Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila, amesema Serikali haina mpango wa kuziondoa au kuzuia Bajaji kusafirisha Abiria kupitia Barabara kuu na kusisitiza kuwa Bajaji na Daladala zote zina haki ya kubeba Abiria kwasababu Wamiliki wake wanalipa kodi za Serikali.

Chalamila ametoa kauli hiyo leo March 15,2020, Ofisini kwake wakati akitoa msimamimo wa Serikali baada ya Madereva Daladala kugoma Jijini Mbeya wakishinikiza Bajaji kuondolewa Barabara Kuu ambazo wanadai zimeidhinishwa kwa ajili ya Daladala pekee.

“Mkiendelea kugoma sitosita kutumia Mamlaka yangu, ninazo Taasisi nyingi, JWTZ, Magereza, Mahakama, na wana Mabasi ambayo yanaweza kubeba Abiria” -Chalamila
20210316_192439.jpg
 
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Godwin Gondwe, ametoa maelekezo kwa Uongozi wa Shule ya Msingi Toangoma, pamoja na Uongozi wa Kata, kuchukua hatua za haraka kukomesha vitendo vya uvunjifu wa maadili vinavyodaiwa kukithiri katika Shule hiyo.

Gondwe ametoa maelekezo hayo alipotembelea Shuleni hapo kwa lengo la kupata ukweli wa kile kilichoripotiwa na Vyombo vya Habari kuhusu kukithiri kwa vitendo vya ngono ambapo ametoa siku saba kwa Uongozi wa Shule na wa Kata kuweka mikakati ya pamoja kwa kushirikiana na Uongozi wa Mtaa ili kwa pamoja wakubaliane ni kwa namna gani vitendo hivyo vitakoma.

Gondwe ameagiza kufukuzwa Shule kwa Wanafunzi watatu ambao wamethibitika kuwa vinara wa vitendo hivyo viovu pia ameagiza kupigwa kwa kura ya siri kwa kila darasa ili kuwabaini wanafunzi wote wanaojihusisha na vitendo hivyo na baada ya kuwabaini wafanyiwe uchunguzi wa kitabibu kuthibitisha tuhuma hizo.

Amesema baada ya kuthibitisha Wazazi wao waambiwe kwa uwazi na hatua stahiki za kitabibu zichukuliwe kwa wale walioathiriwa kiafya na kisaikolojia, na kwa wale vinara hatua kali za kisheria zichukuliwe ikiwemo kuondolewa Shuleni.
View attachment 1727296
Inasikitisha sana...
Wakiguswa na raia miaka 30...

Kumbe wenyewe kwa wenyewe walishaanza kulana kitambo...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom