Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Innocent Bashungwa na Katibu Mkuu wake Dkt. Hassan Abbasi wamekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba kuhusu namna ambavyo Michezo ya Bahati Nasibu (Sport Betting National Lottery) inavyoweza kuchangia maendeleo ya michezo na uchumi wa Nchi kwa ujumla.
Hatua hii ni mkakati mahususi wa kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano Samia Suluhu Hassan la kutaka kuzalisha ajira kwa Vijana kupitia Michezo na Sanaa kwa kuwa ni miongoni mwa sekta zinazo toa ajira kwa Vijana wengi Tanzania.
Kikao hicho kimefanyika jana Aprili 27, 2021 katika Ukumbi wa Kambarage, Hazina jijini Dodoma.
View attachment 1766572View attachment 1766573