Mwaka 1994 Mwalimu Nyerere akiwa kwao Butiama alifatwa na Mawaziri kadhaa ambao walienda kumsema kuwa anaishushia hadhi CCM kwasababu anawasiliana sana na watu wa vyama pinzani.
Nyerere aliwauliza kwanini wanamuita baba wa taifa? na Je yeye ni baba wa taifa wa wanaccm pekee? kisha akaingia ndani, akachukua kadi yake ya chama na kutaka kuirudisha ili asiwe mwanachama wa CCM.
Baada ya kuona hivyo Mawaziri wale wakamuomba sana asirudishe kadi hiyo
Wakati mbio zikiwa zinaendelea Frank alipata mshtuko mbaya wa moyo, lakini kwa namna fulani farasi aliendelea kwenda, na mwili wake uliweza kukaa juu ya farasi hadi alipovuka mstari wa kumaliza.
Baada ya kuvuka mstari wa kumaliza mbio akiwa wa kwanza ndipo aligundulika kuwa alishafariki dakika chache zilizopita.
Kama unaona unachelewa sana kusubiri hadi ufikishe miaka 18 ndo uruhusiwe kunywa pombe kisheria Tanzania, basi wewe usingeweza kuishi Aztec.
Karne ya 13 katika bara la Amerika ya kaskazini kulikua na Himaya/Ufalme ulioitwa Aztec (Aztec empire).
Katika Ufalme huo umri wa mtu aliyekua anaruhusiwa kunywa pombe ni kuanzia miaka 70 na kundelea tu. Miaka 69 kushuka chini walikua hawaruhusiwi kunywa pombe.
Mwaka 1996, Jim Kardach alipendekeza jina Bluetooth litumike kama jina la teknolojia iliyoundwa ili kusaidia uhusiano na ushirikiano wa kuunganisha na kubadilishana data kutoka katika vifaa viwili (Two devices).
Kardach alinukuliwa akisema, "Mfalme Harald Bluetooth ... alikuwa maarufu kwa kuunganisha Scandinavia kama vile tulivyokusudia kuunganisha vifaa bila kutumia waya."
Jina Bluetooth lilianzia zaidi ya miaka 1000 iliyopita (millennium) kwa Mfalme Harald "Bluetooth" Gormsson ambaye alikuwa anajulikana sana kwa vitu viwili:
Kitu cha kwanza ni Kuunganisha Denmark na Norway mnamo mwaka 958.
Pili ni jino lake lililokufa, ambalo lilikuwa na rangi ya bluu na likampatia jina la utani Bluetooth.
Sababu inayoelezwa ni kwamba nyuki wanachangia kwa kiasi kikubwa katika uchavushwaji wa mimea ambayo baada ya uchavushwaji hutoa chakula kwa binadamu, hivyo kama nyuki watatoweka basi mimea mingi haitoweza kuzaa na binadamu watakosa chakula ndio sababu ya kufa.
Katika karne ya 13 Papa Gregory IV alitangaza vita dhidi ya paka.
Alisema kuwa paka weusi ni vyombo vya Shetani. Kwasababu ya imani hii, aliamuru Ulaya kote paka kuawa.
Baada ya muda mpango huu ulisitishwa kwasababu kulitokea uhaba wa paka, uhaba ambao uliruhusu idadi ya panya kuongezeka na kusababisha kuenea kwa ugonjwa wa bubonic.
Hii ilitokea mwaka 1996 huko Hong Kong, Jambazi mmoja aliyeitwa #Cheung Tze Keung alimteka nyara mtoto wa tajiri mkubwa wa Asia #Li Ka-shing na kumtapeli tajiri huyo Dola za kimarekani milioni 130 kama fidia ya kumuachia mwanae, baadaye Jambazi huyo alimpigia simu tajiri #Li Ka-shing na kumuomba ushauri wa jinsi ya kuwekeza pesa hizo.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.