Rais Samia Suluhu Hassan, leo July 11, 2021 ametoa pole kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla na Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Kariakoo kufuatia hasara kubwa waliyoipata kutokana na kuungua moto kwa Soko Kuu la Kariakoo lililopo Jijini Dar es Salaam.
Kufuatia hasara kubwa iliyotokana na kuungua kwa Soko hilo usiku wa July 10, 2021, Rais Samia ameviagiza Vyombo vya Ulinzi na Usalama kufanya uchunguzi wa kina kujua chanzo cha moto huo.
Amesema Soko Kuu la Kariakoo ni soko kubwa Jijini Dar es salaam ambalo lina mkusanyiko mkubwa wa wafanyabiashara na kuteketea kwa soko hilo kutakuwa kumesababisha hasara kubwa kwa Wapangaji na Wamiliki wa soko hilo kongwe nchini.
Rais Samia amesema Soko la Kariakoo licha ya kuajiri Wafanyabiashara wengi lakini ni kitovu cha biashara kwa Nchi za Afrika Mashariki hivyo tukio hilo si hasara kwa Wafanyabiashara tu bali hata kwa Serikali.
View attachment 1849510