Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mwaka 1932-1933 lilitokea janga la njaa hatari sana lililoikumba Ukraine, Janga ilo liliitwa Holodomor.

Kukosekana kwa chakula kulipelekea watu kuanza kulana nyama wenyewe kwa wenyewe, watu walikufa kama kuku. Watu wengine walikua wakifanya uharifu makusudi na kujipeleka Jela wenyewe wakiamini wakiwa huko Serikali
itawahudumia chakula bure, hali iliyosababisha magereza yote kujaa.

Janga hili la kutisha lilidumu kwa msimu mmoja tu wa mwaka 1932-33 lakini lilisababisha vifo vya watu zaidi milioni 12 katika nchi ya Ukraine.

Sababu kuu za kutokea kwa janga hili la njaa ni ukame pamoja na mazao kushanbuliwa na wadudu (nzige) shambani.

Kila ifikapo mwisho ya mwezi November ya kila mwaka huwa ni siku ya kumbukumbu ya janga hili nchini Ukraine.
20210429_192527.jpg
 
Mshairi mashuhuri wa Marekani, Maya Angelou, aliahidi kumsaidia Dr Martin Luther King Jr. kukusanya pesa kwa ajili ya maandamano ya watu masikini. Sharti lake pekee ilikuwa kwamba angeenda kuifanya kazi hiyo baada ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa na marafiki zake.

Lakini ilipofika siku ya kuzaliwa kwake, Aprili 4, 1968, Luther King aliuawa. Baada ya hapo, alikataa kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa miaka. Na kwa zaidi ya miaka 30, yeye na aliyekua mke wa Luther King, Coretta Scott King walikua wanakutana, kupigiana simu au kupelekeana maua kila Aprili 4.
20210429_192901.jpg
 
Mwaka 1952, moshi mkubwa wa manjano ulitanda katika jiji la London kwa siku tano mfululizo na kuua zaidi ya watu 4000.

Moshi huo ulitanda sana kiasi kwamba watu barabarani hawakuweza hata kuona miguu yao wenyewe walipokua wakitembea.

Baadhi ya watu waliokufa hawakupata shida yoyote ya mapafu; walikufa kwa kuanguka na kuzama katika Mto Thames kwakua hawakuweza kuona mto walipokua wanatembea.
20210429_193133.jpg
 
Leo tunarudi Tanzania nimekutana na haya maajabu ya ziwa lenye rangi nyekundu kama damu.

Ziwa hili linaitwa ziwa Natron, lenye joto linalofikiwa kuwa digrii 60 za sentigredi na uwepo wa chumvi kali ya kufa mtu, linavutia sana na hata wakati mwingine unaweza kujisikia kutaka kuogelea ndani yake hasahasa kipindi ambacho unasikia joto, lakini mahali hapo si pa mzaha hata kidogo.

Rangi ya ziwa hili imekuwa kivutio si tu kwa binadamu ila hata kwa wanyama mbalimbali, ila cha kustaajabisha na kuogopesha ni kuwa wanapothubutu kutia mdomo au kuingia kwenye maji hayo hapo hapo wanageuka kwa kukauka na kuwa kama jiwe.

Lakini licha ya hivyo kuna baadhi ya viumbe ambao hawadhuliki katika ziwa hilo, ndege aina ya flamingo na pia kuna baadhi ya samaki hawadhuliki na kiasi kikubwa cha alkaline ipatikanayo katika hili ziwa ndio kwanza wanazaliana kwa wingi.

Watu wengi wanajiuliza ni kitu gani hupelekea viumbe vinavyothubutu kusogelea hili ziwa kukakamaa au kuwa kama majiwe. Watafiti wanaeleza kuwa hili ziwa linakiasi kikubwa cha alkaline na kaustic soda/ magadi ambacho huingia ndani ya mwili wa hicho kiumbe na kupelekea kufa na kukakamaa kabisa.
20210429_193447.jpg
 
Pichani ni Sara Baartman mzaliwa wa Afrika Kusini kutoka katika kabila la Khoikhoi. Alizaliwa mnamo mwaka 1789.

Sara alikuwa ni mwanamke mwenye maumbile makubwa na yenye kuvutia, hususani makalio yake kama jinsi inavyoonekana pichani.

Umbo lake liliwavutia sana Wazungu. Kutokana na umbo lake hilo mwaka 1810 Wazungu walimchukua na kumpeleka Uingereza ambapo alitumika kwa kufanyiwa maonyesho jukwaani na kuwaingizia pesa Wazungu hao.

Mwaka 1814 alihamishiwa Ufaransa ambako pia alikuwa akifanyiwa maonyesho akiwa uchi. Watu walikuwa wakimuita Hottentot Venus (mungu wa mapenzi wa khoikhoi). Sarah alifariki mwaka 1815 akiwa na miaka 26 na inasemekana alikufa kwa ugonjwa wa zinaa unaoitwa Kaswende (syphilis).

Mabaki ya mwili wake kama fuvu pamoja na sehemu zake nyeti ziliendelea kufanyiwa maonyesho katika makumbusho huko Paris, Ufaransa hadi miaka ya 1970's. Mwaka 2002 mabaki hayo yalizikwa.
20210429_193614.jpg
 
Huko Ohio, Marekani, mwaka 2016 Polisi waliripoti wametumiwa picha na muhalifu waliyekuwa wanamtafuta.

Jamaa anaitwa Donald Pugh (pichani), aliwatumia picha Polisi na kuwaomba wabadilishe picha waliyokuwa wameweka kwenye bango la tangazo la kutafutwa kwake kwasababu ilikua inaonekana vibaya, hivyo aliwatumia picha hiyo nzuri ili watu wasimuone kama ana sura mbaya.

Polisi walikubali ombi lake wakaweka picha aliyokua anataka na pia wakamshukuru kwa ushirikiano alioonesha na kumuomba kama ikiwezekana aende kituo cha Polisi wazungumze.
20210429_194127.jpg
 
Miaka ya nyuma kabla ya ugunduzi wa ufutio (eraser) watu walikua wanatumia mkate kama ufutio kufuta alama za penseli.

Mnamo mwaka 1770, Edward Naine kwa bahati mbaya alichukua kipande cha mpira badala ya mkate na kufutia, akaona mpira unafuta vizuri sana, hii ikamfanya aanze kuuza vifutio vya mpira.
20210429_194251.jpg
 
Baada ya Rais wa 35 wa Marekani John F. Kennedy kuuawa, mkewe Jacqueline Kennedy alikataa kuvua suti ya rangi ya waridi (pink) aliyovaa wakati mumewe anauawa. Ilikuwa imechafuliwa na damu ya John F. Kennedy aliposhambuliwa. Alivaa hata wakati Lyndon B. Johnson anaapishwa kuwa Rais wa 36 wa Marekani.

Jacqueline alisema, "Nataka waone kile walichomfanyia mume wangu."
20210429_194344.jpg
 
Mwaka 1829 Mexico ilifuta na kukataza biashara ya watumwa. Watumwa wakawa wanatoroka sehemu Mbalimbali na kukimbilia Mexico.

Watu waliokua wanamiliki watumwa huko Marekani waligundua kuwa watumwa wao walikuwa wanakimbilia Mexico. Marekani ikajaribu kuifanya Mexico isaini mkataba wa watumwa waliotoroka Marekani kwenda Mexico warudishwe Marekani, lakini Mexico ilikataa kutia saini mkataba huo, ikasisitiza kwamba watumwa wote watakua huru mara tu wanapotia miguu katika ardhi ya Mexico.
20210429_194444.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom