'Epuka sana kumchukia mtu anayezungumza kitu kibaya juu yako, huwezi kujua, kaamka leo kavurugwa hasira zake kakumalizia wewe, kesho mwenyewe akikaa atajuta na kukuomba msamaha'
•
Msanii wa Tanzania, Diamond Platnumz amewajibu wanaotaka aondolewe kwenye tuzo za BET, akisema ni mawazo yao na anayaheshimu.
•
'Mimi naheshimu mawazo ya kila mtu, mtu akinifurahia, akinitukana akinisema mimi nashukuru',
alisema Diamond kupitia kituo cha TV cha Wasafi.
•
Wanaompinga msanii huyo kupitia mitandao ya kijamii wanadaiwa kufanya hivyo ili kuonesha hisia zao kutokana na msanii huyo 'kushiriki siasa akikiunga mkono chama tawala cha CCM' nchini humo, kilichoshinda uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 unaolalamikiwa kuwa ulikuwa na udanganyifu.
Hata hivyo tume ya taifa ya uchaguzi Tanzania imepinga madai haya na kusema uchaguzi huo ulikuwa huru na wa haki.
•
Lakini pia wanadai kwamba msanii huyo yuko karibu na wanasiasa, wanaodaiwa kukiuka haki za binadamu.