Makapuku Forum

Makapuku Forum

20210601_060953.jpg
20210601_061018.jpg
 
UNAAMBIWA:

Wapo Watu wengi wenye umri mkubwa Duniani na na mmoja wao ni Bibi Kizee kutoka nchini Nepal anayeitwa Batuli Lamichhane aliyezaliwa March 1903, kwa sasa ana Miaka 118 na bado anaonekana mwenye nguvu licha ya kuanza kuvuta sigara tangu akiwa na Miaka 17 (mwaka 1920) hadi leo.

Anapoulizwa swali la ni kwanini haachi sigara Batuli hujibu kuwa ———“Madaktari ambao tangu napata akili walinishauri nisivute sigara kwakuwa ni hatari kwa afya yangu wote wamefariki Dunia na Mimi bado nadunda kabisa, sasa kwanini niache kujipa raha kwa kuvuta!?”

Batuli huvuta sigara 30 kwa siku na anasema siri kubwa ya kuendelea kuwa na nguvu na mwenye afya licha ya umri wake ni kutoendekeza stress za ajabuajabu——-“Vijana wa sasa wana stress sana ndio maana hawaishi maisha marefu unatakiwa kujipa raha mwenyewe na kuwa na furaha wakati wote (no stress) hapo utaishi maisha marefu yenye afya tele”
20210601_104745.jpg
 
UNAAMBIWA:

Mwaka 2005 Shabiki kindakindaki wa Liverpool Mark Houghton (43) alijinyonga hadi kufa wakati wa Half Time, nyumbani kwake baada ya kile kilichodaiwa chanzo ni Timu yake kupigwa 3-0 na Ac Milan kwenye Fainali za Champion League, baadaye wakati wa kipindi cha pili Liverpool ilikuja na nguvu zote na ikaibuka Mshindi baada ya Mechi kwenda hadi hatua ya Penalties.

Mark alikutwa usiku na Mpenzi wake Jacqueline akiwa amejinyonga kwa kutumia mkanda usiku May 25,2005 katika eneo la Darwen, Lancashire, Uingereza
20210601_104926.jpg
 
UNAAMBIWA:

Mchungaji Lee Jong-Rak kutoka Korea Kusini ametengeneza Kisanduku cha kuwekea Watoto ambacho kimeunganishwa na upande mwingine wa nyumba yake, lengo ni kwamba Watu wote ambao wanataka kutupa Watoto wao vichanga au Watoto wenye matatizo ya akili wawe hata kwa siri wanawaweka hapo badala ya kuwatupa Barabarani wakaishia kufariki Dunia.

Tangu mwaka 1998 Lee ameshawaleta Watoto wengi kuwaonesha upendo na kuwapeleka shule na anapambana na mambo yote ikiwemo kuwabadilisha diapers na kuwabmbeleza usiku wakilia akishirikiana na Mkewe na Wafanyakazi wachache, kwa saa anao Watoto zaidi ya 20 nyumbani kwake, mdogo kabisa ana miezi miwili na mkubwa miaka 18.

“Hauna haja ya kumtupa Mtoto asiye na hatia Kama umeshindwa kumlea mlete tutamtunza” ———Lee
20210601_105103.jpg
20210601_105122.jpg
20210601_105142.jpg
20210601_105158.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom