Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya mvua kubwa katika baadhi ya maeneo ya Mikoa ya Dar es salaam, Lindi, Kusini mwa Mkoa wa Morogoro na Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia) kwa muda wa siku tatu kuanzia leo Jumamosi hadi Jumatatu April 05,2021, athari zinazoweza kutokea ni makazi kuzungukwa na maji na ucheleweshwaji wa baadhi ya shughuli za usafirishaji———“tafadhali zingatia na ujiandae”
Club ya Polisi Tanzania imewasimamisha Wachezaji wake sita kwa makosa ya utovu wa nidhamu, Wachezaji waliosimamisha ni Rashid Juma, Abdullaziz Makame, Pius Buswita, Tariq Seif, George Mpole na Abdulamalick Adam.
Timu ya Madaktari wanane nchini Urusi wamepongezwa kwa ujasiri wao kufuatia kupambania maisha ya Mgonjwa aliyekuwa anafanyiwa upasuaji wa moyo licha ya jengo la Hospitali kuwaka moto.
Unaambiwa wakati Hospitali ikiendelea kuwaka moto kwa nje na hata kwa ndani kwenye baadhi ya vyumba huku Watu wengine wakikimbia ili kujiokoa, Madaktari hao waliendelea na kazi na wakafanikiwa kukamilisha upasuaji salama.
Kikosi cha Zimamoto kilifika na kuendelea na zoezi la kuuzima moto lakini Madaktari waliendelea na upasuaji licha ya kupewa ishara kuwa nje kuna ajali ya moto, walichofanya Watu wa Zimamoto ni kukipa kipaumbele chumba cha upasuaji kwa kuzuia moshi kuingia na kupambana ili moto usikifikie chumba hicho.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.