Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,978
Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam wameendelea na oparesheni ya ukamataji Wahalifu vinara wanaojihusisha na wizi wa pikipiki, magari na vifaa vya magari pamoja na Wauzaji na Wanunuzi wa vifaa hivyo.
Katika oparesheni hiyo Watuhumiwa 49 wamekamatwa katika maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam wakiwa na pikipiki 10 aina mbalimbali na vifaa vyake, gari moja aina Toyota Noah likiwa limetolewa viti ambalo limekuwa likitumiwa na Wahalifu kubebea mali za wizi.
Watuhumiwa hao wamekamatwa pia na vifaa vya aina mbalimbali vya magari kama vile milango ya magari, side mirror, power windows, radio za magari, show za magari ya aina mbalimbali, taa za magari n.k.
“Majina ya Watuhumiwa kwa sasa yanahifadhiwa kwa sababu za kiupelelezi na oparesheni hii ya ukamataji inaendelea, Watuhumiwa wote wanaendelea kuhojiwa na watafikishwa Mahakamani baada ya kukamilisha taratibu zote za kisheria”———Mambosasa
“Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam inatoa wito kwa jamii kuendelea kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za uhalifu na Wahalifu ili kuendelea kuimarisha Usalama wa Jiji letu, tunatoa onyo kwa wote wanahojihusisha na wizi wa magari,pikipiki na vifaa vya magari kuacha mara moja kwani tumejipanga na tutawafikia popote watakapokimbilia au kujificha”———Mambosasa
Katika oparesheni hiyo Watuhumiwa 49 wamekamatwa katika maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam wakiwa na pikipiki 10 aina mbalimbali na vifaa vyake, gari moja aina Toyota Noah likiwa limetolewa viti ambalo limekuwa likitumiwa na Wahalifu kubebea mali za wizi.
Watuhumiwa hao wamekamatwa pia na vifaa vya aina mbalimbali vya magari kama vile milango ya magari, side mirror, power windows, radio za magari, show za magari ya aina mbalimbali, taa za magari n.k.
“Majina ya Watuhumiwa kwa sasa yanahifadhiwa kwa sababu za kiupelelezi na oparesheni hii ya ukamataji inaendelea, Watuhumiwa wote wanaendelea kuhojiwa na watafikishwa Mahakamani baada ya kukamilisha taratibu zote za kisheria”———Mambosasa
“Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam inatoa wito kwa jamii kuendelea kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za uhalifu na Wahalifu ili kuendelea kuimarisha Usalama wa Jiji letu, tunatoa onyo kwa wote wanahojihusisha na wizi wa magari,pikipiki na vifaa vya magari kuacha mara moja kwani tumejipanga na tutawafikia popote watakapokimbilia au kujificha”———Mambosasa


