Makapuku Forum

Makapuku Forum

UNAAMBIWA Utafiti wa Mtandao wa Dove unaojihusisha na urembo Nchini Marekani unaeleza kuwa Wanawake wanaojikubali kuwa wao ni Warembo ni 4% pekee Duniani kote, wengine huwa hawajiamini hata wakisifiwa kuwa wao ni Warembo.

Utafiti huo unaendelea kusema kwamba ni 11% pekee ya Wanawake Duniani huwa wana uthubutu wa kujisifia hata mbele za Watu kuwa wao ni Warembo, wengine hata wakijikubali kuwa Warembo hukosa ujasiri wa kujisifia hadharani kuwa wao ni Wanawake wenye mvuto.

“80% ya Wanawake wanakubali kuwa kila Mwanamke ana kitu cha kipekee kinachomfanya avutie lakini mwenyewe hakioni, 72% ya Wanawake hujisika vizuri kuwa Warembo na 54% ya Wanawake Duniani wanakubali kuwa linapofika suala la urembo Wanawake wao kwa wao hukatishana tamaa na hata yule Mwanamke ambaye Wanaume watamuona Mrembo Wanawake wenzake husema ni wa kawaida tu”———Dove
20210427_174605.jpg
 
UNAAMBIWA Mwanaume mmoja nchini Japan akiwa na umri wa miaka 60 aliishtaki Mahakamani Hospitali moja ya Tokyo baada ya kubaini kuwa wakati anazaliwa Wauguzi walijichanganya na kumkabidhi kwa Mama ambaye hakumzaa March 1953 ambapo walimchanganya na Mtoto mwenzake aliyezaliwa dakika 13 baada ya yeye.

Mwanaume huyo alilalamika kuwa kujichanganya huko kumemfanya alelewe maisha ya kimasikini na single Mother wakati Mtoto mwenzake akilelewa Maisha ya kishua na Wazazi Matajiri———“Mwenzangu anamiliki Viwanda wakati waliompa ni Wazazi wangu, Mama yake ni huyu aliyenilea Mimi kimasikini”

Mahakama ya Wilaya Tokyo iliamuru Hospitali hiyo imlipe fidia ya Euro 227,000 (Tsh. Milioni 634) kwa makosa hayo ya waliyofanya huku wakimtaka Mwanaume huyo ikiwezekana akutane na Wazazi wake wa kweli ili wayamalize na kuishi pamoja.
20210427_174711.jpg
 
UNAAMBIWA Mwanaume mmoja nchini Japan akiwa na umri wa miaka 60 aliishtaki Mahakamani Hospitali moja ya Tokyo baada ya kubaini kuwa wakati anazaliwa Wauguzi walijichanganya na kumkabidhi kwa Mama ambaye hakumzaa March 1953 ambapo walimchanganya na Mtoto mwenzake aliyezaliwa dakika 13 baada ya yeye.

Mwanaume huyo alilalamika kuwa kujichanganya huko kumemfanya alelewe maisha ya kimasikini na single Mother wakati Mtoto mwenzake akilelewa Maisha ya kishua na Wazazi Matajiri———“Mwenzangu anamiliki Viwanda wakati waliompa ni Wazazi wangu, Mama yake ni huyu aliyenilea Mimi kimasikini”

Mahakama ya Wilaya Tokyo iliamuru Hospitali hiyo imlipe fidia ya Euro 227,000 (Tsh. Milioni 634) kwa makosa hayo ya waliyofanya huku wakimtaka Mwanaume huyo ikiwezekana akutane na Wazazi wake wa kweli ili wayamalize na kuishi pamoja.View attachment 1765713
kimbembe kitakuwa ni kumtoa uyo jamaa alokulia ushuani
 
UNAAMBIWA Andrea Ivanova (22) wa Bulgaria ndiye Mrembo ambaye anaipambania rekodi ya Dunia ya Mwanamke mwenye lips kubwa zaidi na mpaka sasa anaamini yeye ndie anaongoza kwa lips kubwa Dunia nzima, mapambano ya kuzisaka lips kubwa yamemfanya afanye upasuaji wa kuongeza lips mara zaidi ya 20 sasa na bado anasema ataendelea na upasuaji zaidi na zaidi hadi Dunia itakapomvisha Taji la Umalkia wa lips... ambapo katika kila upasuaji hutumia Euro 134 (zaidi ya Tsh. Laki 3).
20210427_174839.jpg
20210427_175011.jpg
 
UNAAMBIWA Kulala kidogo wakati wa mchana kwa saa kadhaa sio uvivu bali kunasaidia mambo mengi kiafya ikiwemo kupunguza uwezekano wa kupata maradhi ya moyo, Watu wanaolala kidogo mchana mara mbili angalau kwa wiki wana uwezekano mdogo wa kupata shambulio la moyo.
20210427_175148.jpg
 
Pamoja na ukubwa wa janga la virusi vya corona na jinsi lilivyoiteka dunia, Nchi mbalimbali zimeendelea kuweka pesa nyingi zaidi kwenye matumizi ya zana za kijeshi duniani kwa mwaka uliopita ambapo yameongezeka kwa karibu USD Trilioni 2.

Hayo yamo kwenye takwimu mpya zilizotolewa na Taasisi ya Kimataifa inayohusika na utafiti wa masuala ya amani, SIPRI ya Stockholm, Sweden ambapo imeeleza kumekuwepo na jumla ya matumizi ya kiasi cha USD Bilioni 1,981 hivyo kufanya ongezeko kuwa la 2.6% ikilinganishwa na mwaka 2019.

Mataifa ambayo yanaongoza katika matumzi makubwa ni Marekani, China, India, Urusi na Uingereza na kwa pamoja hayo yanafanya jumla ya asilimia 62 ya jumla ya matumizi ya silaha duniani lakini kwa namna ya kipekee kiwango hicho kwa China kimekuwa kikiongezeka pakubwa kwa mwaka wa 26 mfululizo.

Pamoja na ongezeko hilo la fedha katika sekta ya ulinzi kwa Mataifa mbalimbali yapo baadhi ya Mataifa kwa kiwango kikubwa yalibadilisha fedha za bajeti zake kwa mpango huo na kuzielekeza katika kukabiliana na janga la virusi vya corona mfano Chile, Korea Kusini, Brazil na Urusi.
20210427_175316.jpg
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewatoa hofu Wawekezaji wanaozalisha bidhaa mbalimbali na kusisitiza kuwa Serikali itahakikisha inawalinda na kulinda bidhaa zao ili waweze kupata masoko hapa nchini na hata nje ya nchi.

Ameyasema hayo alipotembelea kiwanda cha kuunganisha mabasi cha BM Motors kinachomilikiwa na Mtanzania Jonas Nyagawa na kiwanda cha madawa cha Kairuki, vilivyopo Kibaha mkoani Pwani ambapo amesema ameridhishwa na uwekezaji huo.

Waziri Mkuu amesema Serikali imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji kwa lengo la kuinufaisha Nchi pamoja na Muwekezaji, ametumia fursa hiyo kuwakaribisha Wawekezaji kuwekeza nchini katika sekta mbalimbali.

“Serikali tupo na nyie, maamuzi tuliyofanya ya kuweka mazingira wezeshi ni maamuzi sahihi, tutapita kusikia changamoto za kila mmoja wenu na tutazitatua, ongezeni mitaji kwenye uwekezaji wenu, tumieni Taasisi za Fedha kuongeza mitaji”———MAJALIWA
20210427_202023.jpg
20210427_202042.jpg
20210427_202131.jpg
20210427_202153.jpg
20210427_202218.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom