Idadi ya vifo kutokana na ajali iliyotokea usiku wa kuamkia leo ikihusisha magari matatu ambayo ni Toyota Coaster, Toyota Cresta na Lori eneo la nanenane mkoani Morogoro imeongezeka na kufikia Watu 9 kutoka Watu watano jana usiku.
Kaimu Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro, Dr. Kesy Ngalawa amesema pia majeruhi watano wa ajali hiyo wapo Chumba maalum cha Uangalizi (ICU).
Mmoja wa majeruhi Frank Ramsoni amesema Toyota Coaster ilikua inatoka Dar kwenda Mbeya na Dereva aliweka mashada kwenye gari hilo kuashiria imebeba maiti ili kupata wepesi wa kufanya safari ambapo baada ya kufika eneo la Kingulwira Morogoro gari lilisimamishwa na Askari.
Dereva wa gari alishuka kisha Msaidizi wake alichukua gari na kuondoka bila ruhusa ya Askari na wakati yuko barabarani gari likiwa kasi Msaidizi alimpigia simu mwenzake aliebaki na Askari na hapo ndipo akashindwa kulimudu gari likapoteza mwelekeo na kugongana uso kwa uso na lori la Kampuni ya Dangote.
R.I.P
View attachment 1826701View attachment 1826702View attachment 1826703