Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20210716-065057_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20210716-065131_Opera%20Mini.jpg
 
Idadi ya Watu waliofariki nchini Ujerumani kutokana na mafuriko ambayo yamesababishwa na mvua kubwa imepindukia Watu 81.

Saa 24 zilizopita idadi ilikua 30 lakini sasa imeongezeka na kufika 81, mamia ya Watu bado hawajulikani walipo huku nyumba kadhaa zikiwa zimeharibika sana na nyingine hata kubomoka kabisa huko Ujerumani Magharibi.
Screenshot_20210716-133042_GBInsta.jpg
 
Makampuni matatu ya China yameonesha nia ya kununua tani 10,000 za korosho ya Tanzania iliyobanguliwa ya ukubwa wa W180 na Karafuu kutoka Tanzania. Taarifa hiyo imetolewa leo Jijini Zhengzhou katika Jimbo la Henan wakati wa ziara ya Balozi Mbelwa Kairuki katika soko la Jumla la Bairong.

Soko la Jumla la Bairong ni la pili kwa Ukubwa nchini China likiwa na eneo la mita za mraba Milioni 1.6, maduka 10,000 na wafanyakazi 100,000 na Mauzo ya soko hili kwa mwaka yanafikia $ Bilioni 20.
Screenshot_20210716-143632_GBInsta.jpg
Screenshot_20210716-143652_GBInsta.jpg
Screenshot_20210716-143710_GBInsta.jpg
 
Imeelezwa kuwa Hospitali ya Bugando Mwanza ina uwezo wa kuwahudumia Wagonjwa wenye matatizo ya upumuaji na kwamba hakuna mapungufu yeyote kwenye mitungi ya Oxygen kama taarifa zinavyosambazwa.

Uongozi wa Hospitali hiyo umesema wanayo mitambo miwili ya kuzalisha Oxygen na kuhudumia Wagonjwa kwa 80%.

Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando Dkt. Fabian Massaga ameyasema hayo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel alipokwenda kujionea huduma zinazotolewa Hospitalini hapo.

“Tunao Wagonjwa ambao sio wengi sana na tunamudu kuwahudumia, tunayo mitambo miwili ya kuzalisha Oxygen kama taasisi tuna mitungi ya kutosha ya Oxygen na Wagonjwa tulionao wanahudumiwa vizuri hamna changamoto yoyote ya Oxygen” ———Dkt. Massaga
Screenshot_20210716-143905_GBInsta.jpg
Screenshot_20210716-143924_GBInsta.jpg
 
Serikali imesema ranchi ya mifugo ya Mkata iliyopo Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro itakuwa sehemu ya kuzalisha mbuzi kwa wingi kwa ajili ya mkakati wa kopa mbuzi lipa mbuzi, ambao unatarajia kuanza hivi karibuni lengo likiwa ni kuwa na mbuzi wa kutosha kwa ajili ya soko la nje ya nchi.

Akizungumza na uongozi wa ranchi hiyo na wilaya wakati wa ziara ya kikazi ya siku moja katika Ranchi ya Mkata, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdalllah Ulega amesema ni muhimu kuangalia namna bora ya kufanya ufugaji wa kibiashara katika ranchi hiyo.

Amesema Serikali imechagua Ranchi ya Mkata kuwa kituo cha kuzalisha mbuzi kwa wingi ambao watakuwa wanasambaza katika maeneo mbalimbali nchini.
Screenshot_20210716-145258_GBInsta.jpg
 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali, Ummy Mwalimu amesema Serikali imejiwekea mkakati wa kuhakikisha inaweka mazingira wezeshi kwa walimu wanaofanyakazi katika maeneo magumu na mbali kufikika.
Screenshot_20210716-145631_GBInsta.jpg
 
Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dr. Philipo Mpango amewataka Idara ya Uhamiaji Mkoa wa kigoma kuwa makini wanapofuatilia Wahamiaji haramu wanapoingia nchini kinyume na sheria za Nchi bila kuwadhalilisha Wananchi.

Amesema Idara ya Uhamiaji wafanye kazi yao kwa weledi kwa ajili ya usalama wa Wananchi na Nchi ambapo amewaagiza kukaa pamoja na Wabunge ili kujadili namna bora ya kuhakikisha wale ambao sio raia na wanaishi nchini kinyume na taratibu za Nchi wanachukuliwa hatua stahiki na sio kumsumbua kila Mwananchi kwa kigezo cha kuzaliwa Kigoma.

"Wananisema Mimi kwenye mitandao mpaka wamenibatiza jina la Burundi Mimi nawapuuza, Burundi yenyewe nimekanyaga kwa mara ya kwanza nilipotumwa na mheshimiwa Rais kwenye kumbukizi ya aliyekuwa Rais wa Burundi hayati Nkurunzinza lakini nawapuuza tu"———Dr. Mpango Makamu wa Rais wa Tanzania

"Dhambi yangu haiwezi kuwa ni kuzaliwa Kasulu, dhambi yetu haiwezi kua ni kuzaliwa Kigoma naomba Viongozi wa Mkoa walisimamie hili" ———-Dr. Mpango Makamu wa Rais wa Tanzania.
Screenshot_20210716-191304_GBInsta.jpg
Screenshot_20210716-191324_GBInsta.jpg
 
Mkurugenzi wa Mji wa Kasulu Kigoma Fatna Laay amekataa kutumia fedha zote shilingi milioni 210 alizopewa kwa ajili ya kujinunulia gari lake la kazi na badala yake ameigawanya fedha hiyo na kuwanunulia Pikipiki Watendaji wa Kata 12.

Maamuzi ya kupatiwa fedha hizo milioni 210 ilitokana na Mkurugenzi huyo kutumia gari bovu kwa miaka mitatu ambapo baada ya kupewa fedha hizo aliamua kununua gari la milioni 162 huku fedha zilizobaki ambazo ni milioni 47 akinunua Pikipiki 12 kwa Watendaji wa Kata 12 na amezikabidhi leo kwa kushirikiana na Mbunge wa Kasulu Mjini ambaye pia ni Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako.
Screenshot_20210716-191517_GBInsta.jpg
Screenshot_20210716-191539_GBInsta.jpg
Screenshot_20210716-191606_GBInsta.jpg
Screenshot_20210716-191633_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom