Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,978
Mchezaji Ibrahima Ndiaye wa Timu ya Taifa ya Senegal ya U23 amejikuta akiachwa na Timu ya Al hilal ya Sudan kwa kuvunjiwa mkataba baada ya kubainika kuwa na tatizo katika ini, tumemtafuta Dr Sizya kutoka voh_updates kutaka kujua tatizo la Ndiaye linatibika au ndio mwisho wa ndoto yake ya Soka.
“Ini ni kiungo muhimu sana ndani ya miili yetu, hufanya kazi zaidi ya 500, moja ya kazi ni kuchuja na kuondoa sumu kutoka kwenye damu”———Dr.Sizya
“Kutokana na sababu mbalimbali kama pombe kupita kiasi, sumu kwenye damu au maambukizi, ini hupata shambulizi na kushindwa kufanya kazi vizuri, hali hii huitwa HOMA YA INI au HEPATITIS, kuna aina 5 ya virusi vya Homa ya ini vi 5 (A,B,C,D,E), aina mbili za virusi (B na C ) ndizo hatari zaidi, Virusi hivi vya homa ya ini B na C husambaa kupitia damu, shahawa au maji maji mengine ya mwili”———Dr.Sizya
“Virusi hivi vina uwezo wa kusambaa na kuambukiza Mtu mara 100 zaidi ya Virusi vya UKIMWI, hii huenda ikawa sababu number moja ya kuachwa na Al hilal kwa kuhofia kuambukiza wengine, zipo dawa ambazo mgonjwa hupewa ili kukabiliana na tatizo hilo, (HCV antiviral drugs) lakini pia lifestyle modifications kama kuacha pombe kunaitajika kama ini limeharibika sana basi upandikizwaji unaweza kuhitajika”———Dr.Sizya
“Ini ni kiungo muhimu sana ndani ya miili yetu, hufanya kazi zaidi ya 500, moja ya kazi ni kuchuja na kuondoa sumu kutoka kwenye damu”———Dr.Sizya
“Kutokana na sababu mbalimbali kama pombe kupita kiasi, sumu kwenye damu au maambukizi, ini hupata shambulizi na kushindwa kufanya kazi vizuri, hali hii huitwa HOMA YA INI au HEPATITIS, kuna aina 5 ya virusi vya Homa ya ini vi 5 (A,B,C,D,E), aina mbili za virusi (B na C ) ndizo hatari zaidi, Virusi hivi vya homa ya ini B na C husambaa kupitia damu, shahawa au maji maji mengine ya mwili”———Dr.Sizya
“Virusi hivi vina uwezo wa kusambaa na kuambukiza Mtu mara 100 zaidi ya Virusi vya UKIMWI, hii huenda ikawa sababu number moja ya kuachwa na Al hilal kwa kuhofia kuambukiza wengine, zipo dawa ambazo mgonjwa hupewa ili kukabiliana na tatizo hilo, (HCV antiviral drugs) lakini pia lifestyle modifications kama kuacha pombe kunaitajika kama ini limeharibika sana basi upandikizwaji unaweza kuhitajika”———Dr.Sizya
mtoto mlito