Makapuku Forum

Makapuku Forum

"Zoezi lijalo la sensa katika nchi yetu kwa mara ya kwanza vutatumika vishikwambi (tablet) katika ukusanyaji wa takwimu na kuonesha maeneo ya kijografia, itapunguza muda wa kukusanya na kuchakata takwimu" Dkt. @mwigulunchemba1, Waziri wa Fedha na Mipango
Bajeti kuu
 
Bajeti kuu... “Eneo lingine ni kuimarisha kilimo cha umwagiliaji, uongezaji thamani ya mazao na upatikanaji wa masoko, kukuza sekta ya viwanda, kuziba mianya ya utoroshwaji wa madini na kuhamasisha ujenzi wa viwanda vinavyotumia rasilimali za hapa nchini,” - Waziri Dk Mwigilu Nchemba
 
Inapendekezwa posho za madiwani zianze kulipwa moja kwa moja kwenye akaunti zao

Bajeti kuu leo
 
"Napendekeza kuanzia mwaka mpya wa fedha 2021 /2022 posho ya shilingi laki moja ilipwe kila mwezi kwa maafisa tarafa kama posho za mafuta na matengenezo ya pikipiki" Dkt. @mwigulunchemba1, Waziri wa Fedha na Mipango
#BajetiyaSerikali20212022
 
"Napendekeza posho ya madaraka kiasi cha shilingi laki moja kilipwe kwa watendaji wa kata kuanzia mwaka mwa fedha 2021/2022" Dkt. @mwigulunchemba1, Waziri wa Fedha na Mipango
#BajetiyaSerikali20212022
 
“Serikali inatambua na kuthamini mchango wa watumishi wa umma na wa sekta binafsi katika kukuza Pato la Taifa, kwa kutambua hilo, Serikali itapunguza kiwango cha chini cha kutoza kodi ya mapato ya ajira (PAYE) kutoka 9% hadi 8%”———MWIGULU
 
"Kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 askari wetu watakuwa na mkataba wa miaka sita na kisha kuingia katika ajira ya kudumu, kutoka kuwa miaka 12 ambapo iliwapelekea kupata changamoto katika utumishi wao" Dkt. @mwigulunchemba1, Waziri wa Fedha na Mipango
#BajetiyaSerikali20212022
 
“Serikali itafuta tozo ya asilimia 6 iliyokuwa ikitozwa kwa ajili ya kulinda thamani ya mkopo wa elimu ya juu (Value Retention Fee) kwa wanufaika na kutenga jumla ya shilingi bilioni 449 kwa ajili ya kuwapandisha vyeo watumishi 92,619”———-MWIGULU
#BAJETI2021
 
"Tangu zoezi la kugawa vitambulisho kwa wajasiriamali, vitambulisho 2,300,000 vimetolewa kwa wajasiriamali na kuingiza shilingi bilioni 46.71" Dkt. @mwigulunchemba1, Waziri wa Fedha na Mipango
#BajetiyaSerikali20212022
 
Mawasiliano
20210610_165703.jpg
 
“Wazee wetu (Wastaafu) hupata shida sana baadhi yao hufadhiliwa malazi kwa kulala misikitini na makanisani na wengine hutegemea wahisani kuhudumia familia zao kinyume na mchango walioutoa katika ujenzi wa Nchi hii”———MWIGULU
 
“Wastaafu wetu walilitumikia Taifa hili kwa uzalendo, uadilifu na bidii kubwa sana, kumekuwa na changamoto za muda mrefu za ulipaji wa mafao yao kutokana na ufanisi mdogo wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii katika kuhudumia wastaafu wetu”———-MWIGULU
 
"Kupunguza kiwango cha kodi kwenye bia zinazotokana na shahiri inayozalishwa nchini kutoka shilingi 765 hadi hadi shilingi 620 kwa lita moja" Dkt. @mwigulunchemba1, Waziri wa Fedha na Mipango
#BajetiyaSerikali20212022
 
Serikali imepunguza kiwango cha chini cha kutoza kodi ya mapato ya ajira (PAYE) kutoka 9% hadi 8%. Hatua hiyo ni mwendelezo wa juhudi za Serikali za kupunguza mzigo wa kodi kwa wafanyakazi, ambapo kiwango hicho kimepunguzwa kutoka 11% mwaka
 
Kuhusu Zanzibar, napendekeza kufanya marekebisho ya Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ili kurudisha utaratibu wa kurejesha VAT kwa bidhaa zinazonunuliwa Tanzania Bara na kutumika Tanzania Zanzibar. #Bajeti2021
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom