Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kilichopo hapo

Hii ni nyumba miongoni mwa nyumba za vijiji vya jirani na hifadhi ya Udzungwa mkoani Morogoro
FB_IMG_1544410597671.jpg
Kinachoonekana juu ya kipaa ni moshi wa kuni, nyakati za mvua hali huwa hivyo
 
Chombo kilichotumwa na NASA kwenda kulichunguza jiwe kubwa linaloelekea huku Duniani, kimefanikiwa kukuta maji kwenye jiwe hilo.

Chombo hicho kinachoitwa OSIRIS-REx kimeanza kurudisha majibu ya utafiti kutoka kwenye jiwe hilo lenye ukubwa wa mita 500 ambalo lipo umbali wa maili 100 kutoka kwenye Jua letu.

Uwepo wa maji kwenye jiwe hilo ni furaha kubwa kwa wanasayansi wa NASA, kwa sababu sehemu yoyote ambapo kuna maji basi kuna uwezekano mkubwa wa viumbe hai kuweza kuishi na huu ni mwanzo mzuri katika kufahamu jinsi mfumo wetu wa Jua ulivyoumbwa.
Screenshot_20181212-081955.jpeg
 
Mwaka 1971 wakati mwanafalaki Jerry Ehman alipokuwa anachunguza mkusanyiko wa nyota unaoitwa Chi Sagittarii uliokuwa umbali wa miaka 200 ya mwanga kupitia darubini ya mawimbi ya radio, Ehman alipokea mawimbi ya radio yaliyodumu kwa sekunde 72 katika mlolongo wa namba 6EQUJ5 ambapo alizizungushia duara, baadae alipoenda kuyatafsiri mawimbi yale ya radio yalisomeka 'Wow'. Mpaka leo hakuna mwanasayansi aliyeweza kuelezea kama mawimbi hayo ya radio yalitokana na vitu vilivyokuwa huko angani au ni viumbe wengine wanajaribu kuwasiliana nasi.
Screenshot_20181212-082122.jpeg
 
Baada ya kusafiri kwa muda mrefu hatimaye OSIRIS-REx chombo kilichotumwa na NASA kwenda kuchukua sampuli za mchanga kwenye jiwe kubwa linaloitwa Bennu ambalo linatarajiwa kuja kugongana na Dunia yetu kimeshasogea na kuanza kurudisha picha zinazoonesha muonekano wa karibu wa jiwe hilo.

Bennu au jina halisi 101955 Bennu ni jiwe lenye ukubwa wa mita 500 (sawa na maghorofa matatu ya PSPF Commercial Tower yapangwe kwenda juu) ni moja kati ya mawe yaliyosalia wakati mfumo wetu wa Jua unaundwa hivyo limebeba historia kubwa dhidi ya uundwaji wa mfumo wetu wa Jua pamoja na Dunia yetu.

OSIRIS-REx kinatarajiwa kutua kwenye jiwe hilo na kuchukua sampuli za mchanga kisha kufanya utafiti kwenye jiwe hilo kwa miaka miwili na kurudisha sampuli hizo ifikapo mwaka 2023. Wanajimu wametabili jiwe hilo kubwa Bennu litakuja kugongana na Dunia yetu kati ya mwaka 2054, 2080, au 2135.
Screenshot_20181212-082232.jpeg
 
Katika mpango wake wa kutaka kuibadilisha sayari ya Mars kuwa kama Dunia ili watu waweze kuishi, Bilionea Elon Musk anataka kutumia silaa za nuklia (thermonuclear) kuyeyusha barafu lililokuwa kwenye ncha ya kaskazini mwa sayari hiyo japokuwa mpango huo umekuwa ukipingwa na baadhi ya wanasayansi wakisema hata kama akiweza kufanya hivyo kiasi cha atmospheric pressure kitaongezeka kwa asilimia 1.2 ya ile ya Duniani, labda kama akisema achimbe chini kabisa kwenye ganda la sayari hiyo ili kutoa Carbon itatusogeza kwa asilimia 5 na kwa sasa hakuna teknolojia inayoweza kutumika kuchimba zaidi ya mita 100 kwenye sayari hiyo.
Screenshot_20181212-082341.jpeg
 
Pindi Jua linapozama (machweo) kwenye Sayari ya Mars anga hubadilika rangi kutoka nyekundu kwenda bluu tofauti na huku Duniani ambapo anga hubadilika rangi kutoka bluu kwenda nyekundu. Hii picha ilipigwa kwenye sayari ya Mars na chombo kinachoitwa Curiosity Mars Rover ndani ya kasoko linaloitwa Gale wakati Jua lilipokuwa linazama (machweo). Mars ni sayari pekee ambayo inasemekana mwanzo ilikuwa inafanana dhahiri na Dunia yetu kabla ya kukumbwa na majanga yaliyopelekea eneo kubwa la sayari hiyo kuwa na jangwa pamoja na dhoruba kali za vumbi muda wote.
Screenshot_20181212-082433.jpeg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom