Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20210718-073411_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20210718-073425_Opera%20Mini.jpg
 
Hizi ni picha za tukio la moto usiku wa saa nne July 17,2021 ambao umeteketeza nyumba kwenye mtaa wa Airport mkoani Dodoma, ni moto ambao kwa ukubwa wake Jeshi la Zimamoto lilifanikiwa kuuzima baada ya dakika 120.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Ramadhan Kailima amesema “tutatoa tathmini baadae chanzo cha moto ni nini, niwasihi Wananchi wasihifadhi vitu ambavyo ni hatari na ni hatarishi kwao, kuuzima moto huu gari moja lingetosha kama kusingekua na vilipuzi ndani”

Unaweza kumtazama Naibu Katibu Mkuu Kailima akiongea kwa urefu kwenye post iliyopita.
Screenshot_20210718-105100_GBInsta.jpg
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Philip Isdor Mpango ameweka jiwe la Msingi ujenzi wa majengo mapya ya Chuo cha Ualimu Kabanga - Kasulu, Kigoma

“Nimefurahi kuona Chuo kinajengwa na Wakandarasi wa ndani SUMA JKT na kusimamiwa na BICCO (UDSM) Kazi hii ni nzuri sana na inaonekana kwa macho”———-DKt. Philip

“Ujenzi wa majengo mapya ni matokeo ya maamuzi ya kuhamisha Chuo cha Ualimu Kabanga kutoka katika majengo chakavu yanayotumika sasa na umefikia asilimia 80 kukamilika”———-Prof. Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu
Screenshot_20210718-105240_GBInsta.jpg
Screenshot_20210718-105301_GBInsta.jpg
Screenshot_20210718-105326_GBInsta.jpg
 
Miongoni mwa story ambazo zimegusa hisia za Watu wengi Weekend hii ni ya tukio la Mtu kupigwa risasi akiwa Baa Sinza kwa Remi Dar es salaam usiku wa July 17 2021.

Kijana Alex maarufu Simba amemuua kwa kumpiga risasi Kijana anayeitwa Gift na kisha na yeye akajiua kwa kujipiga risasi wakiwa kwenye Baa hiyo.

Sasa imebainika kwamba Alex alisherehekea Birthday yake June 13,2021 na cake moja ambayo ilikatwa kwenye Birthday yake siku hiyo ilikuwa na picha ya Bastola na hii inahisiwa kwamba huenda kwa Alex Bastola kilikuwa ni kitu anachokipenda.
Screenshot_20210718-141543_GBInsta.jpg
Screenshot_20210718-141618_GBInsta.jpg
 
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limefanya ukaguzi wa visima vya maji ya kuzimia moto (Fire Hydrants) katika Jiji la Dodoma.

“Visima vya Maji ya Kuzima Moto "Fire Hydrant" kukosekana katikati ya miji au kutokuwa na msukumo wa maji "pressure"wa kutosha, ni changamoto katika miji mikubwa kwenye zoezi la uzimaji moto” ———Zimamoto
Screenshot_20210718-142245_GBInsta.jpg
Screenshot_20210718-142317_GBInsta.jpg
 
Vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa Watoto vimebainika kukita mizizi katika Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma ambapo ripoti ya Wilaya hiyo inaonesha kuwa Watoto 981 wamepewa ujauzito katika kipindi cha miezi sita iliyopita January mpaka June 2021.

Taarifa hiyo imebainika wakati Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mwanaidi Ali Khamis akiwa Wilayami humo kukagua na kujionea utoaji wa huduma za Ustawi wa Jamii na masuala ya Maendeleo ya Jamii.

Naibu Waziri Mwanaidi amesema taarifa hizo haziwezi kufumbiwa macho na badala yake Watendaji wanaohusika wafanye kila linalowezekana kuhakikisha Watuhumiwa wanapatikana na haki inatendeka katika kipindi kifupi iwezekanavyo.

Naibu Waziri Mwanaidi ameongeza kuwa jamii haiwezi kutegemea miujiza ya mafanikio ya kizazi kijacho endapo itabaki kufumbia macho vitendo vya ukatili wa kijinsia hususani dhidi ya Wanawake na Watoto kwa kuangalia Watoto wao wanapata mimba katika umri mdogo na kukatisha ndoto zao.
Screenshot_20210718-142503_GBInsta.jpg
 
Zaidi ya Watu laki moja wameandamana nchini Ufaransa kupinga hatua za hivi karibuni za Serikali za kuwashinikiza Watu kwenda kuchanjwa chanjo ya Corona, Serikali inalenga kuzuia maambukizi ya virusi vipya aina ya Delta vinavyosambaa haraka.

Huko Paris, maandamano tofauti ya mrengo wa kulia na mrengo wa kushoto yametawala sehemu tofauti za Jiji, kuanzia Strasbourg Masharimi, Lille kaskazini, Montpellier kusini na kwingineko.

Maelfu ya Watu wameitiki wito wa kuandamana kutoka kwa Mwanasiasa wa mrengo wa kulia Florian Philippot, Mpambe wa zamani wa Marine Le Pen ambaye alitangaza mapema mwezi huu kwamba atawania Urais katika uchaguzi wa mwaka 2022.

Waandamanaji wamelaani uamuzi wa Serikali uliotolewa siku ya Jumatatu kufanya chanjo ya lazima kwa Wafanyakazi wote wa huduma za afya, na Mtu kutakiwa awe na cheti cha kuthibitisha hana Corona au umechanjwa kikamilifu ili kuingia migahawa na maeneo mengine ya umma.
Screenshot_20210718-142634_GBInsta.jpg
Screenshot_20210718-142654_GBInsta.jpg
Screenshot_20210718-142717_GBInsta.jpg
 
Alex Korosso kwa jina maarufu la Simba anayedaiwa kuua na kisha kujiua, alikuwa mhasibu wa Chama cha Waigizaji Tanzania (TDFAA),imeelezwa.

Hayo yamesemwa leo Jumapili Julai 18, 2021 na mwenyekiti wa chama hicho,Chiki Mchoma maarufu kwa jina la Chiki katika mahojiano yake na Mwananchi.

Tukio la Korosso kujiua lilitokea jana baa ya Lemax maeneo ya Sinza jijini Dar es Salaam, baada ya kuibuka mabishano kati yake na mtu aliyetambulika kwa jina la Gift ambaye alimpiga risasi na kisha naye kujipiga na kufariki hapohapo.

Akimzungumzia Korosso, Chiki amesema alikuwa ni mhasibu wao wa chama baada ya mkutano mkuu wa waigizaji uliofanyika Mei kumpitisha na kubainisha kuwa katika utendaji wake alikuwa ni mtu mwenye maono katika kukipeleka chama hicho mbele.

"Alex alikuwa mtu mwenye akili nyingi na alikuwa na maono ya kuona chama chetu kikipiga hatua mbele na tayari alishatuandikia madododoso mbalimbali ya kuweza kupata fedha za kukiendesha chama chetu, tumesikitishwa sana na kifo chake," amesema Chiki.

Alipoulizwa kama aliwahi kuwa muigizaji na kaigiza filamu gani, Chiki amesema hakuwa mwigizaji bali alikuwa ni mdau mkubwa wa masuala ya kazi za kuigiza na alikuwa katika mpango wa kuanzisha kampuni yake ya kuandaa kazi za filamu na tayari alishaanza kununua baadhi ya vifaa.
Screenshot_20210718-144326_GBInsta.jpg
 
Zaidi ya Watu laki moja wameandamana nchini Ufaransa kupinga hatua za hivi karibuni za Serikali za kuwashinikiza Watu kwenda kuchanjwa chanjo ya Corona, Serikali inalenga kuzuia maambukizi ya virusi vipya aina ya Delta vinavyosambaa haraka.

Huko Paris, maandamano tofauti ya mrengo wa kulia na mrengo wa kushoto yametawala sehemu tofauti za Jiji, kuanzia Strasbourg Masharimi, Lille kaskazini, Montpellier kusini na kwingineko.

Maelfu ya Watu wameitiki wito wa kuandamana kutoka kwa Mwanasiasa wa mrengo wa kulia Florian Philippot, Mpambe wa zamani wa Marine Le Pen ambaye alitangaza mapema mwezi huu kwamba atawania Urais katika uchaguzi wa mwaka 2022.

Waandamanaji wamelaani uamuzi wa Serikali uliotolewa siku ya Jumatatu kufanya chanjo ya lazima kwa Wafanyakazi wote wa huduma za afya, na Mtu kutakiwa awe na cheti cha kuthibitisha hana Corona au umechanjwa kikamilifu ili kuingia migahawa na maeneo mengine ya umma. View attachment 1858277View attachment 1858278View attachment 1858281
Kabisa aise. Tusilazimishane kuchanjwa
 
“Kutokana na Jeshi la Polisi kuzuia Kongamano la Katiba lililokuwa limeandaliwa na Baraza la Vijana la CHADEMA jana July 17,2021 na kuwakamata Wanaharakati, Viongozi wa Dini, Viongozi wa Chama, Wanachama, Wananchi na Watanzania kwa ujumla ambao wanataka kupatikana kwa Katiba Mpya nchini katika Jiji la Mwanza”———-CHADEMA

“Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amelazimika kukatisha siku za maombolezo ya msiba wa Kaka yake Kijijini kwao Machame Moshi na ataelekea Mwanza kushirikiana na Watanzania wote katika kuhakikisha Haki ya kukusanyika na kujadiliana inapatikana kwa mujibu wa Katiba ya Nchi”———CHADEMA
Screenshot_20210718-225127_GBInsta.jpg
Screenshot_20210718-225144_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom