Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema wanaopaswa kuhudhuria shughuli za maziko nchini humo wasizidi 20———“wimbi la pili la Corona limekuja kwa kasi tuchukue tahadhari, sio mazishi tu hadi harusini sherehe zisizidi Watu 20”

“Baa, Disco, Cinema pia marufuku, Askari watapita huko watakaokutwa hatuna haja ya kuwajaza kwenye Mahabusu zetu watapigwa faini kubwa za Pesa ambazo zitawafanya wasirudie makosa”———Museveni
20210607_152613.jpg
 
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema wanaopaswa kuhudhuria shughuli za maziko nchini humo wasizidi 20———“wimbi la pili la Corona limekuja kwa kasi tuchukue tahadhari, sio mazishi tu hadi harusini sherehe zisizidi Watu 20”

“Baa, Disco, Cinema pia marufuku, Askari watapita huko watakaokutwa hatuna haja ya kuwajaza kwenye Mahabusu zetu watapigwa faini kubwa za Pesa ambazo zitawafanya wasirudie makosa”———Museveni
20210607_152722.jpg
 
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema wanaopaswa kuhudhuria shughuli za maziko nchini humo wasizidi 20———“wimbi la pili la Corona limekuja kwa kasi tuchukue tahadhari, sio mazishi tu hadi harusini sherehe zisizidi Watu 20”

“Baa, Disco, Cinema pia marufuku, Askari watapita huko watakaokutwa hatuna haja ya kuwajaza kwenye Mahabusu zetu watapigwa faini kubwa za Pesa ambazo zitawafanya wasirudie makosa”———Museveni
20210607_152828.jpg
 
Marais 100 wa zamani wa Nchi mbalimbali duniani pamoja na Mawaziri wa zamani wakiwemo Mawaziri Wakuu wamelihimiza kundi la Mataifa 7 tajiri duniani - G7 kulipia kampeni za chanjo ya corona Duniani ili kuzuia virusi kubadilika na kurejea kama kitisho cha Ulimwengu.

Viongozi hao wametoa ombi lao kabla ya mkutano wa kilele wa G7 nchini England ambao utaanza Ijumaa wiki hii ambapo Rais wa Marekani Joe Biden atakutana na viongozi wa Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Canada na Japan.

Katika barua yao kwa G7, Viongozi hao wa zamani wamesema ushirikiano wa kimataifa umeshindwa katika mwaka wa 2020 lakini 2021 unaweza kuleta enzi mpya, miongoni mwa Viongozi waliotia saini zao ni Mawaziri wakuu wa zamani wa Uingereza Gordon Brown na Tony Blair, Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon na Viongozi wa zamani 15 wa Afrika.
20210607_152944.jpg
 
Ripoti mpya ya mauaji ya Watu kwa kutumia risasi Nchini Marekani inasema idadi ya waliouwawa kwa mwaka 2021 pekee katika mashambulizi yapatayo 240 ni Watu zaidi ya 8,400.

Vifo vingine vilitokea weekend hii iliyopita baada ya Watu watano kuuwawa kwa risasi kwenye Mji ws Chicago huku 40 wakijeruhiwa, Watu wengine 8 wamejeruhiwa huko New Orleans Jumapili asubuhi wakati mmoja amefariki huko Salt Lake, Utah.

Huko Indianapolis, Indiana wamefariki Watu watatu katika shambulizi siku ya Jumamosi ambako Watu hao walipigwa risasi wakiwa kwenye maegesho ya magari.
20210607_153055.jpg
 
Vichwa viwili vya binadamu na mabaki mengine ya miili yaliachwa katika vituo vya kupigia kura jana katika mji wa Tijuana jijini Mexico wakati wa uchaguzi, mamlaka zimesema.

Saa moja baada ya uchaguzi kuanza, mtu mmoja alirusha kichwa cha mtu katika kituo cha kupigia kura, akivuruga upigaji kura wakati walipoitwa, waendesha mashtaka katika jimbo la Baja California walisema.

Masaaa mawili baadaye, katika kituo kingine cha kupigia kura, mtu mmoja aliacha kichwa kingine na mabaki ya mwili ndani ya boksi la mbao lililowekwa pembeni ya boksi la kutumbukiza kuza.

Mabaki zaidi ya miili ya binadamu yaligunduliwa yakiwa katika mikoba karibu na kituo cha tatu za kupigia kura, kwa mujibu wa ofisi ya mwendesha mashtaka wa Baja California.
20210607_153253.jpg
 
Mbunge wa Viti Maalumu, Halima Mdee akizungumza bungeni alipokuwa akichangia mjadala wa kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa mwaka wa fedha 2021/2022, jijini Dodoma leo.
20210607_153425.jpg
 
Ili kutekeleza vipaumbele vya mwaka 2021/22 kwa ufanisi, Wizara ya Fedha na Mipango inaomba kuidhinishiwa matumizi ya jumla ya shilingi 12,961,271,473,000 kwa Mafungu yote saba (7). Kati ya fedha hizo, shilingi 11,935,643,022,000 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na shilingi 1,025,628,451,000 ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.
20210607_153546.jpg
 
Wizara ya Fedha na Mipango inaomba kuidhinishiwa matumizi ya jumla ya shilingi 12,961,271,473,000 kwa Mafungu yote saba (7). Kati ya fedha hizo, shilingi 11,935,643,022,000 ni kwa ajili ya matumizi ya Kawaida na shilingi 1,025,628,451,000 ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.
20210607_153647.jpg
 
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amesema ni marufuku kumfukuza mwanafunzi shule wakati wa utekelezaji wa waraka wa elimu namba tatu wa mwaka 2016 unaoelezea utaratibu wa kutoa michango shuleni.
Waraka huo namba tatu wa mwaka 2016 unaainisha majukumu ya jamii na wananchi kuhusu michango.

Profesa Ndalichako alikuwa akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Nkasi Kaskazini (Chadema) Aida Khenani ameitaka Serikali kueleza wananchi kuwa kilichobadilika ni ada tu badala ya kutamka kuwa elimu ni bure.

Pia, ametaka kujua kuwa Serikali haioni haja ya kufanya tathimini upya ya utaratibu huo wakiwashirikisha wadau wa elimu ili kufahamu changamoto ni nini badala ya ada pekee.
20210607_153807.jpg
 
Spika wa Bunge, Job Ndugai akizungumza bungeni alipokuwa akiwaonya wabunge kutoleta taarifa za kutambulishwa bungeni waume au wake za watu wakidai ni waume au wake zao, alipokuwa akiongoza kikao cha bunge la bajeti, jijini Dodoma leo. Ndugai amesema amepokea malalamiko kutoka kwa wananchi wakidai waume zao wametambulishwa bungeni kuwa ni waume wa wabunge.
20210607_153927.jpg
 
Mshambuliaji wa Azam FC, Prince Dube ametajwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Mei akiwazidi Erick Mwijage wa Kagera Sugar na Kipanwa Yanga, Metacha Mnata.

Kocha wa Azam,George Lwandamina amekuwa kocha bora akiwazidi Francis Baraza wa Kagera Sugar na Abdallah Mohamed wa JKT Tanzania.
Tuzo ya meneja bora wa Uwanja imeenda kwa Sikitu Kilakala ambaye ni meneja wa uwanja wa Azam Complex.
20210607_154042.jpg
 
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amefuta mashamba 11 yenye hekari 24,119 na kufufua mengine 49 yenye hekari 45,788.5 wilayani Kilosa mkoani Morogoro.

Mbali na kufuta na kufufua mashamba hayo, imeundwa timu ya wataalamu kutoka Wizara ya Ardhi na wataalamu wa mkoa na wilaya ili kufanya uhakiki na kupanga matumizi bora ya ardhi yatakayosaidia wananchi.

Waziri wa Ardhi, William Lukuvi ametangaza maamuzi hayo ya Rais ya kufutwa na kufufuliwa mashamba hayo Juni 7,2021 wakati wa kikao na watendaji pamoja na madiwani wa halmashauri ya Wilaya ya Kilosa kwenye ziara yake ya siku moja.
20210607_161700.jpg
 
Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Pwani imewakamata Wahamiaji wasio na vibali 43 wakiwemo Wasomalia na Waethiopia ambao waliingia nchini kinyume na taratibu zilizowekwa.

Afisa Uhamiaji Mkoa wa Pwani, Omary Hassani amesema Wahamiaji hao walitumia Majahazi wakitoka Mombasa mpaka Bagamoyo kwa kutumia Bandari Bubu ambapo walishuka kwenye Majahazi na kutembea kwa saa 24 porini mpaka kijiji cha kidomole fukayose walipokamatiwa wakisubiri usafiri wa kuwasafirisha kwenda mpakani mwa Tanzania ili waendelee na safari yao ya kwenda South Africa.

Omary amesema wanawashikilia pia Watanzania wanne ambao wanahusika kuwasafirisha Wahamiaji hao ambao wote walikamatwa June 6, 2021 na leo watafikishwa katika Mahakama ya Wilaya Bagamaoyo.
20210607_161810.jpg
 
"Waraka namba 3 wa mwaka 2016 umeainisha bayana wajibu wa Wazazi katika kushiriki kwenye kuchangia maendeleo ya Shule, nitoe wito kwa Wazazi kuendelea kuona umuhimu wa kushirikiana na Serikali, kikubwa Mwanafunzi asifukuzwe Shule kwasababu ya michango hii ni marufuku”———Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Joyce Ndalichako wakati wa maswali na majibu Bungeni leo
20210607_162028.jpg
 
Mwanamke mmoja amefariki dunia baada ya mlinzi wa zamani wa hospitali kujifanya daktari na kumfanyia upasuaji, polisi wamesema leo Jumatatu.

Shameema Begum, akiwa na miaka 80, alifariki Jumapili, wiki mbili baada ya Muhammad Waheed Butt kujaribu kumtibu jeraha lililokuwa mgongoni katika hospitali ya serikali iliyopo jijini Lahore, mashariki mwa Pakistan.

"Hatuwezi kujua kila daktari na kila mtu anachofanya wakati wote. Ni hospitali kubwa," alisema ofisa utawala wa hospitali hiyo ya Mayo iliyoko Lahore na ambaye hakutaka jina lake litajwe.

Alisema haikueleweka ni upasuaji wa aina gani ambao mlinzi huyo alimfanyia mgonjwa ndani ya chumba cha operesheni, ambako wataalamu waliofuzu taaluma ya udaktari walikuwepo.

Hospitali za serikali za Pakistan, ambako wagonjwa hutakiwa kulipa kiasi cha fedha kwa ajili ya matibabu, mara kadhaa zinaweza kukosa ufanisi na kuwa na matatizo.

Familia ya Begum ilimlipa Butt kwa ajili ya upasuaji huo, na alitembelea nyumbani mara mbili zaidi kufunga jeraha la mwanamke huyo.

Lakini wakati damu ilipovuja kwa wingi na maumivu kuzidi, familia yake ilimrudisha hospitalini, ambako waligundua kilichotokea.

Mwili wake unahifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi kujua kama kifo chake kilisababishwa na matatizo yaliyotokana na upasuaji huo.

"Mlinzi ameshtakiwa na yuko mahabusu polisi," alisema msemaji wa polisi wa Lahore, Ali Safdar alipoongea na AFP.
"Butt alijifanya daktari na zamani alitembelea nyumbani kwa wagonjwa wengine."
20210607_180751.jpg
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla leo June 07 amefanya kikao Cha pamoja na watumishi wa mkoa huo kwa lengo la Kuweka mipango ya kusukuma mbele gurudumu la maendeleo kwa maslahi mapana ya wananchi katika mkoa huo na kuwapatia agenda tano za kufanyia kazi.
20210607_181001.jpg
 
Kanali Assimi Goita ataapishwa hii leo kuwa rais wa mpito wa Mali, kufuatia mapinduzi ya pili ndani ya kipindi cha miezi tisa licha ya ukosoaji wa kimataifa wa kile kinachoelezwa kuwa ukwapuaji wa madaraka.

Hotuba ya kuapishwa kwa Goita mwenye umri wa miaka 37 itafuatiliwa kwa umakini wa wanadiplomasia ili kujua ikiwa atatoa ahadi ya dhati juu ya namna miezi minane iliyosalia kwenye kipindi cha mpito itakavyokwenda.

Serikali iliyowekwa baada ya mapinduzi ya kwanza ya Goita Agosti mwaka jana iliahidi kuifanyia mabadiliko katiba kufikia mwezi Oktoba na kuandaa uchaguzi Februari mwakani. Goita aliwafuta kazi rais na waziri mkuu wa serikali ya mpito Mei 24 na kusababisha nchi hiyo kusimamishiwa uanachama na Umoja wa Afrika.
20210607_184509.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom