Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Elisante Ole Gabriel amewataka Watafiti kufanya utafiti kama kuna uwezekano wa kutumia ngozi ya kuku kuzalisha bidhaa mbalimbali za ngozi kama inavyofanyika kwa ngozi za ng’ombe, mbuzi n.k
Prof. Ole Gabriel ameyasema hayo wakati wa kuzindua mafunzo ya mnyororo wa thamani kwa Wadau wa ngozi Dar es Salaam.
“Kuku tunao Milioni 83.3 na wanataga mayai Bilioni 4 yenye thamani ya Tsh Bilioni 800, nguruwe tunao Milioni 2, ngozi, nyama na maziwa tukizitumia vizuri uchumi utakua, tusitupe kitu kwenye wanyama hata kwato, pembe, meno ya ng’ombe, mbuzi, kondoo hata punda yachangie uchumi”——->
View attachment 1727291