Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kiungo wa Yanga Carlos Stenio Fernandes “Carlinhos” ameachana na Yanga SC na kurejea kwao Angola, hiyo ni baada ya kuomba kuvunja mkataba wa club hiyo, tetesi zinadai chanzo cha mchezaji huyo kuomba kuvunja mkataba ni kushindwa kuzoea maisha ya Tanzania ikiwemo vyakula.View attachment 1803488
20210531_135449.jpg
 
Shirika la Habari la China linaripoti kuwa chama cha Kikomyunisti cha China kitalegeza msimamo na kuwakubalia Wapenzi/Wanandoa kuzaa Watoto watatu badala ya wawili kutokana na idadi ya Wazee kuongezeka nchini humo.

Tangazo hilo linafuatia takwimu za sensa zilizoonesha kuwa idadi ya Wachina walio katika umri wa kufanya kazi imepungua katika kipindi cha mwongo mmoja uliopita huku idadi ya Watu walio na zaidi ya umri wa miaka 65 ikiwa imeongezeka.

Jambo hili limewekea shinikizo dhidi ya uchumi na jamii, Chama hicho Tawala cha China kiliweka vikwazo vya idadi ya Watoto kwa wazazi tangu 1980 ili kudhibiti idadi ya Watu nchini humo.

Mwaka 2015 vikwazo vya Wazazi kuwa na Mtoto mmoja viliondolewa na idadi hiyo ikaongezwa na Wazazi wakakubaliwa kuwa na Watoto wawili.
20210531_135616.jpg
 
Usiku wa kuamkia leo Mwimbaji Staa wa Bongofleva Nandy amelionesha Jumba la Nandy Festival Masaki Dar es salaam ambalo limechukuliwa maalum kwa ajili ya kukaa Wasanii wote wanaoshiriki Nandy Festival 2021 na watakaa hapo mpaka safari yao ya kwenda Kigoma ambako Nandy Festival inafanyika weekend ijayo June 5, nyama zinachomwa Watu wanakunywa na Wasanii wote kila mmoja anapewa chumba chake.

Sasa Habari nyingine njema kwa Mashabiki wa Nandy na wale wa Mwimbaji Staa AliKiba ni kwamba leo Alikiba amethibitisha kuwa atakuwepo nyumbani kwao Kigoma kumpa support ya nguvu zote Nandy.

“Sanaa yetu ina upungufu wa wasanii wa kike, inabidi waliopo wapewe nguvu ili waweze kufanikiwa zaidi, ni Msanii anayejituma na mwenye jitihada, Napenda anachofanya na ndio maana Jumamosi ijayo nitaenda nyumbani Kigoma kumpa support katika Nandy Festival”——— Ali Kiba
20210531_135752.jpg
20210531_135808.jpg
 
Kiungo wa Yanga Carlos Stenio Fernandes “Carlinhos” ameachana na Yanga SC na kurejea kwao Angola, hiyo ni baada ya kuomba kuvunja mkataba wa club hiyo, tetesi zinadai chanzo cha mchezaji huyo kuomba kuvunja mkataba ni kushindwa kuzoea maisha ya Tanzania ikiwemo vyakula.View attachment 1803488View attachment 1803489
utopolo kwenye ubora wao
 
Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimezindua kamati ya ushauri ya wadau wa kisekta itakayofanya kazi na kituo cha umahiri cha mafunzo ya taaluma za usafiri wa anga na operesheni za usafirishaji.

Akizungumza katika uzinduzi huo mkuu wa chuo hicho, Profesa Zacharia Mganilwa amesema kamati hiyo imezingatia mahitaji ya sekta binafsi ambapo asilimia 50 ya wajumbe wake wanatoka kwenye sekta binafsi.View attachment 1798310
....utopolo mwingine huu, huu ushauri wa kamati utasaidia nini ikiwa ni ATCL pekee ndio inaachwa itamalaki bila ushindani wa maana!?
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amewataka Madiwani wa Jijini la Dar es salaam kuepuka migongano na mivutano isiyokuwa na faida yoyote kwa Wananchi na badala yake wajikite Katika kujenga hoja na mipango ya kutatua kero kwa maslahi mapana ya Wananchi.

RC Makalla amesema kumekuwa na katabia ka ajabu pale Serikali inapotoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi fulani, Madiwani wanajikuta wanaanza kulumbana kwa Mambo yasiyokuwa na msingi Jambo linalochelewesha kuanza kwa miradi ya maendeleo na kuleta usumbufu kwa Wananchi.

Akizungumza wakati wa kikao cha pamoja kati yake na Madiwani pamoja na Maafisa Watendaji kata, RC Makalla amewataka Viongozi hao kusimamia kikamilifu suala la usafi katika maeneo yao na kuwa mstari wa mbele kwenye usimamizi wa miradi ya maendeleo.

Makalla pia ameonesha kufurahishwa na mafanikio makubwa yanayoendelea kupatikana katika Operesheni tokomeza Majambazi na Vibaka Dar es salaam ambapo amewahakikishia Wananchi kuwa Serikali imejidhatiti kuwalinda na Mali zao.
20210531_220030.jpg
20210531_220102.jpg
20210531_220122.jpg
 
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Simon Sirro amefanya mabadiliko madogo kwa Makamanda wa Polisi, ili kujaza nafasi zilizoachwa wazi.

Katika mabadiliko hayo, Naibu Kamishna wa Polisi Lucas Mkondya amehamishwa kutoka kuwa Kaimu Kamishna wa Fedha na Logistiki Makao Makuu ya Polisi Dodoma kuwa Mkuu wa Usalama Barabarani nchini na RPC Rufiji, Onesmo Lyanga amehamishwa kwenda kuwa RPC Dodoma kuchukua nafasi ya Kamanda Gilles Muroto ambaye anastaafu.

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Ramadhan Ngh'anzi amehamishwa kutoka kuwa Boharia Mkuu kwenda kuwa RPC Mwanza, huku Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Mwamini Rwantale akihamishwa kutoka Kanda Maalum ya Dar es Salaam ambako alikuwa Mkuu wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimali watu kwenda kuwa Kamanda wa Polisi Kikosi cha Tazara.
20210531_223325.jpg
 
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Simon Sirro amemuhamisha RPC wa Mwanza, Muliro Jumanne kuja kuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Kamishna wa Polisi Camillius Wambura ambaye ameteuliwa na Rais Samia Suluhu kuwa DCI.

Kamishna Msaidizi wa Polisi Zuberi Chembera yeye amehamishwa kutoka Makao Makuu ya Upelelezi Dodoma kwenda Makao Makuu ya Polisi Zanzibar kuwa Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa jinai Zanzibar kuchukua nafasi ya Kamishna wa Polisi Hamad Khamis Hamad.

Kamishna Msaidizi wa Polisi Stella Richard amehamishwa kutoka kuwa Kamanda wa Kikosi cha Polisi Tazara kwenda kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida.
20210531_225721.jpg
 
FC Barcelona wamemtambulisha rasmi Sergio Aguero baada ya kusaini mkataba wa kujiunga na kikosi chao hadi 2023, Aguero anajiunga na FC Barcelona baada ya kudumu na Man City ya England kwa miaka 10 (2011-2021)
20210531_230035.jpg
20210531_230054.jpg
20210531_230112.jpg
20210531_230135.jpg
 
Haya ni mambo manne aliyoyazungumza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Innocent Bashungwa leo Bungeni kuhusu mipango ya marekebisho kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) dhidi ya Wazalisha maudhui mitandaoni.

“TCRA itaendelea kuweka mazingira maridhawa ya kuendeleza sekta ya habari na utangazaji kwa kupitia kanuni mbalimbali zinazosimamia sekta ya Utangazaji kwa ajili ya kuboresha huduma za Utangazaji nchini ambapo ili kutimiza azma hiyo Wizara itafanyia kazi hoja 13 kutoka kwa wadau ambazo zimekuwa changamoto katika utoaji wa huduma za utangazaji nchini”———Bashungwa.

“Hoja hizo ni pamoja na kuhakikisha kuwa Wasanii, Wabunifu na wale wasiojihusisha na masuala ya utoaji wa Habari mtandaoni (news and current affairs) wanatoa huduma mtandaoni na wanapata fursa ya kuimarisha maudhui ya ndani ikiwa ni pamoja na Wasanii kutangaza kazi zao bila tozo zozote ili mradi wanazingatia sheria za Nchi”———BASHUNGWA

“Hoja nyingine za kufanyiwa kazi ni pamoja na kuimarisha muundo wa TCRA ili uweze kusimamia ipasavyo masuala ya utangazaji, kupunguza gharama za tozo kwa Televisheni za mtandaoni na watoa huduma wengine wa mitandaoni, kuwa na kisimbuzi kimoja, kuangalia suala la adhabu kali zinazotolewa kwa vituo vya Radio/TV kupitia kamati ya maudhui pamoja na vyombo vya habari vya dini kuchukuliwa kuwa ni vya kibiashara na wengi kucheleweshwa kuruhusiwa kuongeza ukubwa wa leseni zao (mfano kutoka leseni ya Wilaya hadi leseni ya Kitaifa)”———Waziri Bashungwa.

“Hoja nyingine ni kuimarisha usalama wa akaunti za Wasanii wenye wafuasi wengi ili zisiweze kuibiwa na kuuzwa (hacked) pamoja na kukamilisha mfumo wa paamoja wa kufuatilia haki za Wasanii katika Televisheni na Radio”———Waziri Bashungwa.
20210531_230316.jpg
 
Kamanda wa Polisi Shinyanga Debora Magiligimba amethibitisha taarifa za kufariki kwa Idd Masasi (43) aliyetajwa kuwa Jambazi sugu ambae alikua na makazi Kigamboni Dar es salaam na Ndembezi Shinyanga akitajwa kuhusika na matukio ya unyang'anyi wa kutumia silaha.

"Tarehe 30 May 2021 Polisi Shinyanga lilipata taarifa fiche za uwepo wa Jambazi huyo ambae alikua anatafutwa kwa muda mrefu, matukio haya hasa alikua akiyafanya Dar es salaam na alikimbilia hapa Shinyanga baada ya kufanya ujambazi Kigamboni, kumbukumbu zinaonesha kwamba Jambazi huyu alishawahi kuhukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la unyang'anyi mwaka 2011 lakini alitumikia adhabu hiyo gereza la Butimba Mwanza kwa muda mfupi na akatoka baada ya kukata rufaa"

"Polisi Shinyanga kwa kushirikiana na kikosi kazi kutoka Dar es salaam baada ya kupata taarifa zake kiliweka mtego maeneo ya nguzo nane na ilipofika saa tano asubuhi Jambazi huyo alifika eneo hilo ambapo alipobaini kwamba anafatiliwa na Polisi alianza kukimbia, Polisi walimuonya kwa kupiga risasi mbili hewani lakini hakusimama ndipo wakafyetua risasi ambazo zilimjeruhi mguu wa kushoto na mgongoni na wakamkamata, alifariki akiwa anatibiwa Hospitali" ——— RPC Debora Magiligimba.
20210531_230455.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom