Makapuku Forum

Makapuku Forum

Chombo kilichotumwa na NASA kwenda kulichunguza jiwe kubwa linaloelekea huku Duniani, kimefanikiwa kukuta maji kwenye jiwe hilo.

Chombo hicho kinachoitwa OSIRIS-REx kimeanza kurudisha majibu ya utafiti kutoka kwenye jiwe hilo lenye ukubwa wa mita 500 ambalo lipo umbali wa maili 100 kutoka kwenye Jua letu.

Uwepo wa maji kwenye jiwe hilo ni furaha kubwa kwa wanasayansi wa NASA, kwa sababu sehemu yoyote ambapo kuna maji basi kuna uwezekano mkubwa wa viumbe hai kuweza kuishi na huu ni mwanzo mzuri katika kufahamu jinsi mfumo wetu wa Jua ulivyoumbwa.View attachment 965445
Hii nimeipenda
 
Mwaka 1971 wakati mwanafalaki Jerry Ehman alipokuwa anachunguza mkusanyiko wa nyota unaoitwa Chi Sagittarii uliokuwa umbali wa miaka 200 ya mwanga kupitia darubini ya mawimbi ya radio, Ehman alipokea mawimbi ya radio yaliyodumu kwa sekunde 72 katika mlolongo wa namba 6EQUJ5 ambapo alizizungushia duara, baadae alipoenda kuyatafsiri mawimbi yale ya radio yalisomeka 'Wow'. Mpaka leo hakuna mwanasayansi aliyeweza kuelezea kama mawimbi hayo ya radio yalitokana na vitu vilivyokuwa huko angani au ni viumbe wengine wanajaribu kuwasiliana nasi. View attachment 965447
Asee
 
DuFFrfSXQAgDgJ_.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom