Makapuku Forum

Makapuku Forum

20210524_114117.jpg
 
Nahodha wa Simba SC amepewa zawadi ya Tsh milioni 2.5 kwa kuwa mchezaji bora wa mechi (Man Of The Match) upande wa Simba SC katika mchezo dhidi ya Kaizer Chiefs.

Bocco kwenye mchezo huo wa robo fainali alifunga magoli mawili katika ushindi wa 3-0 wa Simba dhidi ya Kaizer Chiefs lakini Simba walitolewa kwa aggregate ya 4-3, zawadi hiyo imetoka kwa mdhamini wao Emirate Aluminium
20210525_042912.jpg
20210525_042935.jpg
 
Mfanyabiashara Fred Ngajiro maarufu kama Fred Vunjabei amepitishwa na Baraza Kuu la UVCCM kuwa Mwenyekiti mpya wa kamati ya Uchumi, Uwezeshaji na Fedha kupitia kikao cha Baraza Kuu ambacho kimemalizika jana Makao Makuu ya CCM Dodoma.

Kamati ya utekelezaji chini ya Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Komredi Kheri James ilikuja na pendekezo la jina la mwenyekiti huyo wa kamati ambapo baadae alithibitishwa na wajumbe kwa kura nyingi za ndio, Katibu wake ni Rose Manumba na pia Baraza lilichagua Wajumbe wengine wanne wa kamati kutoka Bara na Visiwani.

Katibu Mpya wa Hamasa na Chipukizi UVCCM Taifa ni Victoria Charles Mwanziva ambaye jina lake limeridhiwa na Baraza Kuu Taifa kuelekea Mabadiliko ya Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM Taifa.
20210525_043246.jpg
20210525_043327.jpg
 
Hizi ni picha kutoka IKULU Dar es salaam zikionesha Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwa na Mfanyabiashara Alhaji Aliko Dangote pamoja na Viongozi mbalimbali wa Tanzania baada ya kikao kilichofanyika IKULU leo.
20210525_043449.jpg
20210525_043510.jpg
20210525_043530.jpg
20210525_043844.jpg
 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Selemani Jafo amewateua Watangazaji wa Clouds Media Group Millard Ayo na kuwa Mabalozi wa Uhamasishaji Utunzaji wa Mazingira Nchini.

Waziri Jafo akiwa Dodoma amesema Mabalozi hao wameteuliwa kutokana na ushawishi wao kwa Jamii ili kuhamasisha utunzaji wa mazingira na upandaji miti.

Mabalozi wengine walioteuliwa ni pamoja na Haji Manara, Antonio Nugaz, Nandy, Harmonize, Idris Sultan, Monalisa, Mbunge Esther Matiko, Mbunge Joseph Musukuma, Diamond Platnumz, Mwandishi wa Radio Uhuru Sakina Abdulmasoud na May Zumo.
20210525_043959.jpg
 
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Queen Sendiga amekabidhiwa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Mwenyekiti wa CCM Iringa Dr. Abel Nyamahanga.

Queen Sendiga ameahidi kufanyakazi kwa ushirikiano bila ya kujali tofauti ya Vyama na kusema ataifuata Ilani hiyo ambayo ni ya Chama kilichopo madarakani.

Queen ni Mwanachama wa Chama cha ADC na mwaka 2020 aligombea Urais kwenye Uchaguzi Mkuu kupitia ADC.
20210525_044213.jpg
20210525_044240.jpg
20210525_044310.jpg
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Ruvuma limethibitisha kutokea kwa vifo vya Watu wa sita wa familia moja waliofariki kwa kuzama Mto Ruvuma katika kijiji cha Mkalawa Wilayani Nyasa walipokua wanavuka kuelekea shambani kwa kutumia Mtumbwi uliotengenezwa na magome ya miti May 22, 2021.

RPC wa Ruvuma Simon Maigwa amesema mpaka sasa wamepata mwili mmoja ambao ni wa Mtoto wa mwaka mmoja na wengine bado wanatafutwa na timu ya uokoaji———-“Ule Mto maji yake yana rangi nyekundu na una mamba yawezekana wameliwa au wamehamishiwa eneo jingine”
20210525_044456.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom