Makapuku Forum

Makapuku Forum

FT: Leeds United 0-0 Man United
EPL
20210425_192810.jpg
 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Innocent Bashungwa amefanya ziara katika mradi wa kujenga Kituo cha Michezo cha Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) uliopo Kigamboni Kibada, Dar es salaam.

Waziri Bashungwa amefanya ziara hiyo leo akiwa ameongozana na Rais wa TFF Wallece Karia ambapo amekagua mradi huo unaofadhiliwa na FIFA nchini unaotekelezwa Kigamboni na Jijini Tanga.

Waziri ameshuhudia ujenzi unavyoendelea na kuwahamasisha Viongozi kufanikisha zoezi kwa kasi kwa lengo la kumaliza kujenga Viwanja vinne mapema mwisho wa mwaka huu.

Waziri amewataka TFF kwa Awamu inayokuja chini ya miradi inayosimamiwa na FIFA wawekeze katika maeneo mengine nchini kwa kiwango kilekile Kama miradi ya Kigamboni na Tanga kwa kuzingatia hali ya kijiografia ya Nchi yetu ili kutonyima fursa ya kujiendeleza kimichezo kwa Wananchi waishio mbali na Dar es salam na Tanga.
20210425_210119.jpg
20210425_210144.jpg
 
Man City wanatwaa Ubingwa wa Carabao Cup kwa mara ya nne mfululizo baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Tottenham Hotspurs, goli likifungwa na Laporte dakika ya 82 ya mchezo.
20210425_210252.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom