Makapuku Forum

Makapuku Forum

Picha hizi nne zimechaguliwa kuwania tuzo ya Picha inayochekesha sana yaani Wildlife comedy Photography ya mwaka.
Ipi inakuvutia zaidi?

Picha itakayoshinda itachapishwa kwenye jarida la Bornfree na kuuzwa ilikuchangisha pesa za uhifadhi wa wanyama na mbuga za Wanyama kote duniani.
Screenshot_20181123-101818.jpeg
Screenshot_20181123-101804.jpeg
Screenshot_20181123-101747.jpeg
Screenshot_20181123-101732.jpeg
 
Jamani wanaume mtanisamehe kwa hili.
Swali hili linawalenga dada, wapenzi,wake, na kina mama wetu Je nini kinaweza kukufanya umchinje mtu unayekiri kumpenda kwa dhati , umkatekate vipande, uchanganye maiti yake na kitunguu kwenye sufuria yako na tui la nazi umpike na ule kitoweo chake kwa wali ? Taarifa kuwa
mwanamke mmoja raia wa Morocco aliua mpenzi wake na kumpika imeshtua ulimwengu wote.
Screenshot_20181123-101956.jpeg
 
Tumosa na ningendako nawatakia maandalizi mazuri ya wikend. Ndugu yenu mimi sijambo na ninafuatlia kwa umakini kozi ya kiingilishi mliyonilipia, ila ticheri kasema twisheni itanisaidia zaidi, gharama ni elfu 41 mia tano tu, mnipe mapema leo maana wikend imekaribia
Hahahah binamu pesa yote hyo kwa ajiri ya twisheni au tuishieni?
 
Serikali ya Jamaica imependekeza muziki wa REGGAE Ujumuishwe katika orodha ya mwaka huu ya “tamaduni zinazostahili kulindwa zisiangamie” la shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia maswala ya turathi elimu na tamaduni UNESCO. Iwapo mziki huu maarufu kote duniani itaorodheshwa basi itaipa ulinzi wa kisheria chini ya mikataba ya kimataifa, UNESCO.
Screenshot_20181123-102151.jpeg
 
Kwahiyo binamu umewaona tumosa na kaka akee baba wawili tu sisi wengine sio watu humu eenh

...wengine ni watu, ila hawa wamenilia inglishikozi ili niwe namwambia marybaby maneno matamu matamu ya kiinglishi maana maneno ya kiswahili yanaukakasi sana kimalavidavi.

Ile namba ya Wena Sepenga niliitaka maana nasikia anangekewa kwa mtu aliyepata hela nyingi za mkupuo (tafadhari babay Mary asisikie hizi habari, wewe ni ndugu yangu wa ukweli)
 
Mwanamitindo kutoka Marekani,Blac Chyna ametuhumiwa na maelfu ya waNigeria kwenye mitandao ya kijamii kwa kuchochea matumizi ya madawa yanayochubua rangi ya ngozi ya wanawake weusi nchini Nigeri
.
Chyna alitangaza kupitia kwenye mtandao wa Instagram kuwa atakuwa Lagos Nigeria Jumapili hii kuzindua bidhaa za urembo za Whitenicious.

Screenshot_20181123-102327.jpeg
 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amemteua bi Joyce Msuya kutoka Tanzania kuwa kaimu kiongozi wa shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira, UNEP.

Bi Msuya amekuwa naibu katibu mkuu na naibu mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo ambalo lina makao makuu yake jijini Nairobi, Kenya.
Screenshot_20181123-102458.jpeg
 
”Hivi, binadamu, mnafanya nini ?”Posa ya raia wawili raia wa Uingereza imesambazwa mitandaoni baada ya Wanyama ”Otters” kushangilia Jordan Doyle alipopiga goti na kumuliza mpenzi wake Mary Lister kama angekubali kuolewa nayWanyama hao nao walionekana kuinama na kuwashangilia wapenzi hao.
Screenshot_20181123-102609.jpeg
 
Rais Donald Trump wa Marekani amemtetea binti yake Ivanka baada ya uchunguzi kubaini kuwa alitumia anuani ya kibinafsi ya barua pepe katika shughuli rasmi za Ikulu ya White House.

Uchunguzi wa mfumo wa usalama wa ikulu uligundua kuwa mshauri huyo wa rais Trump alituma ujumbe mara 100 kinyume na mpangilio wa usalama wa ikulu.

Mwaka wa 2016, rais Trump alipokuwa akiwania urais, alimponda sana mpinzani wake mkuu bi Hillary Clinton kwa kuhatarisha usalama wa taifa kwa kutumia anuani ya kibinafsi kutekeleza majukumu ya kiserikali akidai ilikuwa rahisi kudukuliwa.
Je Trump atamuadhibu binti yake Ivanka ?
Screenshot_20181123-102745.jpeg
 
Thamani ya sarafu ya Tanzania dhidi ya dola ya Marekani imezidi kuporomoka na kufikia kiwango cha chini zaidi katika kipindi cha miaka mitatu.

Dola moja ya Marekani kwa sasa ni wastani wa Shilingu 2,350 za Tanzania.
Mara ya mwisho kwa kiwango hicho kufikiwa ilikuwa ni Julai 2015 ambapo Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliingilia kati.

Je ungependa serikali iingilie kati ilikuzuia mfumko wa bei za bidhaa muhimu kama chakula mafuta na nishati ?
Screenshot_20181123-102914.jpeg
 
Rappa Tekashi 6ix9ine amekamatwa na maafisa wa kupambana na uuzaji wa sigara na vileo kwa magendo wa jimbo la New York kwa tuhuma za kumiliki silaha bila kibali na kufanya biashara ya magendo.

Rappa huyo mwenye umri wa miaka 22 ambaye jina lake rasmi ni Daniel Hernandez anakabiliwa na kifungo kirefu gerezani baada ya kukiuka masharti ya kifungo chake cha nyumba
Screenshot_20181123-103022.jpeg
 
Wavuvi 16 raia wa Tanzania wameachiwa huru na mahakama moja nchini Kenya .Mahakama ya Migori imewashauri waombe vibali kwa mujibu wa mtandao wa Citizen ilikuepuka kukamatwa tena.

Majuma mawili yaliyopita wavuvi 36 kutoka Kenya walikamatwa na maafisa wa usalama wa Tanzania. Wavuvi hao bado wako kizuizini Tanzania.
Screenshot_20181123-103514.jpeg
Screenshot_20181123-103459.jpeg
 
“Msitoe mimba tena nchini Kenya ni haramu.”
Bodi ya madaktari KPMDU imezuia shirika lisilo la kiserikali la Marie Stopes kutoa huduma zozote zinazohusu utoaji mimba kwani inakiuka sheria za nchi.

Bodi ya madaktari inasema ilifikia uamuzi huo baada kuchunguza malalamiko kuwa matangazo ya Marie Stopes yalikuwa yanaunga mkono utoaji mimba.

Utoaji mimba ni haramu nchini Kenya na huruhusiwa tu ikiwa mwanamke yuko hatarini.
Marie Stopes inasema inahudumu kuambatana na sheria, kwa kutoa ushauri na huduma baada ya utoaji mimba.
Screenshot_20181123-103750.jpeg
 
Rappa Tekashi 6ix9ine amekamatwa na maafisa wa kupambana na uuzaji wa sigara na vileo kwa magendo wa jimbo la New York kwa tuhuma za kumiliki silaha bila kibali na kufanya biashara ya magendo.

Rappa huyo mwenye umri wa miaka 22 ambaye jina lake rasmi ni Daniel Hernandez anakabiliwa na kifungo kirefu gerezani baada ya kukiuka masharti ya kifungo chake cha nyumbaView attachment 943589
Hadi wewe unamjua huyu dogo 69 tekashi??
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom