Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mwaka 1977, Pradyumna Kumar Mahanandia, msanii wa India, aliendesha baiskeli kwa miezi minne na wiki tatu kutoka New Delhi hadi Gothenburg huko Sweden ili kwenda kukutana na mpenzi wake Charlotte Von Schedvin.

Alienda kwa baiskeli kwasababu hakuwa na pesa za kutosha kununua tiketi ya ndege. Baadae Walioana na sasa wana watoto wawili.

babe wangu fanya na hii mvua basi ukuje umeona mapenzi hayo
20210429_170157.jpg
 
Mwaka 1977, Pradyumna Kumar Mahanandia, msanii wa India, aliendesha baiskeli kwa miezi minne na wiki tatu kutoka New Delhi hadi Gothenburg huko Sweden ili kwenda kukutana na mpenzi wake Charlotte Von Schedvin.

Alienda kwa baiskeli kwasababu hakuwa na pesa za kutosha kununua tiketi ya ndege. Baadae Walioana na sasa wana watoto wawili.
20210429_170421.jpg
 
Mwaka 2015, bwana mmoja kwa jina la Joel Vazquez Rojas ambaye alikuwa ni Meya wa mji wa San Pedro Huamelula, Mexico, alifanya sherehe kubwa ya ndoa kumuoa Mamba. Mamba huyo kike alikuwa na umri wa miaka mitatu aliyepewa jina la Maria Isabela.

Katika mji huu jambo hili halikua la kushangaza sana kwasababu huo ndio ulikua utamaduni wao kwa kiongozi kuoa kiumbe na kuishi nae.

Utamaduni huu unaaminika kuwa ndio unasaidia kupatikana kwa samaki wengi katika pwani ya bahari ya mji huo na ikiwa hakuna ndoa kama hiyo itakayofungwa baina ya kiongozi wa mji huo na kiumbe wa namna hio, basi shughuli hiyo tegemezi kwa uchumi wa watu wa mji huo itakua ngumu.

Utamaduni huu umekuwa ukitekelezwa tangu mwaka 1789 na imekua ikifanyika kila mwaka.
20210429_170512.jpg
 
Picha ni Chandler Crews, Kijana ambaye alizaliwa na aina flani ya umbilikimo (dwarfism) inayoitwa achondroplasia na alikuwa na urefu wa futi tatu na inchi sita tu.

Kutokana na kukua kwa teknolojia kijana huyu aliweza kukua na kuongezeka urefu wa miguu pamoja na mikono yake kwa inchi nne zaidi kwa msaada wa teknolojia inayotumika kwenye upasuaji wa kuongeza urefu wa viungo vya mwili.
20210429_170656.jpg
 
The Bunyadi ni mgahawa wa chakula uliokuwepo huko London Uingereza, ulianzishwa mwaka 2016. Baada ya miezi miwili tu ukafungwa kutokana na kuzidiwa na wateja, watu walikuwa ni wengi sana. Banyadi ni neno la kihindi lenye maana ya asili.

Kila mteja anaeingia kwenye mgahawa huu anatakiwa kuwa uchi wa mnyama kama alivyozaliwa. Ukiwa ndani ya mgahawa huu ni marufuku kuwa na simu na pia ni marufuku kupiga picha.

Mmiliki wa mgahawa huu Sebastian Lyall alisema kuwa siku chache baada ya kuufungua mgahawa huu zaidi ya watu 25,000 walikuwa wamesha weka oda ya kula hapo, na baada ya kufungwa kulikua na oda za watu 46,000 zimebaki kupata chakula hapo, taarifa zinasema kwamba walifunga ili kutanua zaidi mgahawa huo kwakua ulionekana kuzidiwa na idadi ya watu.

Mteja akishafika mgahawani hapo anaelekezwa na walinzi katika chumba maalumu ambako anaenda kuvua nguo zake alafu anarudi kuagiza chakula. Bei ya chakula ilikuwa inafika hadi Tsh 200,000=.
20210429_170758.jpg
 
Mwaka 2015, bendi ya Peking Duk waliripoti kuhusu shabiki wa bendi yao ya Peking Duk ya huko Australia, bwana David Spargo, aliefanikiwa kwenda nyuma ya jukwaa (backstage wanapokaa wasanii) kwenye moja ya matamasha yao kwa kutumia ujanja wa kujiorodhesha kama mwanafamilia kwenye ukurasa wao wa Wikipedia na kuwaonyesha walinzi wakamuamini.

Washiriki wa bendi hiyo walivutiwa sana na mbinu yake walimwita na kujumuika nae kwa kupiga stori na kunywa bia pamoja naye.
20210429_170913.jpg
 
Mwaka 1977, Pradyumna Kumar Mahanandia, msanii wa India, aliendesha baiskeli kwa miezi minne na wiki tatu kutoka New Delhi hadi Gothenburg huko Sweden ili kwenda kukutana na mpenzi wake Charlotte Von Schedvin.

Alienda kwa baiskeli kwasababu hakuwa na pesa za kutosha kununua tiketi ya ndege. Baadae Walioana na sasa wana watoto wawili.

babe wangu fanya na hii mvua basi ukuje umeona mapenzi hayo View attachment 1767728
Asiposoma hii post utanimbia nije mimi😁
 
The Bunyadi ni mgahawa wa chakula uliokuwepo huko London Uingereza, ulianzishwa mwaka 2016. Baada ya miezi miwili tu ukafungwa kutokana na kuzidiwa na wateja, watu walikuwa ni wengi sana. Banyadi ni neno la kihindi lenye maana ya asili.

Kila mteja anaeingia kwenye mgahawa huu anatakiwa kuwa uchi wa mnyama kama alivyozaliwa. Ukiwa ndani ya mgahawa huu ni marufuku kuwa na simu na pia ni marufuku kupiga picha.

Mmiliki wa mgahawa huu Sebastian Lyall alisema kuwa siku chache baada ya kuufungua mgahawa huu zaidi ya watu 25,000 walikuwa wamesha weka oda ya kula hapo, na baada ya kufungwa kulikua na oda za watu 46,000 zimebaki kupata chakula hapo, taarifa zinasema kwamba walifunga ili kutanua zaidi mgahawa huo kwakua ulionekana kuzidiwa na idadi ya watu.

Mteja akishafika mgahawani hapo anaelekezwa na walinzi katika chumba maalumu ambako anaenda kuvua nguo zake alafu anarudi kuagiza chakula. Bei ya chakula ilikuwa inafika hadi Tsh 200,000=.View attachment 1767740
Naomba unisindikize kwenye huo mgahawa...
 
Hii picha ilichorwa miaka mingi iliyopita na mchoraji kutokea
Urusi. Ni picha yenye taswira za watu wawili tofauti na pia ni wa jinsia tofauti (mwanamke na mwanaume).

Kwa haraka ukiangalia hii picha unaona taswira ya mwanaume, lakini pia kuna taswira ya mwanamke akitabasamu ila ili uione inakubidi uiangalie kama unataka kufumba macho.
20210429_192158.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom