Makapuku Forum

Makapuku Forum

.
Screenshot_20181110-062223.jpeg
 
Darubini ya Hubble Space yaonesha galaksi yetu ya Milky Way inakuja kugongana na galaksi ya Andromeda ambayo ndiyo galaksi pekee iliyokuwa karibu na sisi kwa umbali wa miaka milioni 2.5 ya mwanga.

Andromeda kwa sasa inakuja kwa kasi ya maili 250,000 kwa saa na wanafalaki wamekadiria ndani ya miaka bilioni 3.5 kutokea sasa (kama ukiwa na bahati kufika huko) Andromeda itakumbana na kuungana na galaksi yetu ya Milky Way katika tukio la kihistoria, kama kuna binadamu watakao kuwepo kipindi hicho wataona anga ambayo hawajawahi kuiona maishani mwao anga itabadilika na kuwa kama kwenye picha inavyoonekana hapo.

Ila vita kati ya galaksi hizi mbili itaendelea mpaka pale shimo jeusi kubwa (Supermassive Black Hole) lililokuwa katikati ya Andromeda litakapokutana na shimo jeusi kubwa lililokuwa katikati ya galaksi yetu ya Milky Way (Sagittarius A*) mashimo hayo yataungana na kuunda galaksi nyingine mpya na hapo ni baada ya miaka bilioni 6 kwa sababu galaksi zinachukua muda mrefu sana mpaka kuungana na huenda kipindi hicho Dunia yetu itakuwa haipo tena kwa sababu Jua litakuwa limeshaimeza ndani ya miaka bilioni 5 kutokea sasa.
Screenshot_20181110-062604.jpeg
 
Serikali ya Tanzania imetishia kufuta leseni za wafanyabiashara wa korosho, iwapo ndani ya siku 4 hawatatoa idadi kamili ya korosho watakazonunua.


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka wanunue zao hilo kutoka kwa wakulima kwa bei ‘waliokubaliana’ ya shilingi 3,000 kwa kilo
wala sio bei iliyoporomoka ya kati ya Sh1,900 mpaka Sh2,700 za Tanzania .
Je nani atamnusuru mkulima wa Korosho?
Screenshot_20181110-062810.jpeg
 
Waasisi wa hekalu la Kishetani wameenda mahakamani kudai fidia ya dola milioni 50 kutoka kwa watengenezaji wa filamu ya “The Chilling Adventures of Sabrina”
kwa kosa la kutumia nembo ya miungu wao ya Baphomet.

Netflix na Warner Bros wamekataa mauliko wa kulizungumzia hilo.
Hekalu hilo la kishetani haliamini uwepo wa nguvu za giza ila linahubiri ukarimu na huruma kwa wote.
Screenshot_20181110-062911.jpeg
 
Ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR yenye umbali wa kilomita 472 nchini Kenya umenufaishwa na mkopo wa dola bilioni 3.2 kutoka kwa serikali ya China .

Kiwango ambacho baadhi ya wakenya hasa wanasiasa wa upinzani walidai kiko juu sana ikilinganishwa na reli ya kilomita 756 ya Ethiopia iliyogharimu dola bilioni 3.4. Je inaleta faida au hasara?
Screenshot_20181110-063012.jpeg
 
Mamia ya wenyeji wa vijiji vilivyoko karibu na mto kwenye mpaka wa Botswana na Namibia wana kila sababu ya kutabasamu.

Waliamka asubuhi na kugundua mizoga ya nyati imetapakaa mtoni.
Uchunguzi wa awali unaashiria kuwa wanyama hao walikuwa wakifukuzwa na simba usiku, wakakimbilia mtoni. Inakisiwa kuwa nyati 400 walitumbukia mtoni.

Wenyeji walionekana wakiopoa mizoga ya nyati na kuichuna.
Wengine walikuja na “pick up” na lori kubeba nyama . Je hii minofu ni salama kwao kula ?
Screenshot_20181110-063131.jpeg
 
Tanzania inakabiliwa na mashauri 13 yaliyofunguliwa katika mahakama mbalimbali nje ya nchi. Jumla ya madai katika mashauri hayo yote ni USD 185,580,009.76.
Screenshot_20181110-063337.jpeg
 
Mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwaka unaoishia Oktoba, 2018 umepungua hadi asilimia 3.2 kutoka 3.4 kwa mwaka unaoishia Septemba. Kupungua huko kumechangiwa hasa na kupungua kwa bei za baadhi ya bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa kipindi kinachoishia Oktoba.
Screenshot_20181110-063453.jpeg
 
Serikali ya Tanzania imetishia kufuta leseni za wafanyabiashara wa korosho, iwapo ndani ya siku 4 hawatatoa idadi kamili ya korosho watakazonunua.


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka wanunue zao hilo kutoka kwa wakulima kwa bei ‘waliokubaliana’ ya shilingi 3,000 kwa kilo
wala sio bei iliyoporomoka ya kati ya Sh1,900 mpaka Sh2,700 za Tanzania .
Je nani atamnusuru mkulima wa Korosho?View attachment 928308
Binamu ashakuleteaa korosho kwelii make kajichimbia huko
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom