RACISM] Mwanasoka Kinda Seid Visin aliewahi kucheza timu za vijana AC Milan amejiua baada ya kubaguliwa huko nchini Italia
Seid kabla ya kuchukua maamuzi ya kujiua aliandika ujumbe kutokana na maamuzi yake, ujumbe ulisomeka ifuatavyo;
"Sikuja nchini Italia kwa kupenda bali nilichukuliwa kutoka nyumbani Ethiopia na wazazi wawili wa Kiitaliano (Adoption) wakanileta huku kama Mtoto wao"
"Mwanzoni maisha nchini Italia yalikuwa mazuri na kila Mtu alinipenda ila mambo yalianza kubadilika punde baada ya kupata ajira ya kufanya kazi hotelini"
"Wateja walisusia huduma yangu, wengi niliowahudumia walinifukuza kama Mbwa, huko viwanjani pia kila siku ilikuwa ni ubaguzi dhidi ya rangi yangu na Uafrika wangu"
"Nilitengwa kila sehemu, haswa Watoto wa Kiitaliano ambao hawana kazi ila Mimi sikuwahi kuchagua kazi, hivyo nimeamua kukatisha maisha yangu kwakuwa sina wa kumlilia wala wa kunisaidia"
Maandishi kwenye kikaratasi yalisomeka hivyo, ametangulia akiwa na umri wa miaka 20 tu
REST IN PEACE SEID