugenzi wa Mipango wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Kuruthumu Mansoor (57) aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya Uhujumu Uchumi, dhamana hii ni baada ya kufutiwa mashtaka ya utakatishaji fedha.

Mapema mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) aliwasilisha ombi la kubadilisha hati ya mashtaka baada ya kumfutia Mshtakiwa huyo mashtaka ya utakatishaji fedha na hivyo kupewa dhamana.

Akisomewa masharti ya dhamana Mshitakiwa ametakiwa kuwa na Wadhamini wawili wenye barua na vitambulisho vya Taifa au vitambulisho vinavyotambulika watakaosaini bondi ya shilingi milioni 20.

Mansoor ametimiza masharti hayo na kuachiwa kwa dhamana baada ya kukaa mahabusu kwa zaidi ya miaka miwili.
Screenshot_20210720-142939_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom