Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA imesema kupitia namba *106# Watanzania wanaweza kujua vitu mbalimbali ikiwemo kujua kama vitambulisho vyao vya NIDA vimetumika na Wahalifu kusajilia line nyingine za simu.
Vilevile Mtu anapobonyeza namba hiyo *106# anaweza kuangalia usajili, namba zilizosajiliwa mitandao yote kupitia kitambulisho chake cha Taifa, pia anaweza kufuta usajili wa laini ambayo haitaki na kufanya maombi ya kuongeza namba.
Namba hii ni mkombozi na itamrahisishia Mtu yeyote kujua 'status' ya matumizi ya kitambulisho chake cha Taifa palepale alipo na kwa haraka hasa kipindi hiki ambacho baadhi ya Mawakala wa usajili wamekosa uaminifu na kusajili laini kwa vitambulisho vya Watu bila idhini yao ambapo laini hizo hutumika kwenye uhalifu mbalimbali ikiwemo utapeli wa mitandaoni.
Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma imewahukumu Watu watatu adhabu ya kunyongwa hadi kufa baada ya kukutwa na hatia ya kumuua Mlinzi kwenye kampuni ya kichina iliyokuwa ikijenga barabara ya Kasulu-Kidawe wakati wakiiba kifaa aina ya control box.
Inaelezwa siku ya tukio watatu hawa walipanga kuiba kifaa hicho lakini wakati wakiiba walipata upinzani mkubwa kutoka kwa Mlinzi huyo (Richard Chija) ambapo mapambano yao yalisababisha Mlinzi kuumia na kutokwa damu nyingi kabla ya kufariki.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.