Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kitendo cha Nahodha wa Ureno Cristiano Ronaldo juzi wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari kuelekea mchezo wao wa Euro 2020 vs Hungary kuondoa chupa mbili za Cocacola kwenye meza ambao ni Wadhamini wa michuano hiyo na kusisitiza Watu kunywa maji zimefanya thamani ya hisa za Cocacola kushuka kwa 1.6%.

Thamani ya hisa ya Cocacola imeshuka sokoni kwa kitendo hicho kutoka USD 56.10 (Tsh 130,087) kwa hisa moja hadi USD 55.22 (Tsh 128,043) sawa na anguko la 1.6% thamani ya Cocacola katika soko ilikuwa USD Bilioni 242 (Tsh Trilioni 561.2) na sasa ni USD Bilioni 238 (Tsh Trilioni 551.8) hivyo Cocacola wamepata hasara ya USD Bilioni 4 (Tsh Trilioni 9.2)
20210616_142138.jpg
20210616_142200.jpg
 
Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP), Sylvester Mwakitalu amemuondolea hati ya kuzuia dhamana aliyekuwa mkurugenzi mtendaji wa kampuni hodhi ya rasilimali za reli Tanzania (Rahco), Benhardard Tito.

Mbali na Tito, hati hiyo pia imeondolewa kwa wenzake wawili ambao ni mwanasheria wa zamani wa kampuni hiyo, Emmanuel Massawe na mwakilishi wa kampuni ya Rothschild (South Africa) Proprietary Limited, Kanji Mwinyijuma.

Watatu hao walikuwa wanakabiliwa na mashtaka nane likiwemo la kuisababishia Serikali hasara ya dola 527, 540 za Marekani sawa na Sh1.2 bilioni.

Dhamana ya washtakiwa hao ilizuiwa na DPP wa zamani, Biswalo Mganga kwa kuwasilisha hati ya kuzuia dhamana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mwaka 2016.
20210616_143415.jpg
 
Mbunge wa zamani na Mkuu wa Mkoa mstaafu, Aggrey Mwanri akifuraia jambo akiwa ndani ya ukumbi wa Bunge wakati wabunge walipokuwa wakiendelea na kikao cha 52 cha mkutano wa Bunge la Bajeti, jijini Dodoma leo. Picha na Edwin Mjwahuzi
20210616_143712.jpg
 
Upande wa mashtaka katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Mtendaji wa PAP, Harbinder Seth, umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa wamepitia barua iliyoandikwa na mshtakiwa huyo na kufikia makubaliano kwa kile alichokiomba.

Seth aliandika barua hiyo Juni 10, kwenda kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), akiomba kukiri mashtaka yake na kupunguziwa adhabu.

Barua hiyo ilijadiliwa kwa siku mbili na upande wa mashtaka na ule wa utetezi na kisha kutolewa mrejesho.

Wakili wa Serikali Mkuu, Marterus Marandu akisaidiana na Ladslaus Komanya jana alitoa maelezo hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.

Wakili Marandu alitoa maelezo hayo wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya upande wa mashtaka kuwasilisha mrejesho wa kile walichozungumza kati yao na Seth kwa ajili ya kuimaliza kesi hiyo.

“Kesi imekuja kwa ajili ya kutoa mrejesho wa barua iliyoandikwa na mshtakiwa huyu (Seth), niseme barua tumeshazipitia kwa pamoja na tumefikia mahali pa kukubaliana kuhusu kile ambacho mshtakiwa alikuwa anakiomba na baada ya hapo, tumekubaliana kuendelea na shauri hili,” alidai wakili Marandu.
20210616_143813.jpg
 
Viongozi wawili kati ya 36 wa Jumuiya za Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI), Sheikh Farid Hadi Ahmed na Mselem Ali Mselem waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya ugaidi wameachiwa huru.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Sylvester Mwakitalu ameieleza Mwananchi Digital leo Jumatano Juni 16, 2021 kuwa amewafutia mashtaka viongozi wote wa jumuiya hiyo na kilichobaki sasa ni taratibu za kutoka gerezani.
Wawili hao ambao walikuwa mahabusu tangu mwaka 2014 pamoja na wenzao kutokana na kukabiliwa na mashtaka hayo ambayo hayana dhamana wameachiwa huru jana Jumanne Juni 15, 2021 baada ya DPP kuwafutia mashtaka yaliyokuwa yakiwakabili.

Taarifa za kuachiwa huru kwa viongozi hao zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuanzia jana jioni zikieleza kuwa viongozi hao wawili ndio wameachiwa huru na mmoja wa mawakili wao, Juma Nassoro amelieleza Mwananchi Digital kuwa wameshapelekwa majumbani mwao.

Katika ufafanuzi wake Mwakitalu amesema, “ni kweli wameachiwa huru. Nimewafutia wote mashtaka yaliyokuwa yanawakabili. Sasa suala la kutoka gerezani kama wameshatoka wote au wangapi hilo ni suala la taratibu za Magereza lakini mimi nimewafutia mashtaka wote.”
20210616_144009.jpg
 
Viongozi wa kimila ambao ni machifu kutoka maeneo mbalimbali nchini wakiwa ndani ya ukumbi wa bunge wakishuhudia wabunge wakiendelea na kikao cha 52 cha mkutano wa Bunge la Bajeti, jijini Dodoma leo. Picha na Edwin Mjwahuzi
20210616_144206.jpg
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemhukumu, mmiliki wa Kampuni ya kufua umeme ya IPTL, Harbinder Seth, kulipa fidia ya Sh 26bilioni baada ya kupatikana na hatia ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Uamuzi huo umetolewa leo, Jumatano Juni 16, 2021 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Huruma Shaidi wakati kesi hiyo ya Uhujumu uchumi namba 27/2017 ilipoitwa mahakamani hapo kwa makubaliano.
20210616_163704.jpg
 
Mmiliki wa Kampuni ya Kufua umeme ya IPTL, Harbinder Seth akitoka katika Mahabusu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akiambatana na Mkewe baada kuhukumiwa kulipa fidia ya Shilingi Bilioni 26.

Seth ameachiwa leo baada ya kulipa milioni 200 ambapo pesa zilizobaki atalipa kwa awamu kulingana na makubaliano baina yake na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) ambapo atatakiwa kulipa kwa kipindi cha miezi 12 (mwaka mmoja).

Mahakama ya Kisutu leo imemuhukumu Mmiliki huyu wa IPTL, Harbinder Seth kulipa fidia ya BILIONI 26 kwa kupatikana na hatia ya kujipatia fedha kwa udanganyifu ambapo amekaa Mahabusu takribani miaka 4.
20210616_164404.jpg
View attachment 1820646
20210616_164440.jpg
 
Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la soka Tanzania (TFF) kupitia Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Benjamin Kalume imetangaza kuwa Hawa Mniga, Evans Mgeusa na Rais anayetetea kiti chake Wallace Karia ndio wagombea waliokidhi vigezo vya kugombea nafasi ya Urais wa TFF August 7 2021 Tanga, wengine wameshindwa kukidhi vigezo kadhaa ikiwemo cha kukosa Wadhamini (endorsement) akiwemo Ally Mayay na Oscar Oscar.
20210616_164610.jpg
 
Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubery Ally amesema kwa mwaka wa pili mfulilizo mwaka huu pia hakutokuwa na Ibada ya Hijja kwa Wageni kutoka nje ya Saudi Arabia kutokana na Janga la Corona.

“Serikali ya Saudi Arabia kupitia Wizara yake ya Hijja wameona waifute Ibada ya Hijja kwa wanaotoka Nchi za nje, itafanyika kwa idadi ndogo ya Mahujaji Elfu 60, niwaambie Watanzania masuala ya Hijja mwaka huu hakuna Watu wajiandae kwa mwaka ujao, Mungu atupe subira juu ya jambo hili kwasababu huu ni mwaka wa pili hatuendi Hijja”———-Sheikh Zubery

Kwa kawaida Mahujaji takribani Milioni mbili kutoka Duniani kote hufika Makkah kutekeleza mojawapo ya nguzo tano za Kiislamu kila mwaka.
20210616_164802.jpg
 
“Yako yaliyofanyika mwaka jana na Mama yetu alikuwa Mshauri Mkuu wa Rais, dunia ilikumbwa na corona na tulitoka na masuluhisho yake, hakuna kuogopa… mbinu za mwaka jana zimefanya vizuri, wengine walitumia za magharibi na waliharibikiwa” ———Polepole.
20210616_164908.jpg
 
Israel imefanya mashambulizi ya anga kwenye Ukanda wa Gaza leo baada ya Wanamgambo wa Kipalestina kurusha maputo yenye vilipuzi kusini mwa Israel, haya ni mapigano ya kwanza kati ya pande hizo mbili tangu mapigano yasitishwe mwezi uliopita ambapo mamia ya Watu waliuawa.

Mashambulizi hayo ni ya kwanza chini ya Serikali mpya ya muungano inayoongozwa na Waziri Mkuu Naftali Bennett aliyechukua kiti Jumapili baada ya kuondolewa kwa Waziri Mkuu wa zamani Benjamin Netanyahu.

Kwa mujibu wa duru za Kipalestina, Jeshi la Israel lililenga eneo moja la mashariki mwa Khan Yunis kusini mwa Ukanda wa Gaza, ambako wanaishi Watu milioni mbili.
20210616_173134.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom