Makapuku Forum

Makapuku Forum

Baraka zimeongeka kwa Mwanamfalme Harry Mtawala wa Sussex na mke wake Mergan baada ya kupata mtoto wao wa pili.


Harry na Meghan wamesema wamempatia mtoto jina la Lilibet ambalo ni jina la utani la Familia ya Kifalme kwa Malkia. Jina lake la kati, Diana, lilichaguliwa kumuenzi "bibi yake mpendwa", Malkia wa Wales.


Lilibet "Lili" Diana Mountbatten-Windsor alizaliwa Ijumaa asubuhi katika hospitali ya Santa Barbara, California.

Kasri ya Buckingham Palace imesema: "Malkia, Manamfalme wa Wales na Duchess wa Cornwall, na mtawala wa Cambridge na mkewe wamefahamishwa na wamefurahishwa na taarifa hizo."

20210607_184748.jpg
20210607_184808.jpg
20210607_184827.jpg
 
Alizaliwa kama Temitope Balogun Joshua mnamo tarehe 12 mwezi Juni katika jimbo la Ondo nchini Nigeria.

Kulingana na Mtandao wa kanisa lake la SCOAN , Joshua alikuwa ndani ya tumbo la mamake kwa miezi 15 kabla ya kuzaliwa kwake.

Akiwa shuleni alijulikana kama muhubiri mdogo kutokana na alivyokuwa akiipenda Biblia na uwezo wake wa kutabiri matukio yaliofanyika katika jamii yake , kwa mujibu wa mtandao wa SCOAN.

Alianzisha kanisa la SCOAN mwaka 1987 akiwa na waumini wachache kabla ya kanisa hilo kupanuka hadi kimataifa.

Mwaka 2009 TB Joshua alianzisha klabu ya kandanda kwa jina My people FC katika juhudi za kuwasaidia vijana.

Kulingana na jarida la Forbes 2011 , Temitope Joshua ni muhubiri wa tatu tajiri nchini Nigeria akiwa na thamani ya $15m.

TB Joshua ana makanisa mengi katika mataifa tofauti barani Afrika na Marekani ya kusini.

Mungu amechukua maisha ya muhudumu wake TB Joshua. Amefariki akimtumikia Mungu, imeandika taarifa rasmi kutoka SCOAN na kuongeza kuwa maneno ya mwisho ya TB Joshua alisema
“Watch and Pray” “One life for Christ is all we have”.
20210607_184957.jpg
 
Pambano la raundi nane bila mshindi.
Pambano kati ya masumbwi Floyd Mayweather Jr na Logan Paul halikutarajiwa kuwa bila mshindi.

Wengi walidhani Paul atatolewa katika hatua za Knock Out lakini aling’ang’ana hadi roundi ya nane.

Pambano hilo halikuwa la ushindani, lilikuwa la maonyesho na hakutangazwa mshindi kwa kuwa halikuwa na jaji.
20210607_185427.jpg
 
Kinachowashangaza wengi ni kwamba TB Joshua alikuwa amesema kuwa hataadhimisha siku yake ya kuzaliwa.

Katika video iliyowekwa mtandaoni baada ya kutangazwa kwa kifo chake Joshua anaonekana akijiimbia wimbo wa 'happy birthday'
20210607_184957.jpg
 
Mwigizaji Kajala Masanja ametoa tamko leo akisema hausiki na picha inayosambaa inayoonesha Wanawake wawili wakiwa uchi wa mnyama kwenye mkao usiofaa huku akisema picha hiyo ime-editiwa na kuwekwa kichwa chake ama kinachofanana na chake na Watu wakidai picha ni ya Kajala na Mwanae Paula.

“Sijawahi na sitawahi kupiga picha ya namna hiyo na Binti niliyembemba tumboni miezi tisa na kumpa kwa uchungu, huenda nina kasoro nyingi kwa wengine lakini msisahau kitu kimoja Mimi bado ni Mama na uchungu wangu kwa Paula ni kama wa kwako wewe unayesoma post hii kwa Mwanao”——
20210607_200044.jpg
20210607_200118.jpg
 
Mwanasiasa mkongwe na machachari, Dk Chrisant Majiyatanga Mzindakaya amefariki dunia jana jioni alipokuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza kwa simu na Mwananchi jana, mdogo wa marehemu, Meja Mstaafu Christopher Mzindakaya alikiri kutokea msiba huo mkubwa katika familia na kusema taratibu nyingine za maziko zitatolewa baada ya kikao cha wanafamilia.
Alisema Dk Mzindakaya alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya moyo, hivyo kufanyiwa upasuaji na kulazwa Muhimbili kwa zaidi ya wiki tatu sasa.
20210608_092225.jpg
 
Wanawake wa mkoa wa Dodoma leo wamefurika katika ukumbi wa JK convention uliopo jijini Dodoma kwa ajili ya kumsikiliza Rais Samia Suluhu Hassan ambaye atazungumza na kundi hilo.

Idadi ya Wanawake wengi imejitokeza ambapo wengi wamelazimika kukaa kwenye mahema yaliyofungwa katika viwanja vinavyotumika kama maegesho ya magari.
20210608_092337.jpg
 
Wanawake wa mkoa wa Dodoma leo wamefurika katika ukumbi wa JK convention uliopo jijini Dodoma kwa ajili ya kumsikiliza Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ambaye atazungumza na kundi hilo nchini.
20210608_092513.jpg
20210608_092534.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom