Makapuku Forum

Makapuku Forum

Aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi Dr. Bashiru Ally akila kiapo cha uaminifu Bungeni leo baada ya kuteuliwa kuwa Mbunge na Rais Samia Suluhu jana.
20210401_130910.jpg
 
Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kupitia TFF limeruhusu mchezo wa Simba SC dhidi ya AS Vita wa Ligi ya Mabingwa Afrika April 3 2021 kuingizwa Mashabiki 10,000.

Awali CAF walizuia Simba SC kucheza na Mashabiki katika mchezo wao wa mwisho wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya El Merreikh ya Sudan uliyochezwa Uwanja wa Mkapa kwa sababu ya kujikinga na Corona.

Kwenye mchezo huo uliochezwa March 16 2021 uwanja wa Mkapa na Simba kupata ushindi wa magoli 3-0, Simba waliruhusiwa kuingiza Watu 200.
20210401_170229.jpg
 
Jeshi la Polisi nchini limesema halitegemei kuona sherehe na shamrashamra za Sikukuu ya Pasaka zilizozoeleka kipindi cha miaka ya nyuma katika kipindi hiki ambacho Nchi bado ipo kwenye maombolezo ya kuondokewa na Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.
20210401_171144.jpg
 
“Jana tulikuja hapa kushuhudia kiapo cha Makamu wa Rais Mpango ila tukakutana na mengine (Mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri), Mama (Rais Samia Suluhu) hatabiriki, hata leo hatujui kama tutatoka salama hapa, kwahiyo kwakuwa hatabiriki mlioteuliwa chapeni kazi”——Spika Ndugai mbele ya Rais Samia Suluhu leo Ikulu Chamwino Dodoma baada ya kiapo cha Viongozi wapya.



20210401_171246.jpg
 
“Nikushukuru Rais Mh. Samia Suluhu, maana jana mabadilko yale ya ghafla nikajikuta na Mimi niko salama, nikuahidi nitaendelea kufanya kazi kwa uadilifu, weledi ili Serikali yetu iweze kupata mafanikio”———Waziri Mkuu Majaliwa mbele ya Rais Samia.
20210401_180843.jpg
 
“Waziri wa Fedha (Mwigulu Nchemba) umepewa kigezo hapa cha Trilioni mbili kwa Mwezi, tunataka Trilioni mbili kwa Mwezi muende mkatanue wigo wa kodi lakini pia mkatengeneze walipa kodi wengi zaidi”———Rais Samia Suluhu baada ya kuwaapisha Viongozi Ikulu Chamwino Dodoma leo jioni

“Trend mnayokwenda nayo sasa mnaua Walipakodi, mnaua Wafanyabiashara, mnatumia nguvu zaidi kuliko akili na Maarifa kupata kodi, sasa wale mnaowakamua mkienda mkachukua vifaa vya kazi, mkafungia akaunti zao na kuchukua pesa kwenye akaunti, akitoka anafunga biashara anahamia Nchi ya Pili”———Rais Samia Suluhu

“Mnaua Wafanyabiashara (kwa kutumia nguvu kukusanya kodi) mnapunguza walipa kodi, nendeni mkatengeneze na kutanua wigo wa walipa kodi, yale mengine yanayowapunguzia Watu ari ya kulipa kodi Waziri (Mwigulu Nchemba) naomba ukayasimamie” -——-Rais Samia Suluhu
20210401_183912.jpg
 
“Nafahamu 2025 ipo karibu na kawaida yetu inapoingia kipindi cha pili cha Rais aliyopo Watu kidogo mnakuwa na lile na hili kuelekea mbele, nataka kuwaambia acheni, twendeni tufanye kazi hili na lile tutajua mbele”———Rais Samia Suluhu baada ya kuwaapisha Viongozi wapya Ikulu Chamwino Dodoma leo jioni

“Nataka kuwaambia rekodi yako inakufuata katika maisha yako, wengine wamekosa hizi nafasi kwa rekodi zao tu, na Mimi nitakuwa na jicho kubwa sana pamoja na kwamba yamelegea lakini yanaona, nitakuwa na jicho kubwa kuangalia rekodi zenu”———Rais Samia Suluhu

“Nitakuwa na jicho kubwa sana kuangalia rekodi zenu na safari ya mbele yetu lakini nataka kuwaambia kila yule mwenye nia ya 2025 aache mara moja”———Rais Samia Suluhu
20210401_184453.jpg
 
“Serikali ni moja pasitokee kuvutana, nendeni mkawatumikie Wananchi, mkafanye kazi baada ya Bunge la Katiba,kwa sasa mko kwenye Bunge la Katiba aah! hivi nina maradhi gani na Katiba!?, nadhani kwakuwa wameni-push push sana Katiba, Katiba lakini kwa sasa wasahau kidogo”———Rais Samia Suluhu baada ya kuwaapisha Viongozi leo jioni Ikulu Chamwino Dodoma

“Kwa sasa mpo kwenye Bunge la Bajeti, Bajeti tunayoitafuta ni ya Serikali kwahiyo Mawaziri wote lazima muwepo Bungeni, mmoja amekwama na hoja anayeijua anasaidia sio ‘hilo si lake atajijua mwenyewe’, bila Bajeti ya Serikali hatutokuwa na fedha za kuendesha Nchi”———Rais Samia Suluhu
20210401_184729.jpg
 
“Nawatakia Pasaka njema, tunamaliza Pasaka Jumatatu, pengine Jumanne tutakuja kuapishana hapa na wengine (Wateule wapya), niwatakie kila la kheri na Pasaka njema”———Rais Samia Suluhu Hassan
20210401_191513.jpg
 
“Waziri wa Fedha (Mwigulu Nchemba) umepewa kigezo hapa cha Trilioni mbili kwa Mwezi, tunataka Trilioni mbili kwa Mwezi muende mkatanue wigo wa kodi lakini pia mkatengeneze walipa kodi wengi zaidi”———Rais Samia Suluhu baada ya kuwaapisha Viongozi Ikulu Chamwino Dodoma leo jioni

“Trend mnayokwenda nayo sasa mnaua Walipakodi, mnaua Wafanyabiashara, mnatumia nguvu zaidi kuliko akili na Maarifa kupata kodi, sasa wale mnaowakamua mkienda mkachukua vifaa vya kazi, mkafungia akaunti zao na kuchukua pesa kwenye akaunti, akitoka anafunga biashara anahamia Nchi ya Pili”———Rais Samia Suluhu

“Mnaua Wafanyabiashara (kwa kutumia nguvu kukusanya kodi) mnapunguza walipa kodi, nendeni mkatengeneze na kutanua wigo wa walipa kodi, yale mengine yanayowapunguzia Watu ari ya kulipa kodi Waziri (Mwigulu Nchemba) naomba ukayasimamie” -——-Rais Samia SuluhuView attachment 1740564

Hii ya kufungiana account na kukombewa pesa zote ilikua mbaya sana...

Wana freeze account kwa maslahi binafsi...
Unashuritishwa kukiri kosa ambalo hata hulijui ni kosa gani na kushurutishwa kulipa faini ambayo hujui ni ya nini...

Ukihoji unaambiwa ni maagizo kutoka juu...
 
Hii ya kufungiana account na kukombewa pesa zote ilikua mbaya sana...

Wana freeze account kwa maslahi binafsi...
Unashuritishwa kukiri kosa ambalo hata hulijui ni kosa gani na kushurutishwa kulipa faini ambayo hujui ni ya nini...

Ukihoji unaambiwa ni maagizo kutoka juu...
Hapa kanikoshaaaa mama ...waleee jamaa wa tiaraaaeiiiii washenzii sanaaaa ...mtu ulifanya return za 18 wanakulazimisha eti hukufanya
 
“Waziri wa Fedha (Mwigulu Nchemba) umepewa kigezo hapa cha Trilioni mbili kwa Mwezi, tunataka Trilioni mbili kwa Mwezi muende mkatanue wigo wa kodi lakini pia mkatengeneze walipa kodi wengi zaidi”———Rais Samia Suluhu baada ya kuwaapisha Viongozi Ikulu Chamwino Dodoma leo jioni

“Trend mnayokwenda nayo sasa mnaua Walipakodi, mnaua Wafanyabiashara, mnatumia nguvu zaidi kuliko akili na Maarifa kupata kodi, sasa wale mnaowakamua mkienda mkachukua vifaa vya kazi, mkafungia akaunti zao na kuchukua pesa kwenye akaunti, akitoka anafunga biashara anahamia Nchi ya Pili”———Rais Samia Suluhu

“Mnaua Wafanyabiashara (kwa kutumia nguvu kukusanya kodi) mnapunguza walipa kodi, nendeni mkatengeneze na kutanua wigo wa walipa kodi, yale mengine yanayowapunguzia Watu ari ya kulipa kodi Waziri (Mwigulu Nchemba) naomba ukayasimamie” -——-Rais Samia SuluhuView attachment 1740564
10 tena kwa mama samia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom