Makapuku Forum

Makapuku Forum

20210713_060647.jpg
20210713_060710.jpg
 
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Fatmah Nyangasa amewakumbusha Wananchi wa Kigamboni kuzingatia miongozo ya kujikinga na kirusi corona kinachosababisha ugonjwa wa COVID-19 kwa kuvaa barakoa na kunawa mikono kwa kutumia maji tiririka.

DC Nyangasa ametoa hamasa hiyo leo akiwa ameambatana na Katibu Tawala wa Kigamboni, Dalmia Mikaya ambapo amewataka Wananchi wa Kigamboni ikiwemo wanaotumia Kivuko kujilinda dhidi ya kirusi corona.

"Muachiane nafasi, mkumbuke kutumia vitakasa mikono, kuvaa barakoa na kuepuka kusongamana” ——— DC Nyangasa.
20210713_171756.jpg
20210713_171820.jpg
 
Jeshi la Afrika Kusini limeanza kuwaingiza mtaani Wanajeshi ili kuwasaidia Polisi katika majimbo mawili ambayo yametawaliwa na vurugu na uhalifu unaodaiwa kufanywa na Wafuasi wa Rais wa zamani wa Nchi hiyo Jacob Zuma wakishinikiza Rais huyo atolewe gerezani.

Kwa siku ya nne vurugu zimeendelea Nchini South Africa huku Watu 6 wakiripotiwa kufariki kutokana na vurugu hizo ambapo wakati vifo hivyo vikitokea, Mahakama inajitayarisha kusikiliza pingamizi lililowasilishwa na upande wa Jacob Zuma dhidi ya kifungo cha miezi 15 jela alichoanza kukitumikia.

Ukiachia mbali Watu hao 6 waliofariki, kuna wengine 219 wamekamatwa ambapo Polisi wametoa onyo kwamba Mtu yeyote atakaetumia mitandao ya kijamii kuchochea ghasia atakamatwa na kufunguliwa mashitaka.
20210713_172015.jpg
 
Nimesoma na kupokea maoni,ushauri na kila aina ya hisia ambazo naamini ni kwa upendo juu ya Clip yangu kuhusu kambi za Kitaaluma nilipokuwa nikizungumza na wananchi wetu katika tafsiri yoyote ile naomba Radhi kwa wote waliokwazika ,wananchi na Viongozi wenzangu hasa pale matumizi ya neno "Waziri" lilipobeba hisia tofauti nawaheshimu Mawaziri wote na nafanya nao kazi kwa ushirikiano mkubwa natambua pia kazi nzuri inayofanywa na Mawaziri wetu wanaosimamia sekta ya elimu - Wapo wanaodhani maelezo ya hisia zangu ni kuanza kupandisha mabega,na pengine mgema akisifiwa tembo hutia maji-niwaondoe hofu sina sababu ya kupandisha mabega.
20210713_172208.jpg
 
Watumishi tisa wamesimamishwa kazi katika Kitengo cha upimaji wa COVID - 19 kwa Wasafiri katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere (JNIA).

Agizo hilo limetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Prof. Abel Makubi alipofanya ziara uwanjani hapo kukagua utekelezaji wa maelekezo aliyoyatoa juzi alipofika hapo akiwa ameambatana na Katibu mwenzake wa Wizara ya Uchukuzi.

Prof. Makubi amesema hakufurahishwa na kitendo cha utovu wa nidhamu, kilichofanywa na Watumishi cha kutokufika kazini bila kutoa taarifa rasmi kwa uongozi.

"Jana Watumishi wanane hawakufika na leo mmoja bila kutoa sababu ya msingi, jumla wanakuwa tisa, imeonekana hapa hili zoezi la baadhi ya Watumishi kutokuja kazini limekuwepo, sasa hii imenisikitisha sana kwa baadhi ya Viongozi kushindwa kuchukua hatua zinazostahili na kulindana kwa kuficha uozo”———Makubi
20210713_172521.jpg
 
UNAAMBIWA:

Utafiti wa Chuo Kikuu cha Virginia unaeleza kuwa ni rahisi zaidi kwa Mwanamke kuvutiwa na Mwanaume ambaye anaficha hisia za kumpenda kuliko kuvutiwa na Mwanaume ambaye ameshamtamkia kuwa anampenda.

“Mwanamke anaweza kuambiwa anapendwa na Mwanaume na akamzungusha kwelikweli na huenda asimkubalie hasa yule ambaye huwa na haraka ya kumtongoza siku za mwanzo za kujuana kwao lakini Mwanamke huyohuyo anaweza kuvutiwa na Mwanaume ambaye anahisi kabisa amedata kwake ila hajamtamkia chochote”

“Mwanamke hujiuliza maswali mengi kwamba huyu Mwanaume anafikiria nini mbona hasemi lolote kwangu na mwisho hujikuta yeye Mwanamke anazama kwenye mahaba na Mwanaume huyo, Mwanamke hapendi Mwanaume mwenye pupa”
20210713_172707.jpg
 
UNAAMBIWA:

Utafiti wa Chuo Kikuu cha Jagiellonian unaeleza kuwa kwa Mwanaume kuwa na Mtoto wa kike kunamfanya aongeze siku zake za kuishi.

“Kadri Baba anavyoongeza Watoto wa kike ndivyo anavyoongeza siku zake za kuishi, Mtoto mmoja wa kike humuongezea Baba wastani wa Wiki 74 zaidi za kuishi hii ni kwakuwa hupata furaha na huondokana na stress na hii kupelekea kinga mwili zake kuwa imara na kumuepusha na magonjwa, kwa Mama haijaonesha kama kuna uwezekano wa Mtoto kumuongezea siku za kuishi”
20210713_172905.jpg
 
Mke wa rais wa Ghana bi Rebecca Akufo-Addo amerejesha fedha za marupurupu aliyolipwa tangu rais Nana Akufo-Addo aingie madarakani mwaka 2017, baada ya wananchi kulalamikia mshahara wake.

Bi Addo kupitia kwa taarifa yake alisema aliamua kurudisha fedha zote ambazo alipewa kama ruzuku ambazo ni dola 151,618.

Wake wa rais na makamu wake walipangiwa kulipwa kiasi cha dola $3,500 kila mwezi , kiwango sawa na wanacholipwa mawaziri kufuatiwa mapendekezo yaliyotolewa na kamati ya bunge mwaka 2019.

Hata hivyo wananchi walipinga ruzuku hii wakisema ni ubadhirifu wa pesa za umma wakati huu ambapo uchumi umeyumbishwa na ugonjwa wa Corona.
20210713_173156.jpg
20210713_173212.jpg
20210713_173228.jpg
 
''Hali sana.anakula kiasi kidogo cha majani mara mbili kwa siku, Anapenda kuzungukazunguka nje ya zizi na anaonekana ana furaha sana tukimbeba.''

Maelfu ya watu wamekuwa wakifika kwa wingi katika shamba moja la mifugo huko Bangladesh kumuona kiumbe cha kipekee; ng'ombe mbilikimo kwa jina Rani.

Ng'ombe huyo jike mwenye urefu wa sentimita 25 ana kilo 28 pekee na ana umri wa miezi 23.

Pamoja na amri ya kutotoka nje, zaidi ya watu 15,000 wameripotiwa kumtembelea Rani katika makazi yake huko Charigram, karibu na mji wa Dhaka.

Mkuu wa shamba hilo Hasan Howladar ameomba utambuzi wa Rani kwenye rekodi ya Guiness Book, akisema Rani ni ng'ombe mwenye umbo mdogo zaidi duniani.

Rekodi ya ng'ombe mdogo zaidi ilikuwa ikishikiliwa na Manikyam, nchi jirani ya India, mwenye urefu wa sentimita 61.1 kutoka usawa wa kwato mpaka juu.
20210713_173427.jpg
20210713_173451.jpg
 
”Nikiwa nimelala uso ukiwa umeegemea meza maalumu ya kukanda, nilisubiri kwa hofu. Mtaalamu wa kuchua kwa kutumia kisu, Elsa, kwa bashasha alikuwa ameshika visu viwili. Hii ni kwasababu wakati mwendo wa kukata unatarajiwa katika kuukanda mwili, katika hii, visu hufanya mithili ya ukataji.”

Ingawa inaonekana kuwa hatari,"masaji ya kisu" au "tiba ya kisu", inaaminika kuwa na nguvu za uponyaji na ni aina ya dawa ya Wachina ambayo inadhaniwa kuwa na zaidi ya miaka 2,000.

Elsa alianza kwa kutumia mikono yake kuukanda mwili wangu.
Kisha visu baridi, vya chuma vilianza kupita, juu ya mgongo wangu, mikono na kichwa changu. Nisingejua kuwa visu vilikuwa kazini kama haikuwa sauti ya visu vilivyokuwa vinagongana mara kwa mara.

Cha kushangaza, watu wengi husinzia baada ya kukandwa na visu kwa dakika 70.
20210713_173712.jpg
 
"Mitandao ya kijamii imekuwa ikisema kwamba Museveni amekufa…watafutwe haraka wanaoeleza taarifa kama hizo kwasababu mnapoteza muda wa watu," amesema Rais wa Uganda Yoweri Museveni

Museveni amewatoa wito wa kukamatwa kwa watu wanaotuma taarifa za uvumi kwenye mitandao ya habari ya kijamii wakamatwe.

Amesisitiza kuwa mitandao ya kijamii imekuwa tatizo na inahitaji kuangaliwa.

Baadhi ya watu walieneza taarifa uvumi juu ya afya yake na mwanae wa kiume kwenye mitandao ya kijamii.
20210713_173923.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom