Makapuku Forum

Makapuku Forum

PAPA MSOFE AFUTIWA MASHTAKA
-
DPP asema hana mpango wa kuendelea na kesi dhidi yake na wenzake
-
Walikuwa wakikabiliwa na mashtaka matano likiwemo la kujipatia fedha kiasi cha Sh943 milioni kwa njia ya udanganyifu
-
Mbali na Msofe, washtakiwa wengine walikuwa wakili wa kujitegemea, Mwesigwa Mhingo, Wenceslau Mtui, Josephine Haule na Fadhil Mganga
-
Miongoni mwa mashtaka yaliyokuwa yakiwakabili ni kuratibu genge la uhalifu, utakatishaji fedha na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu
20210618_142420.jpg
 
UNAAMBIWA

Nchini Norway hakuna ambaye anaweza kuficha siri ya kipato chake kwasababu kila Raia kipato na pesa anayoingiza kwa mwaka huwekwa hadharani mtandaoni na kila Mtu anaweza kupita na kuona, Wafanyakazi wanaweza kuona kiwango cha pesa wanachoingiza Wafanyakazi wenzao na hata jirani yako anaweza kutazama akaona unachoingiza kwa mwaka.

Mwezi wa kumi kila mwaka kiwango cha kodi ambacho Mtu hulipa kwa Mamlaka wa Mapato kuwekwa mtandaoni kikionesha na kipato anachoingiza, Unaambiwa kama utakuwa una maswali kwamba jirani yako ana pesa za kutosha kumiliki Gari kali anayotembelea?, haupati shida unaingia tu online na kupitia mkeka wa hesabu zake.

Kwa sasa ukichungulia jirani yako anatumiwa meseji kuwa ulipita kuchungulia hesabu zake, ila Waandishi wa habari wamepewa uhuru wa kuchungulia bila mwenye taarifa za pesa zake kuambiwa.
20210618_220539.jpg
 
UNAAMBIWA

Case William Kelley (42) kutoka Florida alinunua gari la kifahari (Porsche) kwa USD 140,000 (Tsh. Milioni 324.6) kwa kutumia cheki feki ambayo aliiprint kwenye kompyuta nyumbani kwake, baadaye alikamatwa wakati akijaribu kununua saa 3 za Rolex kwa USD 62,000 (Tsh. Mil 143.7) kwa kutumia cheki nyingine feki.
20210618_220747.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom