Makapuku Forum

Makapuku Forum

Maisha ni mtazamo wa mtu, vile unavyoyaona ndani ya nafsi yako ndivyo yalivyo. Ukiyaona magumu yatakuwa magumu kweli kweli, ukiyaona ya kawaida yatakuwa kawaida, ukiyaona ni fursa yatakusukuma kufanya mambo makubwa zaidi yatayokusogeza mbele kimaendeleo. Uskariri Njia ya kupita, njia zipo nyingi sana tena nzuri sana ukizielewa endapo utazitazama kwa jicho la tatu. Usijiwekee mipaka kwenye maarifa ya utaftaji.
 
Kijana sasa ni muda wa kutumia muda wako vizuri kufikiri mambo mengine zaidi, kufikiri namna ya kukamilisha project yako, kufikiri namna ya kuongeza mauzo kwenye biashara yako. Mapenzi yasikupotezee muda wa kuandaa Maisha ya baadae. Vijana huwa tunajisahau Sana kipengele cha mahusiano yasiyo na kichwa wala miguu. Kijana Umiza kichwa sababu ya biashara Sio mapenzi yasiyo rasmi.
 
Penda unachokifanya itakusaidia sana Kupata mrejesho unaokutia moyo, kuendelea kufanya makubwa zaidi. Usipotafuta pesa ya mtaji wa kuanzia biashara Leo, jiandae kutafuta pesa kwa ajiri ya kulipa madeni kesho sababu hautokuwa na chanzo cha maana cha kukuingizia kipato zaidi ya kukopa. Nguvu utayoitumia kutafuta pesa ya kulipa madeni always inakuwa kubwa zaidi ya hile nguvu unayoitumia kutafuta mtaji wa biashara. Chagua moja Kati ya hivyo vitu viwili Leo Kati ya kupambania mtaji au kupambania madeni, hauwezi kukwepa hayo,,,,,, think💪
 
UKIENDEKEZA MBELE VISINGIZIO VYA CHANGAMOTO, ZITAKUPOTEZA KAAAABISA. Punguza kulia lia ovyo, anza project yako hata Kama ndogo lakini ni yako hiyo, hakusumbui mtu. Jichanganye na watu upate channel za Biashara za maana, kwa mtaji mdogo usikaze kichwa.💪💪
 
Asanteee numbiii
Yawezekana wewe ni Tai sio kuku, lakini mazingira uliyoyakuta, jamii unayo interact nayo mara kwa mara inakutengeneza uendelee kujiona kuku. But kiuhalisia wewe ni Tai. Chagua moja paa angani uingie msituni waliko Tai wenzio ukatafute nzige idadi utakayo ili ushibe au baki zizi la kuku uletewe pumba kwa kipimo hata kama kidogo.
 
Kama unataka kuonekana Kama wewe ni kichwa sana, mchapa kazi Sana Fanya biashara peke yako. Lakini Kama unataka kufika mbali kibiashara unahitaji kushirikiana na watu wengine. Biashara inayokutegemea wewe uwepo wako kwa 100% mara nyingi inaishia njiani, na haina future biashara ya mtu huyo sababu ya competition , mtaji mdogo na pia sio siku zote wewe utakuwa vizuri kiafya au Changamoto zingine za kimaisha au majukum utashindwa kusimama kwenye biashara na inachukuwa muda mrefu mno kuona mwanga. Kuna mazingira mtu binafsi hawezi kupenya, lazima awe na system ya watu anaoshirikiana nao.Mchunguze mtu yeyote aliyefika mbali kibiashara iwe ya huduma au bidhaa au music nk. utagundua kuwa alianza peke yake kisha akatengeneza team ya kushirikiana nayo. kuwa na team katika biashara yako inakuhitaji uwe na mtaji mkubwa sana, kitu ambacho kwa Kijana wa kawaida inakuwa ngumu kuwa na team ya biashara, mwisho wa siku mtu anaishia kufanya biashara ya Kupata hela ya kula tu. Lakini kutokana na kukua kwa sector hii ya biashara Kuna mfumo wa biashara unaokuruhusu wewe kutengeneza team yako ya biashara kwa mtaji wa kawaida ambao kwa mtu mwenye maisha ya kawanda anaweza kuupata, kwa sababu ataingia mkataba wa kufanya Biashara na kampuni yenye brand kubwa kibiashara. But exposure hiyo wengi hawafaham kiundani, wanaiskia juu juu tu, nakushauri ifuatilie ili ufaham Vzur. PARTNERSHIP.
 
Usipoamua kuanza project yako, hata Kidogo Kidogo itakuwa ngumu sana kutimiza malengo ya muda mrefu, miezi itaisha, Miaka itaisha, the same person. Think about business idea, mtaani watu wanahitaji solutions Zako ili ziwasaidie kutatua Changamoto zao. Fikiria namna ya kutatua Changamoto Kwanza pesa zitafuata mkondo wake
 
The way you think, the way you grow.Either positive or negative growth.Be an asset, but not a liability. Investors can invest in you if you Go extra miles, beyond ordinary parameters. In spite of your educational certificates, do you have anything extra to offer?? Naturally, Investors need extra things. Upgrade your status,,,
 
Mambo hayatokei hivi hivi hadi uyasababishe, usiyasubiri bali yasababishe kwa nidhamu ya aina yake ili yatokee. Ili uanze Mwaka mpya na biashara yako ikiwa stable, huu ni wakati muafaka wa kuanza biashara yako.
 
Mafanikio ni pale ambapo kuna balance Kati ya Sala, kazi, Muda, Uhuru wa kipato na hivyo vyote vikupatie Furaha. Ukikosa kimoja wapo bado kuna uhitaji wa kujitathmini, usijisahau sana.💪
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom