Makapuku Forum

Makapuku Forum

Unalikumbuka gari lililorushwa na Elon Musk nje ya Dunia. Kwa sasa gari hilo pamoja na mdoli aliyekuwa ndani tayari limeshafika kwenye sayari ya Mars.

Watafiti wanasema kunauwezekano wa asilimia 6 gari hilo kuja kudondokea Duniani ndani ya miaka milioni 1 ijayo au linaweza likadondokea kwenye sayari ya Venus.
Screenshot_20181108-145217.jpeg
 
Maisha yetu hapa Duniani yangekuwa hatarini kama isingekuwepo sayari ya Jupiter. Sayari hiyo inamchango mkubwa sana katika kuilinda Dunia yetu dhidi ya mawe makubwa pamoja na vimondo vinavyoingia kwenye njia ya Dunia.

Kani kubwa ya uvutano iliyokuwa kwenye Jupiter inasaidia kusafisha njia ya Dunia yetu kwa kuondoa mawe na vimondo ambavyo vingeweza kuigonga Dunia na kusababisha hatari kubwa.

Kwenye picha unaweza ukaona madoa ya brown, hayo ni baadhi ya mawe makubwa yaliyokuwa yanaelekea Duniani lakini yameishia kuvutwa kwenye Jupiter. Hivyo Jupiter ni kama kaka mkubwa ambaye anamlinda mdogo wake ambaye ni Dunia dhidi ya mawe makubwa japokuwa mwaka 1770 kuna jiwe moja kubwa lilisukumwa na Jupiter kuelekea kwenye njia ya Dunia ila lilipita umbali wa maili milioni 1 na Dunia.
Screenshot_20181108-145319.jpeg
 
Wafanyakazi wawili wa kamati ya Kimataifa ya Kuwalinda Waandishi wa Habari CPJ, Angela Quintal na Muthoki Mumo wameachiliwa baada ya kuzuiliwa Tanzania.

Wanadaiwa kukamatwa na Idara ya Uhamiaji Tanzania kutoka hotelini Dar es Salaam ambapo vitu vyao vilikaguliwa na pasi zao za kusafiria kuchukuliwa.
Screenshot_20181108-145712.jpeg
 
Mwanaharakati wa haki za wanawake nchini Uganda Stella Nyanzi amefikishwa mahakamani kwa kumtusi rais Yoweri Museveni wa Uganda.

Nyanzi ambaye alikamatwa mwishoni mwa juma lililopita ameshtakiwa kwa matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii pamoja na kusambaza maandishi yaliyolenga kushusha hadhi ya rais Museveni pamoja na mamake.
Screenshot_20181108-145844.jpeg
 
Rais wa Marekani Donald Trump amemfuta kazi Jeff Sessions kama mwanasheria mkuu.

Sessions alijipata katika njia panda alipojiondoa kutoka kwenye uchunguzi wa madai dhidi ya Urusi.

Idara ya ujasusi inaamini kwamba udukuzi unaodaiwa kufanywa na Urusi dhidi ya mgombea wa urais wa chama cha Democrat Hillary Clinton ulifanywa ukiwa na lengo la kumsaidia bw Trump kumshinda Clinton
Screenshot_20181108-145949.jpeg
 
Kwa mara ya kwanza, wanawake wawili waislamu, katika jimbo la Michigan Rashida Tlaib na wa jimbo la Minnesota Ilhan Omar wamechaguliwa katika bunge la Marekani.

Bi Omar, mwenye umri wa miaka 36, ndiye mbunge mwenye umri mdogo zaidi kuwahi kuchaguliwa bungeni.

Mbunge huyu alihamia Marekani akiwa na umri mdogo kutoka Kenya alikoishi kama mkimbizi kutoka Somalia
Screenshot_20181108-150115.jpeg
 
Serikali ya Nepal imetenga “sikukuu ya mbwa“ ama kwa lugha ya kihindi “Kukur Tihar” ilikumuenzi rafiki huyu wa binadamu.

Katika siku hii mbwa wanaenziwa na kubarikiwa kwa alama nyekundu ama Tika kwenye paji la uso. Samahani sijataja vyakula vya aina mbali mbali minofu na maua .

Wahindi wanaamini kuwa mbwa ni mjumbe wa mungu wao wa kifo Yamaraj kwa hivyo ukimtunza vyema mbwa naye Yamaraj atakutendea wema.

Screenshot_20181108-150229.jpeg
 
Wasimamizi katika kampuni moja ya kichina wamefungwa jela kwa kati ya miaka 5- 10 baada ya kuwaadhibu wafanyakazi walioshindwa kufikia malengo ya mauzo kibiashara na kuwalazimisha kunywa mkojo na pia kula mende.

Gazeti la Morning Post limearifu kuwa mameneja hao 3 walionekana wakiwachapa wafanyakazi na
kuwalazimisha kunywa mikojo.
Screenshot_20181108-150406.jpeg
 
Chama cha rais Donald Trump, Republicans kimepoteza wingi katika bunge la Congress hali ambayo itafanya muda uliosalia wa urais wa Trump kupitia wakati mgumu zaidi.

Republicans pia wamepoteza viti saba vya Ugavana mpaka sasa. Hata hivyo chama hicho kimefanikiwa kubaki na wingi katika bunge la Seneti.

Kwenye uchaguzi wa bunge la Congress, mpaka sasa majimbo 412 yametangaza matokeo. Democrats wanaongoza kwa viti 219 huku Republicans wakifuatia na viti 193.
Screenshot_20181108-150514.jpeg
 
Katika jamii ya Pokot upangaji uzazi kwa watoto umekuwa ukifanywa tangu jadi.

Jamii hii 'humfunga' mtoto wa kike kupitia tambiko ili kumzuia kupata mimba punde tu msichana anapoanza kupata hedhi.

Licha ya Kenya kupiga hatua kubwa kuimarisha afya ya mama na mtoto jamii hii imedumisha mbinu hii ya kitamaduni.

Nimeipenda kwakweli vizuri sana
Screenshot_20181108-150631.jpeg
 
Huzuni imekumba mji wa Uvalde ulioko Texas Marekani baada ya Bwana na Bi harusi walioabiri helikopta kutoka eneo la harusi yao wakielekea kwa fungate kuangamia chini ya saa moja baada ya kuunganishwa na kuwa mke na mume.

Jamaa na marafiki waliohudhuria harusi yao mjini Texas wamesalia na huzuni tele baada ya kupata habari helikopta iliyokuwa imewabeba
Will Byler na mkewe Bailee Ackerman Byler ilianguka dakika chache tu baada ya kupaa.

Wawili hao walikuwa wanafunzi wa mwaka wa mwisho wa chuo kikuu cha Sam Houston State University.
Kilichosababisha ajali hii bado kinachunguzwa.
Screenshot_20181108-150809.jpeg
 
Mwanaharakati wa haki za wanawake nchini Uganda Stella Nyanzi amefikishwa mahakamani kwa kumtusi rais Yoweri Museveni wa Uganda.

Nyanzi ambaye alikamatwa mwishoni mwa juma lililopita ameshtakiwa kwa matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii pamoja na kusambaza maandishi yaliyolenga kushusha hadhi ya rais Museveni pamoja na mamake.View attachment 926127
Mtukufu m7
 
Katika jamii ya Pokot upangaji uzazi kwa watoto umekuwa ukifanywa tangu jadi.

Jamii hii 'humfunga' mtoto wa kike kupitia tambiko ili kumzuia kupata mimba punde tu msichana anapoanza kupata hedhi.

Licha ya Kenya kupiga hatua kubwa kuimarisha afya ya mama na mtoto jamii hii imedumisha mbinu hii ya kitamaduni.

Nimeipenda kwakweli vizuri sanaView attachment 926143
Tuliambiwa tufyatue tuu elimu bure
 
Unalikumbuka gari lililorushwa na Elon Musk nje ya Dunia. Kwa sasa gari hilo pamoja na mdoli aliyekuwa ndani tayari limeshafika kwenye sayari ya Mars.

Watafiti wanasema kunauwezekano wa asilimia 6 gari hilo kuja kudondokea Duniani ndani ya miaka milioni 1 ijayo au linaweza likadondokea kwenye sayari ya Venus. View attachment 926120
Inabidi kaka Jupiter alidake hilo gari lisituharibie shughuli huko mbeleni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom